Nini maana ya ndoto hii?

Nevergive up

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2024
Posts
569
Reaction score
884
Nimeota niko ndani ya nyumba nimefungiwa siwezi kutoka yani kifupi nimetekwa lakni nilikuwa natafuta kila siku njia ya kutoroka nakosa lakini akaja mgeni ndani kumbe hajui kama nimetekwa pale

Basi nikamuomba anifungulie mlango nilisingizia kuna mtu ananiita nje baada ya kunifungulia nikaanza kukimbia lkn ile natoka nje nakutana na giza sana nje kiasi kwamba sioni njia lkn wakati nakimbia hivyohivyo ghafla

Nikaona mtu mbele yangu akingaa sana kama taa akiwa anakimbia mbele yangu kwahyo nikawa naona njia vzr huku nakimbia ,tumekimbia sana nikimfata mtu yule hadi kulipopambazuka ndipo akanionesha njia ya kupita na nikamshukuru na hapohapo usingizi akaisha nikazinduka
 
Kuota unakimbia ni dalili kuna roho ya umauti inakufuatilia,,,,fanya ibada toa swadaka
 
Tafsiri ya haraka usiwe muongo saana sehemu yako ya Kazi hasa.

Utakutana na watu tofauti nyakati tofauti usiwaeleze kuhusu Maisha yako ila wewe angalia mambo Yao Tu Wala usitangaze yaani usiwe mbeya kwenye mambo ya watu.

Kuona njia utapata akili ya kuanzisha Jambo jipya kupitia watu lakini litachukuwa Muda hadi kulifanikisha.
 
Mkuu kukimbia na uongo mbona vitΓΉ 2 tofauti
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…