Ningekuwa CC ya CHADEMA ningemsamehe Kitila Mkumbo

Ningekuwa CC ya CHADEMA ningemsamehe Kitila Mkumbo

Asamehewe Dr kitila kwakweli..ana nia njema kabisa si mropokaji kama zito..chondechonde tumurudishe kundini
 
Kaka, Pasco, kwanza nimefarijika kusoma story yako ambayo imechimbua hadi ndani kabisa na kueleza hisia zako zote kuhusu sekeseke linaloendelea. Ninaomba nijibu kama ifuatavyo:

Nataka tu kukuuliza Pasco, na kwa kutumia busara ya kawaida tu, CCM inachukiwa na wananchi kwa kuwa ina sera mbaya au kwa kuwa ina viongozi wabaya? Nataka niseme, hakuna namna yoyote unayoweza kuwachafua viongozi wakuu wa chama pasipo kukichafua chama? Kwa kuwachafua viongozi wa juu wa chama ni kukimaliza chama na si kukijenga. Katika hilo hawa ndugu zetu wakubali kuwa walifanya kosa.
Mkuu Kyafulilo, hapa naungana na wewe, huwezi kuwachafua viongozi wa chama na chama kikabaki salama!, ila viongozi wanaochafuliwa ni wale viongozi wasafi wanapakwa matope ili waonekane wachafu!, lakini waraka haukumchafua mtu, umeonyesha uchafu wa viongozi ambao umefunikwa, huu mtindo wa kunyamazia uchafu wa viongozi kwa uoga wa kukichafua chama, ni kudharau mwiba, mwisho wa siku mguu huota tende na chama chote kuoza!. Katika huo uchafuaji wa viongozi, jee kuna kitu ambacho sicho, wamesingiziwa au kuzushiwa?!. Waraka ule umeeleza wazi udhaifu wa uongozi uliopo katika kuikabili CCM, huu ni ufa kwa Chadema, kuna aina mbalimbali za kuziba ufa, moja ya aina hizo ni kujaza tuu sementi kwenye ufa, kupiga lipu na kupaka rangi, ufa unakuwa umekwisha. Lakini kama ni ufa mkubwa na uko kwenye msingi, huwezi kuuziba kwa kuuziba tuu, utaendelea, ili kuuziba huu ufa mkubwa, ni lazima kwanza ubomoe kidoge ndipo uzibe. Waraka umeyatamka machafu ya viongozi wenu, ilibidi pia kuibomoa kidogo Chadema ndipo huo ufa uzibwe!. Baadhi ya mabadiliko ni kama mbegu wakati wa germination, mbegu mama hufa, ili ichipue!. Ili kupata faida ya mabadiliko, wanaChadema lazima mkubali "no sweet without sweat", Viongozi wenu waliopo ni keki, mnawapenda sana, ingepoenda wawepo hivyo hivyo na kuendelea kuwepo, huku wanachama man njaa ya mabadiliko, uchaguzi ni wenu, whether you have to eat your cake and its gone, or you leave it as it is na kuendelea kuangaliana!. "You can't eat you cake and have it!".

Pasco umeongea kuhusu suala la nani aombe msamaha, na umekosoa wazo langu la kwamba Kitila Mkumbo aombe msamaha, lakini mimi napenda niwe mkweli katika hili. Hakuna namna yoyote ambayo CHADEMA watafikiria kumtafuta Kitila na kuomba msamaha. Hivyo ndivyo wakubwa walivyo, hata siku moja hawapendi kuonekana kwamba wamewapigia magoti walio wadogo kwao.
Hili nimelisema linawezekana kupitia Baraza Kuu. Prof. Beregu ameisha liona, naamini pia Prof. Safari pia ameliona, naamini Mzee Victor Kimesera hili ameliona, na labda hata Mzee Edwin Mtei pia ameliona, tatizo kubwa la maamuzi ya CC ya Chadema ni ukosefu tuu wa busara ndogo!, mule ndani kuna mijitu ina kelele sasa!, CC yote imetishwa na kelele, busara ikawekwa kando!. Baraza Kuu bado linaweza kurudisha sense ya busara ndani ya Chama, kama hilo Baraza Kuu ni Baraza Kuu kweli na sio Baraza Kuu "ruber stamp" kama mkutano mkuu wa CCM!.

Bado naona Kitila ana msaada mkubwa kwa taifa letu kupitia chadema. Tukishika madaraka ya nchi hii kitila ni potential Minister of Education. Kuna ubaya gani akipiga magoti na akalifaa taifa letu katika nafasi ya waziri wa elimu huko mbeleni? Watu wanadhani akitubu atakuwa amedhalilika, lakini wanasahau impact yake kwa taifa baada ya kukubali hicho tunachodhani ni kujidhalilisha. Bado naona kuna haja ya kitila kukubali kupiga magoti ili yaishe. Yamewezekana kwa Kafulila why not Mkumbo. CHADEMA kinaongozwa na binadamu ambao pia wana mapungufu yao mengi tu, tunaamini hawataliangalia sana hili kosa moja la Kitila na kusahau mambo makubwa mengi aliyokifanyia chama na nchi. Na ni imani yangu kwamba hawa watu wanaoongoza CHADEMA, wanayatazama pia mapungufu yao na kutambua kwamba Kitila kateleza kama ambavyo hata wao waliwahi kuteleza hapo awali au wanavyoteleza kila siku. Tusameheane tusonge mbele.
Mkuu Kyafulilo, jee uliweza kujua "the motive behind waraka ule", Kitila ni political scientist, ameangalia mambo yalivyo ndani ya Chadema, akajiridhisha as it is now, Chadema haiwezi kuiondoa CCM madarakani bila radical changes from within!, waraka uliainisha initiations za radical changes. Kama Chadema ni kweli imedhamniria kwa dhati kuondoa CCM na kwenda ikulu, haiwezi kuzipuuza hoja za ule waraka!, na hapo ilipo its left with only two options, either ikubali kufanya mabadiko makubwa ya uongozi, radical changes za uongozi wa juu, au ijikubalie tuu kuendelea kuwa chama cha kudumu cha upinzani, huku ikiendelea kusinyaa!.

Kwa maoni yangu to be honest, labda kwa vile sio mwana Chadema, naiona Chadema kama haina watu wa kuipeleka ikulu!. I don't see watu wenye potentials katika hao waliopo, inawezekana kabisa wakawepo, ila kwa vile bado hawajajionyesha as serious able people with abilities na capabilities, lets me give you the benefits of doubts kuwa wataibuka na kuipeleka Chadema ikulu come 2015!, kikwazo pekee kwa Chadema, ambacho kita i cost sana Chadema, ni payment of karma price ya kuwasingizia watu usaliti na hivyo kuwachafua. Kama ni wasaliti kweli, karma itawashughulikia, lakini kama Chadema imewasingizia, they will shine huko waendako and Chadema will pay the price!.
All the best.
Pasco.
 
mimi siwaungi mkono kabisa chadema na najiandaa kurudisha kadi ni kweli kabisa mabadiliko yanahitajika ndani ya cdm hatuwataki wakina mbowe watu wa kuhamasisha vurugu tu tunatakaupizani wa hoja tena za msingi mimi binafsi nawaunga mkono wakina zitto na kudhibitisha hili cdm 2000-2005 kilikua chama cha hoja za msingi cheki leo ni watu wa umbea tu hawana jipya tena na hawajui chama kuwepo hapo kulipo ni kwa jitihada za watu watatu tu zitto, slaa na kidogoo mbowe ila kiukweli mbowe hana maadili ya uwongozi anakurupuka tu na wasahau kuongoza nnchi hii
 
Mkuu Ndikwe, unakumbuka jinsi alivyowafurusha City Water?!, amini nakuambia, alitaka kuwatimua Richmond siku nyingi ila ...(naamini unaijua sababu!).
Hizo pesa anatumia sio kuhonga bali kusaidia, its only for support!. Akifanikiwa kufika kule juu, ataigeuza Tanzania kuwa ni nchi ya hahadi, itakuwa nchi ya maziwa na asali!. Yaani ataigeuza pepo!.
Pasco

Haya mkuu Pasco, Unajua Lowassa kiukweli huwa natambua kwa kuwa mtu wa maamzi ila Mh.anatumia nguvu nyingi sana kutafuta urais ndilo jambo linalonipa shaka kidogo. Kingine unadhani kwanini Nyerere alimkana kipindi kile? Unajua tunajifunza kuwa kumbe kulikuwa na siri nzito ya kukataliwa hawa jamaa (Kikwete & Lowasa) maana jakaya tayari kaharibu nchi kupindukia karibia kila kona. Maisha magumu kwa wananchi, pesa haina thamani,Uchumi umedorora, kubwa zaidi vijana tumemeliza vyuo vikuu mpaka sasa mwaka wa 3 tupo uraiani tunasota tu na ndicho kinatufanya kuwa na hasira na ccm maana wenye kunufaika ni watoto wa makada wa CCM au undugu. Mifumo yote hii imeletwa na CCM hususa chini ya huyu Jakaya ambaye ni miongoni mwa waliyo katalia na J.K.Nyerere na Ndugu yake Lowassa.
Swali langu, je unataka tuamini vipi kuwa Lowassa hatakuwa Kirusi kama Kikwete maana Mtoto wa masikini yoyote hapa tanzania hususani msomi analia na mifumo ya kujuana iliyoundwa na ccm hiii?
 
Back
Top Bottom