Nini kimemsibu Anne Kilango?

Nini kimemsibu Anne Kilango?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
2,203
Reaction score
3,321
Huyu mama alijipambanua kama mpambanaji dhidi ya ufisadi na kujizolea tuzo ya mwanamke jasiri zaidi lakini kwa mshangao wa wengi wapiga kura wamemzuia kuingia bungeni nini sababu za kuanguka kwake?
 
huyu mama alijipambanua kama mpambanaji dhidi ya ufisadi na kujizolea tuzo ya mwanamke jasiri zaidi lakini kwa mshangao wa wengi wapiga kura wamemzuia kuingia bungeni nini sababu za kuanguka kwake?

Ni upepo tu, kama ulivyovuma Kahama kwa Lembeli, Nyamagana kwa Wenje, Musoma kwa Vincent, kwa Zambi, kwa Wasira, kwa Lowasa, etc, and same upepo utavuma Arusha mjini kwa Lema.
 
Yeye na failia yake umeshamlipia kutibiwa/kufia India. Wewe utatibiwa/kufia wapi?
 
Sio kwa Lema,kwani Arusha watu hawaitaki CCM kabisa,hats umsimamishe Nape kwa tiketi ya Chadema atapita

Aibu sana hii...mtu wanayemchukia na kumbeza akiwa ccm sasa wamvhague mtu huyo huyo akiwa chadema?
Bonge la aibu.
Ndo hayo hayo yamekosesha watu urais na uspika.
 
Aibu sana hii...mtu wanayemchukia na kumbeza akiwa ccm sasa wamvhague mtu huyo huyo akiwa chadema?
Bonge la aibu.
Ndo hayo hayo yamekosesha watu urais na uspika.

Do you get the logic behind his statement? Au unakurupuka tu?
 
Wiki iliyo pita nilikuwa Same kwenye jimbo la huyo mama nikajaribu kudodosa sababu za kumpiga chini, kubwa kuliko zote nilio kuwa naelezwa ni Dharau, mama alikuwa na dharau ya hari ya juu na kiburi , hivi viwili ndo vilifanya wamsafishe siasa
 
huyu mama alijipambanua kama mpambanaji dhidi ya ufisadi na kujizolea tuzo ya mwanamke jasiri zaidi lakini kwa mshangao wa wengi wapiga kura wamemzuia kuingia bungeni nini sababu za kuanguka kwake?

Nadhan tatizo bado lipo kwetu sisi wapiga kura hasa wa vijijini kusikokua na TV....mama Kilango alikua mpambanaji lkn wa kwenye tv sio Same....nadhan Same walihitaji madaraja, maji, barabara, shule na mengineyo ikiwamo kutumika pamoja ktk shughuli za maendeleo ya wananchi. Ni kama ilivyokua kwa Kafulila nadhani
 
  • Thanks
Reactions: nao
Aibu sana hii...mtu wanayemchukia na kumbeza akiwa ccm sasa wamvhague mtu huyo huyo akiwa chadema?
Bonge la aibu.
Ndo hayo hayo yamekosesha watu urais na uspika.

Acha uongo hawamchukii Nape bali matendo yake ndy yanayo chukiwa akibadilika atapendwa kuliko unavyodhani
 
Nadhan tatizo bado lipo kwetu sisi wapiga kura hasa wa vijijini kusikokua na TV....mama Kilango alikua mpambanaji lkn wa kwenye tv sio Same....nadhan Same walihitaji madaraja, maji, barabara, shule na mengineyo ikiwamo kutumika pamoja ktk shughuli za maendeleo ya wananchi. Ni kama ilivyokua kwa Kafulila nadhani

Usipotoshe uma kazi ya mbunge si kujenga madaraja au kuwaletea maji hizo ni kazi za wakusanya kodi mimi nilimwona Kilango alikuwa mbunge wa kawaida huwezi kumlinganisha na Kafulila ambaye alikuwa anaibua uozo Kwa wewe unaye mtetea Kilango ebu niambie alichowahi kuibua alipokuwa bungeni kwa kipindi chake chote
 
Ukishangaa hilo shangaa kushindwa kwa kafulila na kushinda kwa tibaijuka
 
Aibu sana hii...mtu wanayemchukia na kumbeza akiwa ccm sasa wamvhague mtu huyo huyo akiwa chadema?
Bonge la aibu.
Ndo hayo hayo yamekosesha watu urais na uspika.

Mkuu unashangaa. Siasa za bongo Ukiwa point A hufai kabisa wewe ni mchafu najisi (unfit for human consumption) lakini ukihamia point B wewe uko msafi halali kabisa! Jamaa alisema hawa jamaa nawajua vizuri sana ni wezi wa kura lakini msihofu nyinyi lindeni kura za wabunge lakini zangu (urais) niachieni mimi mwenyewe. Lakini baada ya kura jamaa akawa wa kwanza kupiga kelele kwamba ameibiwa kura. Jamani si alituambia tulinde za ubunge za urais tumwachie mwenyewe?
 
Nani kakuambia yule ni mpinga ufisadi? Je ulimsikia mara baada ya kupewa wizara? Hovyo? Watu walikuwa wanatafuta kiki na wameshapata. NA mwenzake Ole sendeka na Mwakyembe.
 
Back
Top Bottom