No stress ya dhambi! Labda sheria za nchi.. pili huna hofu juu ya uchawi au nguvu zozote za kiroho! Kuna baadhi ya watu hujitesa kwa kuamini tu hizo nguvu za kiroho ama ktk negative au positive!.
Kila chakula kwako ni halali hakuna hofu ya kufuru au kujichafua kiroho!
Kila fikra unaweza kufikiri bila ya Kuwa na limitation ya kumkufuru kiumbe fulani!.
Hakuna sheria ya dini inakukaba kuhusu maisha yako ya ndoa,wewe au nyinyi ndo waamuzi wakuu ya nini muamue bila ya hofu za kiimani!.. Kuna watu wanaishi ndoa zao kwa mateso na wanashindwa kuachana kisa sheria za dini!
Unaimarika kiakili vizuri ktk kutatua matatizo yako kwani hakuna wa kumtegemea pale unaposhindwa kila kitu I mean huna kauli za kusema "Namuachia Mungu" kila tatizo lako utakomaa nalo..
Angalizo Kama mtu anataka Kuwa mpagani basi yafaa awe na akili imara na timamu sana Tena sana kwa maana Kuwa mpagani hakukupi ruhusa ya moja kwa moja Kuwa huru ktk kila kitu so ni muhimu mtu kuzingatia sheria za kimazingira(fikiri zaidi hapo) ili Kuwa salama na kuwa ktk ubora wako wewe Kama kiumbe hai kinachoweza kufuata sheria mama za dunia pasipo msukumo ama kutishwa au kushurutishwa na kiumbe mwengine.