Nini maana ya Azimio la Zanzibar?

Nini maana ya Azimio la Zanzibar?

Naomba mneno haya yatafsiri matendo. Azimio hili likishindikana kuwekwa ktk vitendo wabakaji wa katiba na demokràsia watavimba kichwa.
 
Mikutano kwenye majimbo yenu inaruhusiwa lakini hamfanyi.

Si mbowe ,zito, mdee wala mnyika anayefanya mkutano jimboni kwake wakati mnaruhusiwa.kwa nini?
Yani hapa umepiga penyewe! kwanini kwenye majimbo yao hawafanyi?
 
Hili AZIMIO LA Zanzibar lifuatiwe na azimio jingine huko Pemba la kuunganisha vyama na kupanga mikakati ya kujipanga na Uchaguzi.
 
Nini maana ya Azimio la Zanzibar?

Vyama 6 vya Upinzani nchini vimetoa maazimio kadhaa mazito Kuhusu hali ya Demokrasia ya vyama vingi nchini Tanzania. Kwa ujumla maazimio hayo yanaitwa Azimio la Zanzibar. Maana yake nini?

Maana yake ni Kwamba Vyama vya Upinzani nchini vinachukizwa na vitendo vinavyofanywa na Serikali ya Rais Magufuli dhidi ya Viongozi, wanachama na wafuasi wa Vyama vyao kwa kuwafungulia kesi na kuwasweka magerezani. Kuwatangaza Freeman Mbowe na Esther Matiko kuwa wafungwa wa kisiasa Maana yake ni kuiambia dunia kuwa nchini Tanzania sasa watu wanafungwa kutokana na imani zao za kisiasa. Kesi iliyowaweka mahabusu Mbowe na Matiko inaangukia kwenye tafsiri ya Wafungwa wa Kisiasa Kwa mujibu wa Shirika la Amnesty International. Hivyo wanapaswa kuachiwa mara moja. Hii ni mara ya pili kwa wanaharakati za kisiasa nchini kutambua wenzao kama ‘political prisoners’. Mara ya kwanza ilikuwa Mwaka 1991 ambapo Kamati ya Mageuzi ( NCCR ) Katika Mkutano wake wa kidemokrasia ilimtangaza Maalim Seif Shariff Hamad kuwa ni mfungwa wa kisiasa. Serikali ilimwachia huru mara baada ya Tamko hilo.

Freeman Mbowe na Esther Matiko watakuwa ni alama ya mapambano dhidi ya ukandamizaji wa haki za Watu.

Vyama vimeamua kudharau amri batili ya Rais John Magufuli kuzuia mikutano ya hadhara. Hivyo Mwaka 2019 Vyama vitaanza kufanya mikutano ya hadhara kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi bila kujali agizo la Rais. Huu ni uamuzi wa kimapinduzi uliochelewa, uamuzi wa kukataa kutii amri batili isiyoheshimu Katiba na Sheria za nchi. Kwa uamuzi huu Vyama vimeamua kupigania Demokrasia kwa vitendo na kuendesha kampeni ya kuheshimu Katiba inayoruhusu Vyama kufanya mikutano. Kwa ufupi Vyama vimetangaza vita dhidi ya udikteta. Kamati ya Pamoja ya Vyama itatangaza ratiba ya kuanza kwa mikutano ya hadhara kwa mujibu wa sheria mara baada ya Vyama kuidhinisha ( ratification) Azimio la Zanzibar kwenye vikao vyao na kuwasilisha nyaraka ( instruments of ratification) kwenye Kamati hiyo.

Vyama vimesisitiza kuwa havitambui Serikali ya Zanzibar chini ya Ali Mohammed Shein. Vinataka haki ya Wazanzibari kuchagua Viongozi wanaowataka iheshimiwe. Vyama vitachukua kadhaa kuhakikisha kuwa Zanzibar inapata Serikali iliyochaguliwa na Wananchi wa Zanzibar Oktoba 25, 2015.

#AzimioLaZanzibar limesema SASA BASI. IMETOSHA. AZ limetangaza vita itakayoweka misingi ya kuheshimiana miongoni mwa Viongozi na Kati ya Viongozi na Wananchi. Misingi ya Demokrasia ya kweli na kuondoa udikteta Tanzania.
Jinsi ya kutatua matatizo matatu ya Mwl. Nyerere (Ujinga, Umasikini na Maradhi) - JamiiForums
 
Mikutano kwenye majimbo yenu inaruhusiwa lakini hamfanyi.

Si mbowe ,zito, mdee wala mnyika anayefanya mkutano jimboni kwake wakati mnaruhusiwa.kwa nini?

Chadema ni washamba wa kisiasa na mtandanganya wajinga wenzenu tu
Acha ufala kenge wewe! Na wale wanasiasa wasio na majimbo wakafanyie wapi siasa?
 
Mikutano kwenye majimbo yenu inaruhusiwa lakini hamfanyi.

Si mbowe ,zito, mdee wala mnyika anayefanya mkutano jimboni kwake wakati mnaruhusiwa.kwa nini?

Chadema ni washamba wa kisiasa na mtandanganya wajinga wenzenu tu
Hapa ndio utaona tuna wanasiasa WAPUMBAVU. Yaani zito jimboni kwake anaona hamna kiki ila akija kinondoni ndio atapata kiki.Kila mbunge akifanya siasa jimboni kwake shida ni nini?
 
CCM walivyokuwa wapuuzi wanafikiri hii ni kama UKAWA watapandikiza mapandikizi yao safari hii tunawafinya chini kwa chini.
 
Rais wa nchi aliapa kuilinda katiba ya Jamhuri ya Muungano .
Katiba inaruhusu vyama vingi vya siasa,katiba inaruhusu mikutano.
Yeyote anaezuia vyama kufanya kazi zake ni wazi anavyunja katiba.

Azimio la Zanzibar ni kipimo kinachopima vyema kipi kiheshimiwe kati ya tamko la Kiongozi na katiba ya nchi.

Msiparaganyike kwa kugawiwa kwa fedha na vyeo,mmeamua kusimama pamoja ,simameni ilimradi hamvunji sheria
 
AZIMIO LA ZANZIBAR, ni makubaliano kati ya watu wa Marekani na vibaraka wa karne ya 21 wanaoishi Tanzania kwa manufaa ya watu wa Marekani.
Azamio la Zanzibar linalenga kulinda katiba.

Kulinda kariba sio kulinda isichanwe au isiibiwe,bali ni kuhakikisha kila kilichotajwa ndani ya katiba kinaenda kama katiba ilivyotaja.
Mikutano ya vyama vya siasa popote ndani ya jamhuri ya muungano ni takwa la kikatiba.

Ni haki iliyotajwa ndani ya katiba,yeyote anaepinga mikutano na kazi za vyama vya siasa ni wazi anavunja katiba.
Wanasheria watusaidie adhabu ya mtu anaevunja katiba,maana kariba ndio sheria mama wa sheria zote ,na sheria yoyote inayopingana na katiba basi sheria hiyo ni batili.
 
Asiejua maana haambiwi maana. "TAMKO LA KUWATAJA MH MBOWE NA MATIKO KUWA WAFUNGWA WA KISIASA" Kwa wanaoelewa Diplomasia basi ni jambo kubwa mno.

Acha tuone hizo Busara za Mfumo ( System) kama zipo.
 
Maaalim ccm damu..wewe hapo ccm.damu...alafu mnatuhadaa hapa

hawa wana nia ya kumfunga mzee Hashim Lungwe, maana kwenye hilo kundi yeye ndio mpinzani pekee

Lowassa waziri mkuu wa zamani hawezi kua mpinzani

Mzee wa mama Tanzania aliwahi kupewa ubunge na kikwete(ccm), upinzani ameanza lini?

Seif Sharif Hamad huyu alikua kibaraka wa mda mrefu wa mchonga hawezi kua mpinzani

Zitto zuberi kabwe huyu hata wenzake chadema wanajua si mpinzani huyu

Labda mzee Lungwe, nae nasema labda

Hii nchi kuna wapinzani kweli ila si hili kundi lililokutana Zanzibar.
 
Rais wa nchi aliapa kuilinda katiba ya Jamhuri ya Muungano .
Katiba inaruhusu vyama vingi vya siasa,katiba inaruhusu mikutano.
Yeyote anaezuia vyama kufanya kazi zake ni wazi anavyunja katiba.

Azimio la Zanzibar ni kipimo kinachopima vyema kipi kiheshimiwe kati ya tamko la Kiongozi na katiba ya nchi.

Msiparaganyike kwa kugawiwa kwa fedha na vyeo,mmeamua kusimama pamoja ,simameni ilimradi hamvunji sheria
qRI8Gs7.gif
 
Rais wa nchi aliapa kuilinda katiba ya Jamhuri ya Muungano .
Katiba inaruhusu vyama vingi vya siasa,katiba inaruhusu mikutano.
Yeyote anaezuia vyama kufanya kazi zake ni wazi anavyunja katiba.

Azimio la Zanzibar ni kipimo kinachopima vyema kipi kiheshimiwe kati ya tamko la Kiongozi na katiba ya nchi.

Msiparaganyike kwa kugawiwa kwa fedha na vyeo,mmeamua kusimama pamoja ,simameni ilimradi hamvunji sheria
Nendeni mahakamani
 
  • Thanks
Reactions: mmh
Nini maana ya Azimio la Zanzibar?

Vyama 6 vya Upinzani nchini vimetoa maazimio kadhaa mazito Kuhusu hali ya Demokrasia ya vyama vingi nchini Tanzania. Kwa ujumla maazimio hayo yanaitwa Azimio la Zanzibar. Maana yake nini?

Maana yake ni Kwamba Vyama vya Upinzani nchini vinachukizwa na vitendo vinavyofanywa na Serikali ya Rais Magufuli dhidi ya Viongozi, wanachama na wafuasi wa Vyama vyao kwa kuwafungulia kesi na kuwasweka magerezani. Kuwatangaza Freeman Mbowe na Esther Matiko kuwa wafungwa wa kisiasa Maana yake ni kuiambia dunia kuwa nchini Tanzania sasa watu wanafungwa kutokana na imani zao za kisiasa. Kesi iliyowaweka mahabusu Mbowe na Matiko inaangukia kwenye tafsiri ya Wafungwa wa Kisiasa Kwa mujibu wa Shirika la Amnesty International. Hivyo wanapaswa kuachiwa mara moja. Hii ni mara ya pili kwa wanaharakati za kisiasa nchini kutambua wenzao kama ‘political prisoners’. Mara ya kwanza ilikuwa Mwaka 1991 ambapo Kamati ya Mageuzi ( NCCR ) Katika Mkutano wake wa kidemokrasia ilimtangaza Maalim Seif Shariff Hamad kuwa ni mfungwa wa kisiasa. Serikali ilimwachia huru mara baada ya Tamko hilo.

Freeman Mbowe na Esther Matiko watakuwa ni alama ya mapambano dhidi ya ukandamizaji wa haki za Watu.

Vyama vimeamua kudharau amri batili ya Rais John Magufuli kuzuia mikutano ya hadhara. Hivyo Mwaka 2019 Vyama vitaanza kufanya mikutano ya hadhara kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi bila kujali agizo la Rais. Huu ni uamuzi wa kimapinduzi uliochelewa, uamuzi wa kukataa kutii amri batili isiyoheshimu Katiba na Sheria za nchi. Kwa uamuzi huu Vyama vimeamua kupigania Demokrasia kwa vitendo na kuendesha kampeni ya kuheshimu Katiba inayoruhusu Vyama kufanya mikutano. Kwa ufupi Vyama vimetangaza vita dhidi ya udikteta. Kamati ya Pamoja ya Vyama itatangaza ratiba ya kuanza kwa mikutano ya hadhara kwa mujibu wa sheria mara baada ya Vyama kuidhinisha ( ratification) Azimio la Zanzibar kwenye vikao vyao na kuwasilisha nyaraka ( instruments of ratification) kwenye Kamati hiyo.

Vyama vimesisitiza kuwa havitambui Serikali ya Zanzibar chini ya Ali Mohammed Shein. Vinataka haki ya Wazanzibari kuchagua Viongozi wanaowataka iheshimiwe. Vyama vitachukua kadhaa kuhakikisha kuwa Zanzibar inapata Serikali iliyochaguliwa na Wananchi wa Zanzibar Oktoba 25, 2015.

#AzimioLaZanzibar limesema SASA BASI. IMETOSHA. AZ limetangaza vita itakayoweka misingi ya kuheshimiana miongoni mwa Viongozi na Kati ya Viongozi na Wananchi. Misingi ya Demokrasia ya kweli na kuondoa udikteta Tanzania.
Hawa ni vbaraka waliotumwa na mabwana zao wenye wivu na maendeleo ya nchi hii.wanataka kuleta machafuko na hofu kwa wananchi. nina imani serikali itawashughurikia ipasavyo. kama ni mikutano kwenye majimbo yao wameruhusiwa lakini hamfanyi.

Si mbowe ,zito, mdee wala mnyika anayefanya mkutano jimboni kwake wakati mmenaruhusiwa. ni wajinga ndio mtawadanganya kwa hoja zenu dhaifu.
 
Haki,hasa katika utawala wa dikteta,huwa haiombwi bali inapiganiwa.Kwa uamuzi huo,mko sahihi kwa asilimia 100 na tunawaunga mkono.

Wazungu wanasema,"better late than never"
 
Back
Top Bottom