Nini maana ya 'kupandishwa cheo' kwa watuhumiwa wa ujambazi?

Malisa Godlisten

JF-Expert Member
Jan 20, 2010
201
1,534
Kauli ya Rais kuwa watuhumiwa wa ujambazi wanaokamatwa na silaha wasipelekwe mahakamani bali "wapandishwe cheo" ina maana gani? Nini maana ya "kupandishwa cheo" kwa mtuhumiwa wa ujambazi?

1. Kusamehewa
2. Kuuawa
3. Kunyang'anywa silaha
4. Kutubu
5. Mengineyo...

Na kwanini "Rais wetu mwema" asingesema "wapandishwe cheo" baada ya Mahakama kudhibitisha tuhuma zao? Ina maana Rais wetu hana imani na mahakama?? Kuruhusu Polisi "kupandisha cheo" watuhumiwa wa ujambazi sio kukiuka utawala wa sheria?

Je Rais haoni kwa kauli yake hiyo atasababisha watu wengi wasio na hatia "kupandishwa cheo" kwa kusingiziwa tu ujambazi?? Yani Polisi kama ana kisa na wewe anakubambikizia tu silaha kisha "anakupandisha cheo" bila kukufikisha mahakamani. Je huku si kukiuka misingi ya haki za binadamu na utawala bora?

Unakumbuka wale wafanyabiashara wa Ulanga "waliopandishwa cheo" kwa kusingiziwa ni majambazi na Kamanda Zombe lakini baadae ikaja kubainika kuwa hawakuwa majambazi?? Kwanini Rais ameruhusu Polisi "wapandishe watu vyeo" kwa tuhuma tu, wakati mahakama zipo??

Malisa G.J
 
Nimefurahishwa na neno kupandishwa cheo.....kumbe ndio maana yake!!! Dk Mwakyembe alipandishwa cheo...akakana thesis yake ya udaktari...mzee wetu Lubuva alipandishwa cheo tukaona HAKI inavyotendeka ktk zoezi LA kuhesabu kura....na tukaona zoezi zima likirushwa live na vituo vyote has a TBC!! Taifa....mzee wetu Zanzibar alipandishwa cheo...akasimamia kwa HAKI uchaguzi Zanzibar.....msululu ni mrefu...mzee wangu Kova akiwa RPC dar huku flowmeter ya TPA ikichepusha mafuta nje ya hazina ya serikali kwa miaka 5 Akasitaafu kwa heshima na Gwaride kule Moshi...asante malisa kwa kuniongezea msamiati...Heri chief Mangungu hakuwa anajua anachosaini kuliko profesa Wa sasa anae vaa miwani ya MBAO mchana kweupe....sababu ya NJAAA
 
Mkuu hata mimi nimeiona hiyo. Na ninadhani Rais ajaribu kuwa makini kwa kauli zake. Ataliangamiza taifa. Tafsiri ya haraka haraka niliyoipata ni kwamba Rais amewapa polisi mamlaka ya kuuwa watuhumiwa wa ujambazi. Hii ni hatari sana, Polisi wetu tunawajua walivyo, Polisi wamekuwa wakibambikia watu kesi.

Kwa kauli hiyo polisi akiwa na bifu na wewe anakupiga risasi kwa kisingizio cha ujambazi na kutoa taarifa kuwa jambazi lenye silaha limekimbia kusikojulikana na tunaendelea kulisaka. Kauli kama hizi kutolewa na kiongozi wa nchi siyo vizuri na ni hatari sana. Rais anaweza kuwa anafanya vizuri lakini kumbe anatengeneza matatizo katika jamii. Polisi ni ndugu zetu, jamaa zetu, tunaishi nao nyumba moja za kupanga, tunakunywa nao bar moja n.k.

Tuna wafahamu vizuri, tunafahamu namna hawa hawa polisi wanavyoshirikiana na majambazi, tunafahamu namna polisi hawa hawa wanavyokodisha silaha kwa majambazi. Je, leo hii polisi wamekuwa waadilifu kiasi gani mpaka Rais anawapa mamlaka ya kuuwa mtu yeyote? Naomba nieleweke kuwa sitetei majambazi, lakini wasiwasi wangu ni kwamba kuna watu watauwawa kwa kusingiziwa majambazi. Kama polisi wanadiliki kutoa silaha kwa majambazi, je watashindwa kuua kwa kisingizio kuwa huyu mtu alikuwa jambazi na alikuwa akijiandaa kwenda kufanya uharifu?

Rais kabla ya kutoa kauli kama hizi tafakari kwanza.
 
Kupandishwa cheo kumuweka mbali na binadamu, mimea, wanyama na umbile la juu la uso wa dunia. Hiyo ni tafsida maalumu kuashiria kwamba hakuna jambazi anayeua raia atakayebakishwa hai.
Pamoja na kwamba uongozi wa sheria ndiyo kila kitu sometimes ukatili unahitajika ili kudhibiti matukio ya kihalifu, shida itakuwa kubwa endapo kutakuwa na kuzungukana miongoni wa maofisa wenyewe katika kudhibiti ujambazi
 
Kauli ya Rais kuwa watuhumiwa wa ujambazi wanaokamatwa na silaha wasipelekwe mahakamani bali "wapandishwe cheo" ina maana gani? Nini maana ya "kupandishwa cheo" kwa mtuhumiwa wa ujambazi?

1. Kusamehewa
2. Kuuawa
3. Kunyang'anywa silaha
4. Kutubu
5. Mengineyo...

Na kwanini "Rais wetu mwema" asingesema "wapandishwe cheo" baada ya Mahakama kudhibitisha tuhuma zao? Ina maana Rais wetu hana imani na mahakama?? Kuruhusu Polisi "kupandisha cheo" watuhumiwa wa ujambazi sio kukiuka utawala wa sheria?

Je Rais haoni kwa kauli yake hiyo atasababisha watu wengi wasio na hatia "kupandishwa cheo" kwa kusingiziwa tu ujambazi?? Yani Polisi kama ana kisa na wewe anakubambikizia tu silaha kisha "anakupandisha cheo" bila kukufikisha mahakamani. Je huku si kukiuka misingi ya haki za binadamu na utawala bora?

Unakumbuka wale wafanyabiashara wa Ulanga "waliopandishwa cheo" kwa kusingiziwa ni majambazi na Kamanda Zombe lakini baadae ikaja kubainika kuwa hawakuwa majambazi?? Kwanini Rais ameruhusu Polisi "wapandishe watu vyeo" kwa tuhuma tu, wakati mahakama zipo??

Malisa G.J
Chauongo hivi unafikiri uliyesikia ni wewe peke yako? Kilichosemwa ni kuhusu askari kumnyang'anya jambazi bunduki. Kwamba huyu askari waliyofanyahivyo wasipelekwe mahakamani bali wapandishwe cheo. Tatizo nini?
 
Kauli ya Rais kuwa watuhumiwa wa ujambazi wanaokamatwa na silaha wasipelekwe mahakamani bali "wapandishwe cheo" ina maana gani? Nini maana ya "kupandishwa cheo" kwa mtuhumiwa wa ujambazi?

Malisa G.J

Kwakua mmezoea kupinga kila kitu sasa mmeamua kutunga uwongo ili mpate simpaty kwa wananchi. Nimeisikiliza clip yote hakuna sehemu ambapo Raisi katamka kua watuhumiwa wa ujambazi wapandishwe cheo. alichokitamka Raisi ni kua yule askari atakayejitoa mhanga kuinyang"anya silaha haraka haraka apandishwe cheo
 
Chauongo hivi unafikiri uliyesikia ni wewe peke yako? Kilichosemwa ni kuhusu askari kumnyang'anya jambazi bunduki. Kwamba huyu askari waliyofanyahivyo wasipelekwe mahakamani bali wapandishwe cheo. Tatizo nini?

Kwakua wamezoea kupinga kila kitu ni shidaa mkuu
 
Halafu hii JF tutakuja sasa kuwashitaki kwa kuruhusu hizi kauli za upotoshaji kuwekwa humu. Nyie endeleeni tu kuziachia. Tupo serious na maendeleo halafu mnaruhusu hizi kauli za uongo na upotoshaji.
 
VIONGOZI WA DINI MNANYAMAZA TU HAYA NDIYO YA KUYASEMEA. MTALAUMIWA NA MUMGU! WATU WATAUAWA MAANA KESHA TOA AMRI "WAWAPANDISHE CHEO"
Mwanakwetu haya kwetu no mageni. Lakin tunashukuru sana kwa kutuongezea matumizi mbadala ya maneno. Waalimu nao waanze kupandisha vyeo wanafunzi watukutu.
 
Sikiliza vizuri sana! Rais amekosea jinsi ya kueleza! Kama alikuwa anamaanisha kupandisha cheo askari amekosea sana kujieleza! Kosa lile lile awe anasoma! Hana uwezo kuelezea bila kusoma! Labda baada ya muda sana!anajichanganya!!! Askari wataua sana raia wasio na hatia kwa kukurupuka kwake kuwapandisha cheo!Tamko hili na lile lingine la kuwapa Milions ya mapema lipi ndio lipi? Maana sasa yatakinzana!! Lile la Makonda hili la JPM! Wote wakurupukaji!
 
Kwakua wamezoea kupinga kila kitu ni shidaa mkuu
Na hiki ndicho kinawaharibia. Si kila nafsi hupenda kusikia uongo. Ndio maana hata watu wao bungeni wamefika watatu wanaadhibiwa kwa kusema uongo na kushindwa kuufuta kwa aibu.
 
Wazee hiyo ndio order ya ' Extrajudicial killing' imetoka hivyo, as simple as that.
Yaani maana yake kwa ufupi kabisa ni kuwa Rais ametoa ruksa kwa vyombo vya usalama kuua mtu yoyote anahisiwa kuwa jambazi bila kufuata utaratibu wa mahakama. NUKTA
wasiwasi wangu mimi ni kuwa uzoefu umeonyesha kuwa extrajudicial killing hufanyika;
1. Kwenye tawala za kiimla ambapo maneno ya mtawala ndio sheria.
2. Ina tabia ya kuwalenga zaidi viongozi wa siasa, watu wanaopinga mawazo ya watawala na watu walioko kwenye taasisi za kiraia zinazotoa sauti dhidi ya uonevu wa raia.
Sasa ukiunganisha hizi picha;
1. Kuminywa kwa uhuru wa kujieleza.
2. Makatazo dhidi ya shughuli za kisiasa.
3. Mhimili wa bunge kuongozwa na serikali kuu.
4. Bunge kuhoji hukumu ya mahakama.
5. Kufungiwa kwa vyombo vya habari na wanahabari kuburuzwa kortini.
6. Tamko la kuruhusu extrajudicial killing.
Utaona kama kuna fumbo limekaribia kutimia, limekosa tu vipande vichache. Na kwa speed tunayoenda nayo vitakamilika.
Kama unaipenda Tanzania ndugu yangu, ONGEA SASA au NYAMAZA MILELE.
 
Nchi inapokosa uongozi mzuruna makini ni shida sana.Leo tunaongozwa na kiongozi ambaye ni dikteta hajui kuchunga kauli sake. Watendaj wake nao no mabomu yanayosubiri kulipuka baada ya muda.

IPO hatar ya Tanzania kurudi nyuma kimaendeleo Sikh za usoni.

Nitawashangaa sana tune ya haki za binadam wakilifumbia macho swala kama hili.
 
Back
Top Bottom