Nini hatima ya Lipumba vs Maalim Seif

Nini hatima ya Lipumba vs Maalim Seif

Kinachowatoa mate hawa wengine pia ni pale anaposema yy anaitaka UKAWA ya katiba na si ya Ikulu
 
Pro pesa anajua kuingia kwa mh lowasa upinzani kumeleta uhai mkubwa sana,kwanini yeye lipumba kabla ya hapo alikuwa na madiwani ,wabunge wangapi bara?je?wamepungua au wameongezeka baada ya yeye kujiuzuru?siku zote yeye ndiye amekuwa kinara wa kuvunja makubaliano ya umoja wa upinzani ,dk za mwishomwisho kabla ya uchaguzi.je kwanini pro pesa alipotoka kufundisha aliliacha jina la LUGUYU LIPUMBA?
 
Sasa La Professa unataka umpokee mtu kwenye upinzani alafu utaki agombee..si wewe ulisema ufisadi ni mfumo wa ccm mana tangu lowassa atoke madarakani bdo ufisadi upo? ukiwa muongo ue na kumbukumbu
 
tatizo sio lowasa wala kashifa za lowasa tatizo lilikua wao(lipumba na slaa) kukubali kuachia nafasi ya kua wagombea urais. for the sake of ukawa wagomea ubunge wengi waliachia nafasi zao,wakiwaachia wenzao walioonekana kua na ushawishi na nguvu zaid. lkn halikuwezekana kwa baadhi ikiwa ni pamoja na waliojihakikishia kua wagombea urais ktk vyama vyao.

hata km angewekwa mtu mwingine kuchukua nafasi hio mbali na lowasa nina uhakika yangejitokeza km haya. na hata visingizio vingebadilika.
 
Aaah! Prof. Kumbe unaweza kumkaribisha shetani kanisani akusaidie kuhubiri, lakini kwa masharti kwamba asipewe upadri au uchungaji kwa sababu ni shetani....!! Kwa hiyo ndio maana ukakubali fisadi ajiunge upinzani awasaidie lakini uongozi asipewe maana hana maadili, ni fisadi. Na ulikuwa tayari kushirikiana na mtu unayesema hana maadili ili mradi tu asipewe nafasi ya kugombea urais? Kule Rwanda ulikokimbilia baada ya kujiuzulu kuna kitu walikufanyia huko kichwani mwako, sio kawaida atii!!
 
kwenye video hii ni maelezo ya seif ambaye ilifikia mpaka kuzomewa 21/8/2016 na wanachama wa CUF kwa usaliti alioufanya



Na hii hapa ni maelezo ya Prof. Lipumba akieleza jinsi seif alivyomsaliti kama alivyofanya kwa Marehemu Aboud Jumbe



Naamini wengi wenu mngefanya pengine hata zaidi ya kujiuzulu. Ila kama wewe ni mwanachadema ruhsa kuendelea kushambulia maana inafaida kwenu. hata kama ningekuwa mimi pia ningeendelea kushambulia maana ndo siasa yenyewe hiyo.
 
Lipumba hakutakiwa kujiuzulu bali kuondoa chama chake kutoka ukawa baada ya ujio wa Lowassa!!
 
Dah nimemuelewa sana Prof. hongera sana maelezo yamejitosheleza
 
Prof. Kaeleweka kwa Wenye kutumia kichwa kufikiri sio kunyolea Mapanki
 
Why amechukuwa miaka kumi 14 baada ya khutba hio ndio akajiuzulu hebu lete jengine
 
Mh Profesa nguli wa uchumi 98% ya maisha yake anafanya siasa sasa sijui alienda shule kufanyaje maana hana tofauti na akina tambwe hiza sasa..
 
Mh Profesa nguli wa uchumi 98% ya maisha yake anafanya siasa sasa sijui alienda shule kufanyaje maana hana tofauti na akina tambwe hiza sasa..

Aslimia 98% ya Maisha yake anafanya Siasa?

Kazaliwa 6th June 1952, kwa sasa Ana Miaka 64 na 98% ni Miaka 62 hivyo kaanza Siasa 1954!!
Najua Ulipigwa Penalt kwny hesabu kidato cha nne
 
Back
Top Bottom