johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 104,319
- 183,598
Wadau naomba kujuzwa maana sahihi ya neno 'kughushi'. Endapo mtu alitumia cheti cha mtu mwingine kuingia sekondari na akasoma mwenyewe hadi chuo kikuu atakuwa ameghushi? Kama ndiyo mnasemaje kwa ambaye hakusoma lakini katumia cheti cha mtu mwingine kupata ajira? au huyu ataitwa mwizi wa cheti? Tafadhali nielimisheni taratibu bila jazba maana tuliosoma enzi za ujamaa kusomea cheti cha mwanakijiji mwenzio kwa faida ya kijiji na taifa haikuwa shida tuliita 'uzalendo'! ahsante.