Linguistic
JF-Expert Member
- Mar 16, 2021
- 3,671
- 8,237
Wakuu Nimefanya utafiti sana wa jambo hili ningependa kuweka kwa ufupi tu historia ya Disco Tanzania.
Wakuu Richie Dillon alianza u’DJ 1984 Mwanza Alshars Tikkha Disco ndiyo DJ wa kwanza bongo kufanya mixing ya beat to beat miaka ya 1990 akiwa huko Mwanza na kuwapiga bao ma’DJ wa Dar.
Muziki wa Disco ulianza US katikati ya miaka 60 wakati huo ukijumuisha funk,soul,pop na salsa,mashabiki makubwa walikuwa jumuiya ya wanyamwezi (black Americans) walatino na Psychedelic (Mateja) na walikuwa wanajumuisha pia na live performance mfano wa disco ni Soul Train.
Mwanzo wa Disco ni New York chini ya DJ David Manuso ambapo alianzisha klabu ya wanachama tu nyumbani kwake na baadhi ya wanamuziki walipata umaarufu wa kuburudisha diskoni kwanza kama LaDonna Adrian Gaines maarufu kama Donna Summer ambaye alijulikana pia kama Queen of Disco na First Lady of Love.
Disco lilienea duniani na Tanzania hatukubaki nyuma kama Disco lilianza rasmi miaka ya 70 hususan mwaka 1971 ambapo maDj wa mwanzo wengi walikuwa wanamuziki kama Francis Bundala aka Dj Sweet Francis alikuwa muimbaji katika bendi aliyoianzisha mwaka 1964 ya The Screemers na Adam Salehe Mwambile aka Addy Sally(RIP)
Disco Tanzania lilianza katika hoteli ya Africana likijulikana kama GoGo Disco na DJ wa kwanza alikuwa Bhoka Wilson toka Southern Rhodesia wakati huo sasa ni Zimbabwe alikuwa pia muimbaji wa Cabbaret pale Simba Grill hoteli ya Kilimanjaro.
Mwaka 1972 Dj Sweet Francis naye akawa DJ hapo mpk mwaka 1973 ampako akaja DJ mwanamama toka South Afrika Dj Judy Kingui ambaye alikuwa mke wa mwanamuziki Kingui wa bendi ya The Rifters ambapo alihudumu mpaka mwaka 1975.
Mwaka 1972 likaanzishwa Disco la Sansui pale SeaView hotel chini ya Dj McTwist hakudumu sana na Addy Sally akawa Dj hapo.
Na mwaka huo 1975 Addy Sally alikuwa DJ Mlimani Park enzi za bumping.
Mwaka 1976 Addy Sally akaenda Arusha kuanzisha disco Arusha by Night na wakapata Cave Disco chini ya Dj Sweet Francis.
Kukawa kuna kushindana fulani kati ya hawa madj wawili kiasi cha kuweka wacheza show na mmoja wa wacheza show alikuwa Choggy Sly ambaye alikuja kuwa Dj maarufu pia.
Mwaka 1977 kukawa na mfumuko wa madisco kama Keys hotel Mbowe ambapo Dj Sweet Francis alikuwa hapo na kumfundisha kazi Dj Jerry Kotto.
Mwaka 1978 akaibuka Dj Luke Joe wakati huo akiwa sekondari na golikipa mzuri sana wa soka kwenye disco la Stereo ambapo lilipata umaarufu baada ya kuhamia hoteli ya Kunduchi
Miaka ya 80 ndiyo utitiri wa madisco uiibuka na madj wakali kama Niga Jay Saydou na Kalikali, Richie Dillon ambaye alianzia KUfanya Udj.wake Mwanza akaenda Nairobi Boomerang na kuja Dar Valentino Continental 7th Floor Bilicanas.
Wakuu Niishie hapa kwa leo nikija tena tutaanzia miaka ya 80.
Karibuni Kwa Mjadala
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Wakuu Richie Dillon alianza u’DJ 1984 Mwanza Alshars Tikkha Disco ndiyo DJ wa kwanza bongo kufanya mixing ya beat to beat miaka ya 1990 akiwa huko Mwanza na kuwapiga bao ma’DJ wa Dar.
Muziki wa Disco ulianza US katikati ya miaka 60 wakati huo ukijumuisha funk,soul,pop na salsa,mashabiki makubwa walikuwa jumuiya ya wanyamwezi (black Americans) walatino na Psychedelic (Mateja) na walikuwa wanajumuisha pia na live performance mfano wa disco ni Soul Train.
Mwanzo wa Disco ni New York chini ya DJ David Manuso ambapo alianzisha klabu ya wanachama tu nyumbani kwake na baadhi ya wanamuziki walipata umaarufu wa kuburudisha diskoni kwanza kama LaDonna Adrian Gaines maarufu kama Donna Summer ambaye alijulikana pia kama Queen of Disco na First Lady of Love.
Disco lilienea duniani na Tanzania hatukubaki nyuma kama Disco lilianza rasmi miaka ya 70 hususan mwaka 1971 ambapo maDj wa mwanzo wengi walikuwa wanamuziki kama Francis Bundala aka Dj Sweet Francis alikuwa muimbaji katika bendi aliyoianzisha mwaka 1964 ya The Screemers na Adam Salehe Mwambile aka Addy Sally(RIP)
Disco Tanzania lilianza katika hoteli ya Africana likijulikana kama GoGo Disco na DJ wa kwanza alikuwa Bhoka Wilson toka Southern Rhodesia wakati huo sasa ni Zimbabwe alikuwa pia muimbaji wa Cabbaret pale Simba Grill hoteli ya Kilimanjaro.
Mwaka 1972 Dj Sweet Francis naye akawa DJ hapo mpk mwaka 1973 ampako akaja DJ mwanamama toka South Afrika Dj Judy Kingui ambaye alikuwa mke wa mwanamuziki Kingui wa bendi ya The Rifters ambapo alihudumu mpaka mwaka 1975.
Mwaka 1972 likaanzishwa Disco la Sansui pale SeaView hotel chini ya Dj McTwist hakudumu sana na Addy Sally akawa Dj hapo.
Na mwaka huo 1975 Addy Sally alikuwa DJ Mlimani Park enzi za bumping.
Mwaka 1976 Addy Sally akaenda Arusha kuanzisha disco Arusha by Night na wakapata Cave Disco chini ya Dj Sweet Francis.
Kukawa kuna kushindana fulani kati ya hawa madj wawili kiasi cha kuweka wacheza show na mmoja wa wacheza show alikuwa Choggy Sly ambaye alikuja kuwa Dj maarufu pia.
Mwaka 1977 kukawa na mfumuko wa madisco kama Keys hotel Mbowe ambapo Dj Sweet Francis alikuwa hapo na kumfundisha kazi Dj Jerry Kotto.
Mwaka 1978 akaibuka Dj Luke Joe wakati huo akiwa sekondari na golikipa mzuri sana wa soka kwenye disco la Stereo ambapo lilipata umaarufu baada ya kuhamia hoteli ya Kunduchi
Miaka ya 80 ndiyo utitiri wa madisco uiibuka na madj wakali kama Niga Jay Saydou na Kalikali, Richie Dillon ambaye alianzia KUfanya Udj.wake Mwanza akaenda Nairobi Boomerang na kuja Dar Valentino Continental 7th Floor Bilicanas.
Wakuu Niishie hapa kwa leo nikija tena tutaanzia miaka ya 80.
Karibuni Kwa Mjadala
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app