geranteeh
JF-Expert Member
- May 21, 2015
- 266
- 618
Habari za weekend Wakuu, Madere na Wapenzi wa magari. Bila shaka leo ni siku nyingine ya kujifunza kitu ambacho pengine tumekutana nacho sana hasa sisi washinda barabarani. Kwa kawaida mfumo wa gari lako pale mbele kwenye engine ni moto tupu ndo maana utasikia hiki kimechoma hiki au kile kikichomwa kinasababisha hivi lakini hayo yote ntawaachia mechanics wenye elimu zao.
Mimi leo kama kawaida ntakupa elimu ya kukufanya uelewe kama mtumiaji wa gari na si kama fundi ndiyo maana tunashauri tatizo ukiona ni kubwa wasiliana na fundi wako kwa utaalamu na marekebisho zaidi. Turudi kwenye mada kabla sijaanza kukutoa ulimi ndugu yangu. Ni muhimu kuelewa hili somo kwani joto la engine yako ndilo linalokadiria maisha yake kwani endapo hutokuwa makini na joto la mashine itasababisha kuua engine yako ukaingia gharama ya kununua engine mpya. Kuna kanuni ya udereva ambayo watu wengi huwa hawaizingatii ambayo unatakiwa wakati unaendesha kila baada ya sekunde kadhaa uangalie dashboard yako kwani itakupa taarifa kama vile joto litapanda basi utaona kwenye mshale wa jotoridi au kwa gari za kisasa kuna taa ya joto huwaka sasa endapo utakua ni mtazama mbele basi hizi taarifa hutozipata na kupelekea gari yako kupata hitilafu zaidi au hata engine kufa kwani nina watu ninaowafaham zaid ya watano washawahi kuua engine zao kwa kuendesha gari huku joto likiwa juu. Trust me walinunua engine mpya na wengine miswaki.
NINI SABABU YA TAA YA TEMPERATURE KUWAKA AU MSHALE WA JOTO KUPANDA?
Kuna sababu nyingi sana ambazo zinaweza sababisha gari yako kupanda joto ila sababu kubwa ni kiwango cha maji kwenye rejeta yako kupungua au kuisha kabisa. Kazi kubwa ya rejeta yako ni kupoza engine ambapo maji hupelekwa kwenye engine kwa upozaji kisha kurudi kwenye rejeta yanapozwa then yanarudi kwenye engine na huu mzunguko huenda na kuenda mpaka utakapozima gari lako hivo basi pindi maji yanapokosekana kwenye rejeta automatically engine inakosa kitu cha kupozwa hivo joto hupanda na kusababisha matatizo zaidi.
Kuna mtu anaweza uliza kwanini maji ya kwenye rejeta inatokea yanaisha? Kuna sababu nyingi lakini kubwa ambayo hata namm nimei experience ni kupasuka kwa rejeta kiasi kupelekea kuvuja kwa maji na unapowasha gari ile pressure inakua kubwa hata mpasuko ukiwa mdogo tu basi maji yatatoka kwa wingi na solution yake ni kwenda kuziba kwa fundi rejeta.
Sababu ya pili inayopelekea maji kupotea ni kuziba kwa vinjia vya rejeta ambapo kumbuka niliandika kuhusu mzunguko wa kutoka kwenye engine kwenda kwenye rejeta na kurudi so huo mzunguko hufanyika kwenye vinjia vya rejeta hivo inapotokea vimeziba itapelekea maji kutozunguka na kutafuta pa kutokea mfano kwenye weak pipe, kimtungi cha reserve au kwenye kifuniko cha rejeta.
Sababu ya pili inayopelekea temperature kupanda ni kutofanya kazi kwa feni ya rejeta. Utajiuliza femi ya rejeta ndo nini? Kama ulikua makini kwa nliyoyaongea hapo juu utapata picha ya kuhusu ule mzunguko wa maji kutoka kwenye rejeta kwenda kwenye engine na kurudi je ulijiuliza kwenye rejeta hayo maji yanapozwa na nini kabla ya kurudi kwenye engine?
Kuna vitu viwili ambavyo vinapoza maji ya kwenye rejeta cha kwanza kabisa ni feni ambayo ipo mbele ya rejeta na cha pili ni upepo kutoka nje ya gari unaopitia kwenye show ya gari pale mbele. Ushawahi jiuliza kwanini gari pale mbele haizibwi lazima kila gari inakuwa na matundu matundu? Atleast leo ushapata jibu ndugu yangu. Sasa tukirudi kwenye mada endapo hii feni ikiwa haifanyi kazi inamaana maji ya kwenye rejeta hayatapozwa kumaanisha rejeta itarudisha maji yakiwa yamoto so engine haitapozwa na temperature itapanda.
Sababu nyingine ya temperature kupanda ntazitaja kwa ufupi na kwa umoja ambazo ni kama vile kifuniko kuharibika cha rejeta hivo kupitisha maji na mvuke kwa juu hivo kupelekea maji kupungua, pipe zinazopeleka maji kwenye engine kulegea ama kutoboka hivo kupelekea maji kupungua.
NINI CHA KUFANYA ENDAPO JOTO LA GARI LIMEPANDA?
A.. Kwanza unatakiwa kujua kwamba hutakiwi kuendesha gari yako endapo joto limepanda either kwa alama ya taa ya temperature au ule mshale kupanda hakikisha unatafta sehem unaegesha gari haraka sana. Baada ya kuegesha gari izime au kama hali ni mbaya sana gari za kisasa hujizima zenyewe.
Baada ya hapo shuka na ufungue bonet ya gari yako kwanza ili hewa iingie na gari ipate kupoa zaidi na usifungue au kugusa chochote. Acha gari yako kwa muda mpaka utakapojiridhisha imepoa estimation huwa ni nusu saa inatosha sana na kwa gari zakisasa hata uwashe vipi gari haitawaka endapo utajaribu kuwasha trust me so usijisumbue (hii ni ikiwa joto limepanda sana).
Baada ya hapo tafuta kitambaa au taulo na ukikosa hata nguo yako uitumie kufungulia mfuniko wa rejeta taratibu then angalia kiwango cha maji au coolant kilichopo endapo kimepungua kama kimepungua ongeza then washa gari ikiwezekana nenda garage ikaangaliwe.
B. Endapo utawasha gari yako na kukuta taa bado inawaka au ukaendesha kwa muda mshale ukapanda basi angalia feni ya rejeta kama inafanya kazi kama haifanyi kazi ni vema ukawasiliana na fundi wako aje kuirekebisha akiweza kuirekebisha ni jambo la kheri kwani kuna wakati inakua nia matatizo ya umeme waya haupeleki moto au fuse inakua na shida au kama itahitajika mpya unaweza ukatupatia rizqi nasi tukakuuzia kitu mang'anyu ila kumbuka haishauriwi kuendesha gari yako ikiwa joto liko juu hata mara moja kwani madhara yake madogo ni kuharibu silinda head gasket na makubwa ni kuua engine.....
Makala hii imeandikwa na Hamis Mgaya
Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi leo kama kawaida ntakupa elimu ya kukufanya uelewe kama mtumiaji wa gari na si kama fundi ndiyo maana tunashauri tatizo ukiona ni kubwa wasiliana na fundi wako kwa utaalamu na marekebisho zaidi. Turudi kwenye mada kabla sijaanza kukutoa ulimi ndugu yangu. Ni muhimu kuelewa hili somo kwani joto la engine yako ndilo linalokadiria maisha yake kwani endapo hutokuwa makini na joto la mashine itasababisha kuua engine yako ukaingia gharama ya kununua engine mpya. Kuna kanuni ya udereva ambayo watu wengi huwa hawaizingatii ambayo unatakiwa wakati unaendesha kila baada ya sekunde kadhaa uangalie dashboard yako kwani itakupa taarifa kama vile joto litapanda basi utaona kwenye mshale wa jotoridi au kwa gari za kisasa kuna taa ya joto huwaka sasa endapo utakua ni mtazama mbele basi hizi taarifa hutozipata na kupelekea gari yako kupata hitilafu zaidi au hata engine kufa kwani nina watu ninaowafaham zaid ya watano washawahi kuua engine zao kwa kuendesha gari huku joto likiwa juu. Trust me walinunua engine mpya na wengine miswaki.
NINI SABABU YA TAA YA TEMPERATURE KUWAKA AU MSHALE WA JOTO KUPANDA?
Kuna sababu nyingi sana ambazo zinaweza sababisha gari yako kupanda joto ila sababu kubwa ni kiwango cha maji kwenye rejeta yako kupungua au kuisha kabisa. Kazi kubwa ya rejeta yako ni kupoza engine ambapo maji hupelekwa kwenye engine kwa upozaji kisha kurudi kwenye rejeta yanapozwa then yanarudi kwenye engine na huu mzunguko huenda na kuenda mpaka utakapozima gari lako hivo basi pindi maji yanapokosekana kwenye rejeta automatically engine inakosa kitu cha kupozwa hivo joto hupanda na kusababisha matatizo zaidi.
Kuna mtu anaweza uliza kwanini maji ya kwenye rejeta inatokea yanaisha? Kuna sababu nyingi lakini kubwa ambayo hata namm nimei experience ni kupasuka kwa rejeta kiasi kupelekea kuvuja kwa maji na unapowasha gari ile pressure inakua kubwa hata mpasuko ukiwa mdogo tu basi maji yatatoka kwa wingi na solution yake ni kwenda kuziba kwa fundi rejeta.
Sababu ya pili inayopelekea maji kupotea ni kuziba kwa vinjia vya rejeta ambapo kumbuka niliandika kuhusu mzunguko wa kutoka kwenye engine kwenda kwenye rejeta na kurudi so huo mzunguko hufanyika kwenye vinjia vya rejeta hivo inapotokea vimeziba itapelekea maji kutozunguka na kutafuta pa kutokea mfano kwenye weak pipe, kimtungi cha reserve au kwenye kifuniko cha rejeta.
Sababu ya pili inayopelekea temperature kupanda ni kutofanya kazi kwa feni ya rejeta. Utajiuliza femi ya rejeta ndo nini? Kama ulikua makini kwa nliyoyaongea hapo juu utapata picha ya kuhusu ule mzunguko wa maji kutoka kwenye rejeta kwenda kwenye engine na kurudi je ulijiuliza kwenye rejeta hayo maji yanapozwa na nini kabla ya kurudi kwenye engine?
Kuna vitu viwili ambavyo vinapoza maji ya kwenye rejeta cha kwanza kabisa ni feni ambayo ipo mbele ya rejeta na cha pili ni upepo kutoka nje ya gari unaopitia kwenye show ya gari pale mbele. Ushawahi jiuliza kwanini gari pale mbele haizibwi lazima kila gari inakuwa na matundu matundu? Atleast leo ushapata jibu ndugu yangu. Sasa tukirudi kwenye mada endapo hii feni ikiwa haifanyi kazi inamaana maji ya kwenye rejeta hayatapozwa kumaanisha rejeta itarudisha maji yakiwa yamoto so engine haitapozwa na temperature itapanda.
Sababu nyingine ya temperature kupanda ntazitaja kwa ufupi na kwa umoja ambazo ni kama vile kifuniko kuharibika cha rejeta hivo kupitisha maji na mvuke kwa juu hivo kupelekea maji kupungua, pipe zinazopeleka maji kwenye engine kulegea ama kutoboka hivo kupelekea maji kupungua.
NINI CHA KUFANYA ENDAPO JOTO LA GARI LIMEPANDA?
A.. Kwanza unatakiwa kujua kwamba hutakiwi kuendesha gari yako endapo joto limepanda either kwa alama ya taa ya temperature au ule mshale kupanda hakikisha unatafta sehem unaegesha gari haraka sana. Baada ya kuegesha gari izime au kama hali ni mbaya sana gari za kisasa hujizima zenyewe.
Baada ya hapo shuka na ufungue bonet ya gari yako kwanza ili hewa iingie na gari ipate kupoa zaidi na usifungue au kugusa chochote. Acha gari yako kwa muda mpaka utakapojiridhisha imepoa estimation huwa ni nusu saa inatosha sana na kwa gari zakisasa hata uwashe vipi gari haitawaka endapo utajaribu kuwasha trust me so usijisumbue (hii ni ikiwa joto limepanda sana).
Baada ya hapo tafuta kitambaa au taulo na ukikosa hata nguo yako uitumie kufungulia mfuniko wa rejeta taratibu then angalia kiwango cha maji au coolant kilichopo endapo kimepungua kama kimepungua ongeza then washa gari ikiwezekana nenda garage ikaangaliwe.
B. Endapo utawasha gari yako na kukuta taa bado inawaka au ukaendesha kwa muda mshale ukapanda basi angalia feni ya rejeta kama inafanya kazi kama haifanyi kazi ni vema ukawasiliana na fundi wako aje kuirekebisha akiweza kuirekebisha ni jambo la kheri kwani kuna wakati inakua nia matatizo ya umeme waya haupeleki moto au fuse inakua na shida au kama itahitajika mpya unaweza ukatupatia rizqi nasi tukakuuzia kitu mang'anyu ila kumbuka haishauriwi kuendesha gari yako ikiwa joto liko juu hata mara moja kwani madhara yake madogo ni kuharibu silinda head gasket na makubwa ni kuua engine.....
Makala hii imeandikwa na Hamis Mgaya
Sent using Jamii Forums mobile app