Ningekuwa CC ya CHADEMA ningemsamehe Kitila Mkumbo

Ningekuwa CC ya CHADEMA ningemsamehe Kitila Mkumbo

Ulipomsema Saanane, nakulinganisha na Kitila aliyemwita MIDAEIGHT wakati wakiandaa waraka wa uasi ambao wewe umeupenda!
Hakuna popote nilipoonyesha kwa namna yoyote ile kwamba naukubali waraka wao wa siri. Nihukumu kwa lingine lakini si hilo.
 
Hivi unawezaje kumsamehe mtu ambaye hajaomba msamaha na anasisitiza hawezi omba kwa sababu hajafanya Kosa. Ni kweli issue ya Ben Saanane na Kitila Mkumbo zinafanana. Lakini Ben alisamehewa na kuwekwa chini ya uangalizi baada ya yeye mew yews kukiri Kosa na kuomba asemehewe. Kitila Mkumbo yeye amekiri kushiriki Kaunda waraka lakini aligoma kuomba msamaha licha ya kusisitizwa na wajumbe wa Kamati Kuu kwa kigezo kwamba yeye haoni Kama kafanya Kosa na hivyo hana sababu ya kuomba msamaha.
 
hakuna kumsamehe..aende zake akaunde chama chake na rais wake wa mwandiga
 
Hivi unawezaje kumsamehe mtu ambaye hajaomba msamaha na anasisitiza hawezi omba kwa sababu hajafanya Kosa. Ni kweli issue ya Ben Saanane na Kitila Mkumbo zinafanana. Lakini Ben alisamehewa na kuwekwa chini ya uangalizi baada ya yeye mew yews kukiri Kosa na kuomba asemehewe. Kitila Mkumbo yeye amekiri kushiriki Kaunda waraka lakini aligoma kuomba msamaha licha ya kusisitizwa na wajumbe wa Kamati Kuu kwa kigezo kwamba yeye haoni Kama kafanya Kosa na hivyo hana sababu ya kuomba msamaha.
Nakubaliana na wewe kwamba asamehewe iwapo atakubali kuomba msamaha. Ni wakati mzuri kwa wale tulio karibu na Mkumbo kumshawishi afanye hivyo kwa faida yake na ya chama.
 
Mkuu Mujuni, kwanza mimi sio CCM, bali namkubali sana Lowassa!. CCM kilikuwa chama cha kijamaa enzi za Nyerere, azimio la Zanzibar liliuzika ujamaa ila ukabaki kwenye maandishi!. Tena maandishi hayo yako hadi kwenye katiba ya nchi!.
Pasco

Mbona Lowassa hajawahi kuponda ufisadi,hajawahi kukubali ama kukanusha ile kashfa ya RICHMOND pia kwanini anatumia pesa nyingi kuhonga makanisani na misikitini pamoja na boda boda anachokitaka kwa watanzania hawa haswa ni nini maana huu mchakato umeanza pindi alipojiuzuru tu uwaziri mkuu,na je kabla ya hapo alikuwa haoni kuwa watanzania wanahitaji msaada wake? Tafadhali maelezo na ufafanuzi hapo.
 
Katika watu waliofukuzwa na CC ya CDM, ni KITILA MKUMBO tu aliyestahili japo kupata ka MSAMAHA, Lakini sasa kwa jinsi anavyojinadi kwenye media za wenzetu ni dhahili kabisa kwamba hata huyu jamaa hastahili aina yoyote ya kitu kinachoitwa MSAMAHA.Watu wengi sana walijenga mawazo hasi kwa CC kumfukuza kitila kwa sababu alionekana kama vile kujutia makosa yake lakini kwa kile anachoendelea kukifanya kupitia MEDIA kinampoteza bila yeye kujua.Mimi binafsi nimekuja kugundua kuwa kitila ni msomi mwenye elimu nzuri kutoka kwenye vitabu lakini bwana KITILA MKUMBO anaupungufu wa elimu ya kuzaliwa ambayo ndo inayomwongoza binadamu kwa 60% ya maisha yake.BUSARA ya mtu haitokani na kwamba amesoma mpaka level gani ya elimu lakini busara ya mtu ni kipaji ambacho MUNGU anagawa kwa kila binadamu kulingana na utashi wake kwake.Pia busara huboreshwa zaidi na mazingira ambamo mtu huyo amekulia.Hivyo basi bwana kitila anaupungufu wa elimu ya kuzaliwa ndo maana watu wamekuwa wakishudia jinsi gani bwana huyu alivyokuwa akifuata mkumbo wa akina ZITO na MWIGAMBA.
 
Nakubaliana na wewe kwamba asamehewe iwapo atakubali kuomba msamaha. Ni wakati mzuri kwa wale tulio karibu na Mkumbo kumshawishi afanye hivyo kwa faida yake na ya chama.
Mkuu Kyafulili, tangu mwanzo nimekuunga mkono bandiko lako kwa humility ulioonyesha, ila kuna jambo moja muhimu sana nimeligiundua kwako hapo mwanzo nililiover look!.

Unakubaliana na maamuzi ya CC ya Chadema, they did the right thing, Kitila ni mkosaji aliyestahili adhabu ile!. Huu nao mimi nauita ni upofu uliosababishwa na mahaba makubwa kwa Chadema!.

Kitila ni an academician, ule waraka ni an academic paper ya regime change through "a winning coalition" through the normal electoral process ya ndani ya chana!, hakuna uhaini wowote pale wall hakuna mapinduzi yoyote pale!, it was a regime change only!.

Masikini CC ya Chadema imejaa vilaza wengi zaidi kuliko wasomi!, na baadhi ya wasomi wenu ni wasomi wa divinity, kwao mawazo yoyote tofauti yanatafsiriwa kama uasi, hivyo nao hawakuweza kuona "the motive behind" waraka ule, wakaishia kuuita uhaini na kutoa hukumu iliyopaswakwa wahaini!.

Kitendo cha Kitila kuomba msamaha, ni kukubaliana na upuuzi wa CC ya Chadema!. Nilisema watu wenye sense kama wewe ndio wangeweza kuokoa Chadema kwa CC kujitathmini, na kurudi kumomba msamaha Kitila kwa kumsingizia uhaini!. Kwa vile ni vigumu sana baba kumuomba msamaha mtoto aliyemuadhibu kwa makosa, baba atajisikia kuwa mdogo kama piriton, the African way ni baba kwenda kwa babu, (baraza Kuu), na kumueleza babu, nimemkosea mtoto!, Babu ndie atamuita mtoto, na kumweleza shetani alimpitia baba na kufanya yasiyo paswa, yule ni baba yako, anakupenda ndio maana alikudhibu kwa makosa, amejuta, msamehe, muheshimu, mtashikana mikono na baba, mtasameheana, mtakumbatiana na maisha yatasonga mbele!.

Sijawahi kuipitia CV ya Kitila, ila ukimsoma, utajiridhisha jamaa ana very high IQ, ni level ya kina Beregu, Safari, Mnyika etc. Akifuatilia arguments za wengi wa viongozi wenu wana ordinary IQ na wengine low IQ, hivyo kitendo cha kumpoteza kitila, hawa ordinary na low IQ wanaona poa, kwa sababu kwao Kitila was just a person tuu kama alivyo Sugu au kiongozi mwingine yoyote!, wale wenye high IQ wanaumia kwa sababu kumpoteza Kitila kwao sio issue, kwao issue ni kuipoteza ile "the best brain", hivyo Chadema ku suffer "brain drain", naamini hapa unanielewa!. Kwa Chadema kumfukuza Kitila, it has everthing to loose and nothing to gain!", kwa Kitila kufukuzwa Chadema, he has nothing to loose, (except time and efforts alizotumia na kupoteza), kwa sababu amefukuzwa na brain yake anayo!, and has everything to gain kwa kuivest anywhere else!. Hivyo the loosers ni Chadema na sio Kitila!, aombe msamaha kwa kosa gani?!.
Pasco.
 
Siungi mkono kitila kuomba radhi Ben Saanane aliomba msamaha sababu ana kazi nyingine zaidi ya kulamba viatu vya wakubwa
 
Last edited by a moderator:
Ulaaniwe kwa kuleta udini na ukabila!

Ww kama huna macho utasubir sana kulijua hilo tired aka uliyechoka. Wajanja tushabaini hilo. Chademangi ni chama cha kaskazini. Wafuga nguruwe wamejaa.
 
Mkuu Kyafulili, tangu mwanzo nimekuunga mkono bandiko lako kwa humility ulioonyesha, ila kuna jambo moja muhimu sana nimeligiundua kwako hapo mwanzo nililiover look!.

Unakubaliana na maamuzi ya CC ya Chadema, they did the right thing, Kitila ni mkosaji aliyestahili adhabu ile!. Huu nao mimi nauita ni upofu uliosababishwa na mahaba makubwa kwa Chadema!.

Kitila ni an academician, ule waraka ni an academic paper ya regime change through "a winning coalition" through the normal electoral process ya ndani ya chana!, hakuna uhaini wowote pale wall hakuna mapinduzi yoyote pale!, it was a regime change only!.

Masikini CC ya Chadema imejaa vilaza wengi zaidi kuliko wasomi!, na baadhi ya wasomi wenu ni wasomi wa divinity, kwao mawazo yoyote tofauti yanatafsiriwa kama uasi, hivyo nao hawakuweza kuona "the motive behind" waraka ule, wakaishia kuuita uhaini na kutoa hukumu iliyopaswakwa wahaini!.

Kitendo cha Kitila kuomba msamaha, ni kukubaliana na upuuzi wa CC ya Chadema!. Nilisema watu wenye sense kama wewe ndio wangeweza kuokoa Chadema kwa CC kujitathmini, na kurudi kumomba msamaha Kitila kwa kumsingizia uhaini!. Kwa vile ni vigumu sana baba kumuomba msamaha mtoto aliyemuadhibu kwa makosa, baba atajisikia kuwa mdogo kama piriton, the African way ni baba kwenda kwa babu, (baraza Kuu), na kumueleza babu, nimemkosea mtoto!, Babu ndie atamuita mtoto, na kumweleza shetani alimpitia baba na kufanya yasiyo paswa, yule ni baba yako, anakupenda ndio maana alikudhibu kwa makosa, amejuta, msamehe, muheshimu, mtashikana mikono na baba, mtasameheana, mtakumbatiana na maisha yatasonga mbele!.

Sijawahi kuipitia CV ya Kitila, ila ukimsoma, utajiridhisha jamaa ana very high IQ, ni level ya kina Beregu, Safari, Mnyika etc. Akifuatilia arguments za wengi wa viongozi wenu wana ordinary IQ na wengine low IQ, hivyo kitendo cha kumpoteza kitila, hawa ordinary na low IQ wanaona poa, kwa sababu kwao Kitila was just a person tuu kama alivyo Sugu au kiongozi mwingine yoyote!, wale wenye high IQ wanaumia kwa sababu kumpoteza Kitila kwao sio issue, kwao issue ni kuipoteza ile "the best brain", hivyo Chadema ku suffer "brain drain", naamini hapa unanielewa!. Kwa Chadema kumfukuza Kitila, it has everthing to loose and nothing to gain!", kwa Kitila kufukuzwa Chadema, he has nothing to loose, (except time and efforts alizotumia na kupoteza), kwa sababu amefukuzwa na brain yake anayo!, and has everything to gain kwa kuivest anywhere else!. Hivyo the loosers ni Chadema na sio Kitila!, aombe msamaha kwa kosa gani?!.
Pasco.

Huyu jamaa huwa haeleweki mara kule mwanzo ulisema chadema kuna udini na ukabila. Leo tena unageuka mara akiri kubwa haendani na akiri ndogo. Pasco wewe endelea na karata yako ya udini na ukabila kwa chadema acha porojo zingine.
 
Kafyulila umenena! ninaunga mkono kauli yako. lakini ninaongeza pia kwamba kama mimi ningekuwa baraza kuu ningefanya maamuzi magumu ya kuwasamehe wote watatu lakini kwa kutoa onyo kali kwamba wamejifunza wasirudie jaribio lile na linalofanana nalo. wote waendelee kuwa wanachama wa kawaida adhabu ya kuwaondoa kwenye nyadhifa zao iendelee.
 
Siyo kila anayekuja na mawazo tofauti au mtizamo tofauti ni mwanaCCM. Acheni utoto huo. Ni kwa lipi baya nililomsema Ben Saanane? Sijawahi kutofautiana na Ben Saanane, ila nimemtolea mfano tu, focus ya mjadala hapa ni Kitila, kama una la kuchangia kuhusu Kitila fanya hivyo.


Hivi wewe kwa akili yako unafikiri Ben Saanane aliisaliti CDM au alikuwa kwenye mission ya kuwafichua wasaliti? Ben hajawahi kuwa msaliti na hivyo hakuhitaji kusamehewa ila tu 'msamaha' ilikuwa ni kutafuta neno zuri la kuwafanya nyie vilaza muelewe....
 
Mbona Lowassa hajawahi kuponda ufisadi,hajawahi kukubali ama kukanusha ile kashfa ya RICHMOND pia kwanini anatumia pesa nyingi kuhonga makanisani na misikitini pamoja na boda boda anachokitaka kwa watanzania hawa haswa ni nini maana huu mchakato umeanza pindi alipojiuzuru tu uwaziri mkuu,na je kabla ya hapo alikuwa haoni kuwa watanzania wanahitaji msaada wake? Tafadhali maelezo na ufafanuzi hapo.
Mkuu Ndikwe, unakumbuka jinsi alivyowafurusha City Water?!, amini nakuambia, alitaka kuwatimua Richmond siku nyingi ila ...(naamini unaijua sababu!).
Hizo pesa anatumia sio kuhonga bali kusaidia, its only for support!. Akifanikiwa kufika kule juu, ataigeuza Tanzania kuwa ni nchi ya hahadi, itakuwa nchi ya maziwa na asali!. Yaani ataigeuza pepo!.
Pasco
 
Cdm iko sahihi na anayelalamika ndo mwenye shida akaombe radhi
 
Huyu jamaa huwa haeleweki mara kule mwanzo ulisema chadema kuna udini na ukabila. Leo tena unageuka mara akiri kubwa haendani na akiri ndogo. Pasco wewe endelea na karata yako ya udini na ukabila kwa chadema acha porojo zingine.
Pole sana Mkuu Mkama Rumanyika, unahitaji level fulani ya uelewa kunielewa!, ukiendelea kunisoma soma, uelewa wako utaimprove na labda utaanza kunielewa, kwa sasa all I can say is just sorry!.
Pasco
 
Kusamehe ni jambo la kawaida kabisa kwenye maisha yoyote yale lakini kwa hivi sasa hata Mkumbo atakubali kwenda kwenye chama alichotangaza waziwazi kuwa hakifai na pia kuongozwa na mtu ambae yuko "too local".
Kwahiyo hata yeye mwenyewe nafsi yake haitamruhusu kabisa!
 
pole sana mkuu mkama rumanyika, unahitaji level fulani ya uelewa kunielewa!, ukiendelea kunisoma soma, uelewa wako utaimprove na labda utaanza kunielewa, kwa sasa all i can say is just sorry!.
Pasco

unapojivika busara na uwezo bora wa kufikiri wakati mawazo yako yenyewe yanapingana yenyewe kwa yenyewe sikuelewi!

Au hako kasheria uchwara kana kufanya ujenge hulka mujwabini za kujiona mwenye fikara makini wakati ni umalipyoto tu ndio ukusumbuao kijana wangu!
 
Hivi wewe kwa akili yako unafikiri Ben Saanane aliisaliti CDM au alikuwa kwenye mission ya kuwafichua wasaliti? Ben hajawahi kuwa msaliti na hivyo hakuhitaji kusamehewa ila tu 'msamaha' ilikuwa ni kutafuta neno zuri la kuwafanya nyie vilaza muelewe....
Kama jambo hulijui jitahidi basi kunyamaza kimya. Ukipayuka payuka kama unavyofanya unaonekana hayawani. Fuatilia chanzo cha Ben kuingia kwenye kile kikundi cha masalia, usikurupuke tu.
 
Mkuu Kyafulili, tangu mwanzo nimekuunga mkono bandiko lako kwa humility ulioonyesha, ila kuna jambo moja muhimu sana nimeligiundua kwako hapo mwanzo nililiover look!.

Unakubaliana na maamuzi ya CC ya Chadema, they did the right thing, Kitila ni mkosaji aliyestahili adhabu ile!. Huu nao mimi nauita ni upofu uliosababishwa na mahaba makubwa kwa Chadema!.

Kitila ni an academician, ule waraka ni an academic paper ya regime change through "a winning coalition" through the normal electoral process ya ndani ya chana!, hakuna uhaini wowote pale wall hakuna mapinduzi yoyote pale!, it was a regime change only!.

Masikini CC ya Chadema imejaa vilaza wengi zaidi kuliko wasomi!, na baadhi ya wasomi wenu ni wasomi wa divinity, kwao mawazo yoyote tofauti yanatafsiriwa kama uasi, hivyo nao hawakuweza kuona "the motive behind" waraka ule, wakaishia kuuita uhaini na kutoa hukumu iliyopaswakwa wahaini!.

Kitendo cha Kitila kuomba msamaha, ni kukubaliana na upuuzi wa CC ya Chadema!. Nilisema watu wenye sense kama wewe ndio wangeweza kuokoa Chadema kwa CC kujitathmini, na kurudi kumomba msamaha Kitila kwa kumsingizia uhaini!. Kwa vile ni vigumu sana baba kumuomba msamaha mtoto aliyemuadhibu kwa makosa, baba atajisikia kuwa mdogo kama piriton, the African way ni baba kwenda kwa babu, (baraza Kuu), na kumueleza babu, nimemkosea mtoto!, Babu ndie atamuita mtoto, na kumweleza shetani alimpitia baba na kufanya yasiyo paswa, yule ni baba yako, anakupenda ndio maana alikudhibu kwa makosa, amejuta, msamehe, muheshimu, mtashikana mikono na baba, mtasameheana, mtakumbatiana na maisha yatasonga mbele!.

Sijawahi kuipitia CV ya Kitila, ila ukimsoma, utajiridhisha jamaa ana very high IQ, ni level ya kina Beregu, Safari, Mnyika etc. Akifuatilia arguments za wengi wa viongozi wenu wana ordinary IQ na wengine low IQ, hivyo kitendo cha kumpoteza kitila, hawa ordinary na low IQ wanaona poa, kwa sababu kwao Kitila was just a person tuu kama alivyo Sugu au kiongozi mwingine yoyote!, wale wenye high IQ wanaumia kwa sababu kumpoteza Kitila kwao sio issue, kwao issue ni kuipoteza ile "the best brain", hivyo Chadema ku suffer "brain drain", naamini hapa unanielewa!. Kwa Chadema kumfukuza Kitila, it has everthing to loose and nothing to gain!", kwa Kitila kufukuzwa Chadema, he has nothing to loose, (except time and efforts alizotumia na kupoteza), kwa sababu amefukuzwa na brain yake anayo!, and has everything to gain kwa kuivest anywhere else!. Hivyo the loosers ni Chadema na sio Kitila!, aombe msamaha kwa kosa gani?!.
Pasco.
Kaka, Pasco, kwanza nimefarijika kusoma story yako ambayo imechimbua hadi ndani kabisa na kueleza hisia zako zote kuhusu sekeseke linaloendelea. Ninaomba nijibu kama ifuatavyo:

Kwanza bado nabaki kwenye msimamo ule ule wa kuunga mkono maamuzi ya CHADEMA ya kuamua kuwaadhibu kwa kile kilichokuwa kinaendelea. Ninaunga mkono maamuzi haya kwa sababu mtindo na utaratibu wa kutafuta madaraka uliotumiwa na kikosi hiki, haukuwa na mstakabali mzuri kwa chama. Utakumbuka kuwa kama sehemu ya utekelezaji wa mikakati ya waraka ule, Samsoni Mwigamba alitengeneza ID iliyoitwa mkulima masikini na akaitumia hiyo kuwananga viongozi wa chadema humu JF, huku akiwatuhumu kwa mengi yakiwemo ya kubadilisha vipengele vya katiba, tuhuma ambazo alishindwa kuzidhibitisha. Unakumbuka vema namna ambavyo makala za mwigamba humu jamvini ziliharibu taswira ya CHADEMA, nakuonekana ni chama ambacho viongozi wake wanakula ruzuku/wanatumia ruzuku kwa mambo yao binafsi na kujinufaisha bila kukisaidia chama. Unakumbuka kwamba skendo za Mbowe kutembea na Mbunge wake na kujenga nyumba huko Dubai ziliibuliwa katika kipindi kile?

Nataka tu kukuuliza Pasco, na kwa kutumia busara ya kawaida tu, CCM inachukiwa na wananchi kwa kuwa ina sera mbaya au kwa kuwa ina viongozi wabaya? Nataka niseme, hakuna namna yoyote unayoweza kuwachafua viongozi wakuu wa chama pasipo kukichafua chama? Kwa kuwachafua viongozi wa juu wa chama ni kukimaliza chama na si kukijenga. Katika hilo hawa ndugu zetu wakubali kuwa walifanya kosa.

Pili, Zitto alishakuwa na mienendo yenye kutilia mashaka tangu zamani, akianza na kukalia report ya uchunguzi wa mkataba wa madini wa Buzwagi, kupewa nafasi ya kuongozana na JK kwenda Sudan kusini kumwapisha Rais mpya wa huko bila kuwa na sababu zozote - jambo lililotafsiriwa kama ni rushwa, kuwasaliti wenzake wakati wa mpango wa kutoka bungeni ili kumpinga JK, kuanzisha na kufadhili kikundi cha masalia, nk. Katika mlolongo wa sintofahamu hizi ambazo zimejitokeza huko nyuma, ilikuwa ni aghalabu sana kwa CHADEMA kumsamehe mtu kama Zitto ambaye tangu mwanzo alionyesha kutafuta umaarufu wa yeye peke yake na si wa chama. Ikumbukwe pia Zitto alitiliwa shaka kwenye sakata la Lwakatare, ambapo yeye pekee aliandika barua kutaka chama kimtose Lwakatare, huku akijua kwamba Lwakatare angetoswa asingekuwa na uwezo wa kulipia gharama za kesi na hivyo angeshindwa kesi na pengine angewekewa maneno yenye kukifanya CHADEMA kifutwe. Mlolongo wa matukio ya Zitto yalimfanya ashindwe kuvumiliwa katika hili. Likewise, Mwigamba ambaye hakufanya vema alipokuwa mhasibu wa chadema makao makuu.

Katika hayo, naona ya kwamba akina Kitila walifanya kosa, ambalo kiujumla hata Kitila mwenyewe alilikubali na akawa radhi kuachia ngazi. Na hapo ndipo ninaposema kwa ustaarabu na uungwana aliouonyesha Kitila kwa CHADEMA wakati wa sakata hili, tofauti na walivyofanya wenzake, kwa hakika anastahili msamaha. Lakini pia kwa kuwa alikubali kosa na akawa tayari kujiuzuru, si vibaya pia akubali kuomba msamaha kwa faida ya chama na kwa faida yake.

Najua kwamba inawezekana kutokana na hasira au vinginevyo amefikia mahali pa kukata tamaa na kukiona CHADEMA si mbadala mzuri wa CCM, lakini naamini kama atapewa nafasi nyingine anaweza kuwa msaada mkubwa sana kwetu na akakisaidia chama chetu kuwa mbadala halisi wa CCM. Daima kama binadamu tunajifunza kutokana na makosa. Hakuna msafi hata mmoja kati yetu. Tofauti na akina Zitto na Mwigamba ambao walishakuwa wanakosea na kuonywa several times na hawakubadilika, Kitila hili ni kosa lake la kwanza. Apewe onyo, bila shaka ameshajifunza na amejua ni wapi alipoharibu. Yafaa asamehewe aendelee kusaidiana na wapambanaji wengine ndani ya CHADEMA.

Kitila ni mtu wangu wa karibu, namfahamu kwamba ni mpambanaji, ana rekodi nzuri ya kazi kila alipowahi kwenda, amekuwa mkuu wa kitivo pale DUCE kwa miaka isiyozidi miwili kafanya mambo ambayo hayalinganishwi na yaliyofanya na watangulizi wake waliokaa kwa muda mrefu. Ni mbunifu, mwenye IQ kubwa. Lakini zaidi ya yote, kwa asili yake Kitila Mkumbo ni mwanasiasa. Yeye na siasa hawatenganishiki, lakini kwa uwezo wake na upenda mageuzi wake, sioni pengine panapomfaa zaidi ya CHADEMA. Kitila hawezi kuwa mwanaCCM kwa kuwa hataweza kabisa kuendena na sera za ndiyo mzee, sioni chama kingine chochote cha siasa nje ya CHADEMA ambako Kitila ataweza kudemonstrate uwezo wake halisi wa kufanya mambo. Itapendeza kwa hakika wakubwa wetu hawa ndani ya CHADEMA wafikirie upya kuhusu huyu bwana, tunaweza kuwa na hasira nyingi sana dhidi yake lakini haitasaidia chochote. Mtoto akinyea mkono hatuukati, bali tunauosha na kumkanya mtoto asijisaidie mikononi tena.

Pasco umeongea kuhusu suala la nani aombe msamaha, na umekosoa wazo langu la kwamba Kitila Mkumbo aombe msamaha, lakini mimi napenda niwe mkweli katika hili. Hakuna namna yoyote ambayo CHADEMA watafikiria kumtafuta Kitila na kuomba msamaha. Hivyo ndivyo wakubwa walivyo, hata siku moja hawapendi kuonekana kwamba wamewapigia magoti walio wadogo kwao. Lakini kwa kuwa sisi tunamhitaji Kitila ndani ya chama, tunayo nafasi ya kumwombea msamaha, na ikiwezekana tunayo nafasi ya kumsindikiza kwenda kuomba msamaha. Wazo la kuomba msamaha ni lazima liwe initiated na Kitila mwenyewe akisaidiana na sisi. Hawa walio juu hawawezi hata siku moja kukubali kula matapishi yao wenyewe. Alifanya hivyo Kafulila na mambo yametulia sasa. Wakati mwingine ni vizuri kuwa mpole kwa ajili ya kuokoa mambo mengine mengi na makubwa kwa faida yako binafsi na ya taifa.

Bado naona Kitila ana msaada mkubwa kwa taifa letu kupitia chadema. Tukishika madaraka ya nchi hii kitila ni potential Minister of Education. Kuna ubaya gani akipiga magoti na akalifaa taifa letu katika nafasi ya waziri wa elimu huko mbeleni? Watu wanadhani akitubu atakuwa amedhalilika, lakini wanasahau impact yake kwa taifa baada ya kukubali hicho tunachodhani ni kujidhalilisha. Bado naona kuna haja ya kitila kukubali kupiga magoti ili yaishe. Yamewezekana kwa Kafulila why not Mkumbo. CHADEMA kinaongozwa na binadamu ambao pia wana mapungufu yao mengi tu, tunaamini hawataliangalia sana hili kosa moja la Kitila na kusahau mambo makubwa mengi aliyokifanyia chama na nchi. Na ni imani yangu kwamba hawa watu wanaoongoza CHADEMA, wanayatazama pia mapungufu yao na kutambua kwamba Kitila kateleza kama ambavyo hata wao waliwahi kuteleza hapo awali au wanavyoteleza kila siku. Tusameheane tusonge mbele.
 
Ndiye nani huyu Mkumbo sijui Kitilya, tushamsahau, hivi ana sifa gani vile???
 
Back
Top Bottom