Zee la Hekima umeongea vizuri sana. Ila kuna ishu ndogo hujaizingatia. Msukule kama dhana, hakuna mwenye ubishi nayo. Lakini ukitafuta istilahi Msukule katika lugha ya Kiingereza, hapo ndipo tunaachana. Ni lazima ufahamu kuwa lugha ni sehemu muhimu wa UTAMADUNI wa watu. Na Utamaduni mmoja unatofautiana na mwingine! Kwa hiyo itoshe tu kusema, kwa Utamaduni wa mkusanyiko wa makabila ya Wabantu (Kiswahili inclusive) neno Msukule linafahamika. Ila kwa Utamaduni wa kiinglish ni suala tete!