Nini haki ya jirani juu ya Common Wall?

ZINDAGI

JF-Expert Member
Dec 5, 2015
1,116
1,422
Nipo na jirani yangu ambaye ndio kajenga ukuta unaotenganisha nyumba zetu, napenda kujua je nina haki yoyote juu ya ukuta huu kwa upande wa nyumba yangu?

Jirani yangu ananitishia kunishitaki iwapo nitaufanya jambo lolote upande wangu.

Naomba msaada wenu.
 
Kama kajenga mpakani basi upande ulio kwako unaweza kufanya chochote alimradi isihusishe kuubomoa....ingawa hiyo yote ni matokeo ya kuwa na jirani mbinafsi.

Nijuavyo mimi huo mpaka mnamiliki nyie wote, hivyo mmoja wenu akitaka kujenga ukuta basi ni vizuri mkakaa chini na kujadiliana...na kama itawezekana basi hata kuchangia gharama nusu kwa nusu.
 
Mlitakiwa muache nafasi kati yenu wawili.

Yani kila mtu aache may be mita moja kisha ajenge ukuta wake au aweke uzio au vyovyote vile aonavyo.

Kama hakuacha nafasi dawa hapo na ww simamisha ukuta wako karibu kabisa na alipojenga wa kwake.

Kama hivi yani

IMG-20200720-WA0076.jpg
 
Mlitakiwa muache nafasi kati yenu wawili.

Yani kila mtu aache may be mita moja kisha ajenge ukuta wake au aweke uzio au vyovyote vile aonavyo.

Kama hakuacha nafasi dawa hapo na ww simamisha ukuta wako karibu kabisa na alipojenga wa kwake.

Kama hivi yani

View attachment 1516250
Hivi viwanja ni vidogo na upana wake huwezi kuacha mita moja kila upande.
Site plan inaonyesha viwanja vyote vimetenganishwa na mstari mmoja ikiimanisha ni common wall na sio ukuta mbili.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom