Nini hasa kinachoikwamisha Africa kuendelea?

Its Pancho

JF-Expert Member
Sep 21, 2018
14,138
22,507
Muda mwingine unajiuliza waafrika tumemkosea nini Mungu.?
Lakini ukichimba unakuja kugundua adui yetu wa maendeleo yupo kati kati yetu. Hayuko mbali..!

Mwalimu aliwahi kusema maadui wakuu watatu hapa Tanzania ni.
Umaskini
Ujinga
Maradhi/magonjwa

Nafkiri mwalimu huenda aliangusha miwani yake kidogo wakati anaendelea kutafuta maadui hao watatu.
Alisahau adui mmoja mkubwa na ngumu kumtokomeza

UBINAFSI..
Ndio ni ubinafsi. Adui huyu alianza kuwepo toka enzi za utawala wa machifu.
Mkwawa kwenye historia ni shujaa.
Lakini aliuza wenzake..!
Ndio aliuza wenzake kwa wahindi ili tu apewe kioo,shanga,bunduki..!
Mpka kufikia kwa kina mobutu sese seko..
Namna alivyochukulia madaraka kama silaha kuu ya kulisha tumbo lake kuliko kipimo alichowekewa..!
Ubinafsi...!

Hapa afrika viongozi wanapoomba kura , watashinda na sisi hohe hahe mitaani, watakula na sisi,watalima na sisi..lakini baada ya matokeo na kupata ushindi wanaouita wa kishindo.

Utawaona tu kwenye V8 zao huku tukiamriwa kuwapisha njiani wakubwa wana haraka kuliko sisi kajamba nani..!
Tuna haraka kwani mambo yetu hayana umuhimu kuliko yao ya kuwahi viti virefu baada ya kutoka kula posho za siku kikaoni..!

Tusiwaseme vibosile hata wewe ukipata shavu hilo najua utawaza moyoni wanao wakasome ulaya.mkeo umfungulie biashara..ujenge hekalu kama la mfalme sulemani..!
Huku ukinadi Sera kuwa utawaletea watoto wetu hohehahe madawati na kuwatoa chini ya mwembe wakae darasani..!

Lakini ubinafsi huwa unakuja pale unapopata kitu.
Ukiwa huna unakuwa mmoja wetu. Ukipata sisi sio class yako..!

Dunia hii iko sawa ila watu ndo hatujawahi kuwa sawa.
Kuhubiri na kutenda ni vitu viwli tofauti..!

Tuwe na kiasi.

Pancho boy
 
Muda mwingine unajiuliza waafrika tumemkosea nini Mungu.?
Lakini ukichimba unakuja kugundua adui yetu wa maendeleo yupo kati kati yetu. Hayuko mbali..!

Mwalimu aliwahi kusema maadui wakuu watatu hapa Tanzania ni.
Umaskini
Ujinga
Maradhi/magonjwa

Nafkiri mwalimu huenda aliangusha miwani yake kidogo wakati anaendelea kutafuta maadui hao watatu.
Alisahau adui mmoja mkubwa na ngumu kumtokomeza

UBINAFSI..
Ndio ni ubinafsi. Adui huyu alianza kuwepo toka enzi za utawala wa machifu.
Mkwawa kwenye historia ni shujaa.
Lakini aliuza wenzake..!
Ndio aliuza wenzake kwa wahindi ili tu apewe kioo,shanga,bunduki..!
Mpka kufikia kwa kina mobutu sese seko..
Namna alivyochukulia madaraka kama silaha kuu ya kulisha tumbo lake kuliko kipimo alichowekewa..!
Ubinafsi...!

Hapa afrika viongozi wanapoomba kura , watashinda na sisi hohe hahe mitaani, watakula na sisi,watalima na sisi..lakini baada ya matokeo na kupata ushindi wanaouita wa kishindo.

Utawaona tu kwenye V8 zao huku tukiamriwa kuwapisha njiani wakubwa wana haraka kuliko sisi kajamba nani..!
Tuna haraka kwani mambo yetu hayana umuhimu kuliko yao ya kuwahi viti virefu baada ya kutoka kula posho za siku kikaoni..!

Tusiwaseme vibosile hata wewe ukipata shavu hilo najua utawaza moyoni wanao wakasome ulaya.mkeo umfungulie biashara..ujenge hekalu kama la mfalme sulemani..!
Huku ukinadi Sera kuwa utawaletea watoto wetu hohehahe madawati na kuwatoa chini ya mwembe wakae darasani..!

Lakini ubinafsi huwa unakuja pale unapopata kitu.
Ukiwa huna unakuwa mmoja wetu. Ukipata sisi sio class yako..!

Dunia hii iko sawa ila watu ndo hatujawahi kuwa sawa.
Kuhubiri na kutenda ni vitu viwli tofauti..!

Tuwe na kiasi.

Pancho boy
FOR GREAT THINKERS: Is Africa still a dark continent or a crucial partner in sustaining a better world?
 
Jibu la ukweli na jepesi ni kwamba njia zote za uchumi zina shikiliwa na nchi za magharibi kumbuka wao ndio pia wameshikilia pia siasa za Africa
Kweli lakini waliweza vipi kushika sehemu muhimu namna hiyo na nyeti
MTU hawezi ingia kwako bila kuwa na funguo ya mlangoni kaipataje.?
Kavunja mlango?
 
Ukoloni mambo leo ukighubikwa na fikra za kuwa omba omba
Kuna viongozi hawaamini kujiendeleza kwa rasiliamali zetu wenyewe .
Kinachohitajika ni mipango na isioindishwe pindishwe kama wanavyofanya

Ni sawa na kuchoma muhindi huku unakula kwanini usisubiri uive?
 
UKOLONI MAMBO LEO
magufuli anajitahid kuijenga tz
But kuna raia wanapnga juhud . Like kwa gadaf wa libya
Kwamba ni ukoloni mambo Leo pekee ni tatizo ?
Je nini kifanyike kuondoa ukoloni?
 
Africans cannot rule themselves because they don't have brain and mental capacity to govern a society..
Give them guns they would kill themselves,
Give them power they would use to steal all government money.
Give them independence and democracy
They would use it to promote tribalism,ethnicity,hatred killings and wars..
 
UKOLONI MAMBO LEO
magufuli anajitahid kuijenga tz
But kuna raia wanapnga juhud . Like kwa gadaf wa libya
Nadhani tatizo letu liko hapa. Kuhalalisha kushindwa kujiongoza kwa kutafuta wa kuwalaumu basi siku zinaenda na miaka inapita.
 
Umaskini wa kwtu Africa una changiwa na dini za kigeni' Tumemwacha Mungu wa mababu zetu tumegeukia miungu ya kigen ukristo na uislamu ,mtu akiweza kukuvuruga Iman yako Ni rahisi sana kutawala fikra zako.Fikiri kuwa dini zililetwa Kama kitangulizi Cha ukoloni kwa lengo la kutunyonya baada ya apo wakatuacha nazo akilin ,kwa hyo bdo tuna utumwa wa kifikra kila kitu tumeambiwa tumwachie Mungu .
 
Umaskini wa kwtu Africa una changiwa na dini za kigeni' Tumemwacha Mungu wa mababu zetu tumegeukia miungu ya kigen ukristo na uislamu ,mtu akiweza kukuvuruga Iman yako Ni rahisi sana kutawala fikra zako.Fikiri kuwa dini zililetwa Kama kitangulizi Cha ukoloni kwa lengo la kutunyonya baada ya apo wakatuacha nazo akilin ,kwa hyo bdo tuna utumwa wa kifikra kila kitu tumeambiwa tumwachie Mungu .
Hili nalo neno
 
Kweli lakini waliweza vipi kushika sehemu muhimu namna hiyo na nyeti
MTU hawezi ingia kwako bila kuwa na funguo ya mlangoni kaipataje.?
Kavunja mlango?
hakika ni ubinafsi tu na si sababu nyingine,viongoz wetu wengi wanapambania nafasi za kutuongoza ili tu wapate nafasi ya kujibinafsisha.na hii nafkili ni kasumba yetu sisi waafrika hatakama ningekuwa mimi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom