Ninatafuta mpenzi/mume nipo serious

Ninatafuta mpenzi/mume nipo serious

Kwann utafute mume wa mtandaoniiiii
Popote tu dada mume anapatikana. Kumbuka umri wangu ni miaka 47 kwa hiyo si rahisi sana kumjua mgane au mtalaka kwa kuwa hawaandikwi mgongoni. Ila pia kupitia njia hii nimejifunza sana mambo mengi hasa uongo na utapeli. Sasa mimi huwa nina uwezo mkubwa sana wa kuwatambua hawa viumbe wa namna hii na haichukui round unakuwa nje ya mjadala tu. Ninatumaini umenielewa.
 
Ukweli ni kazi ngumu sana. Matapeli ni wengi na wanafiki pia. Ila kwangu waligonga mwamba. Ningekuwa ninatafuta waume za watu au wale wanaume wanaotaka kulelewa na wanawake ungekuta ninao wengi sana ila kwa kuwa nilikuwa makini sana niliweza kugundua uongo mwingi sana. Tena waogope sana wale ambao wanajifanya ni wacha Mungu. Ni eneo la kuficha uongo tu. Nilitumia mbinu kubwa sana kuwanasa wengine na uongo wao. Kwa hiyo kwa sasa niko na mambo yangu zaidi kimaisha.
kwa hakika wenye kusubiri wako na pamoja na allah (t.w) in shaa allah kila lenye khairat liwe upande wako.
 
47 mingi sana bana dhaaa
Kwa hiyo unataka kitu gani? Wako wenzako waliondanganya umri ili tu waweze kuwa na mimi . Ila in the process ya kufahamiana huwa nikikutana na uongo hata punze maana yake huna uaminifu na hunifai pia. Bora uwe mkweli kuanzia awali ili mimi niweze kuamua kuliko udanganye it means mtu tayari anaanza uongo from the beginning sasa mkiwa pamoja si hatari sana hiyo?
 
sawa my dia nime elewa sema nili sema 47 kwa mtu wa kuoa ni shida sana hao wanao danganya miaka sindo vijana wakina sisi
 
kwa hakika wenye kusubiri wako na pamoja na allah (t.w) in shaa allah kila lenye khairat liwe upande wako.
Amina. Ninaamini kama Mungu ameniandikia kuwa na mwenza wa upendo wa kweli, mwaminifu na asiye na uongo au kuficha mambo basi atamleta siku moja. Ukweli niko makini na huwa ninauliza maswali mengi sana tena ya kutega na inanisaidia sana kwa kuwa wapo ambao hawajui jana walisema nini na leo wametunga kitu gani cha kudanganya. Kuna mmoja huyo stamsahau kwa ufundi wa uongo na unafiki katika eneo ambalo kwangu lilikuwa ni kigezo kikubwa sana ila kwa kuwa ninamshirikisha sana Mungu aliweza kunifunulia ukweli na siku moja nitamwambia ukweli wake kwa kuwa kidogo karibu ningeamini sana na kuona anafaa.
 
Acha upumbavu wako mpnz anatafutwa sehem yyte ile
Ohh my dear umesema ukweli ila just mweleweshe taratibu ataelewa kwa lugha nyepesi please. Mimi nitampata tu na nina uhakika haitachukua muda mrefu. Hata hapa inawezekana yupo ila tu hajaona post yangu.
 
God is in control... utapata mama usijar...stand by ur faith
Amina tuombeana uzima na ukweli nitaweka hapa kwa kuwa nilianzia hapa pia hata kama sikumpatia hapa ila nitawaeleza kwa kuwa nimeshukuru sana wengi wa waliojibu post yangu wamekuwa na maoni mazuri sana. Ukweli nimekutana mpaka na watumishi wa Mungu humu au niseme watu ambao wana imani na wamenielekeza hata maeneo ambayo ninahitaji kutulia zaidi na kumuomba Mungu na pia kuonana na washauri wa dini pia na mengine mengi tu. Hivyo kwangu ni mafanikio makubwa sana sana. Na niwashukuru sana watumishi wote humu waliotumia muda wao PM kuongea na mimi kimaadili zaidi na wamenisaidia sana kuongeza uelewa wangu wa kuwanasa waongo.
 
shikamoo ant, ngoja tumuombe Mungu amulete anko
Amen sana cma na please omba kwa kumaanisha usilete utani kwa kuwa inahitajika Mungu afanye kazi yake zaidi. Atakuja kwa majira yake mola. Asante
 
  • Thanks
Reactions: cma
Utapata tu mwenza wa kusukuma muda,sisi bado kidogo kufikia hiyo status.
 
Utapata tu mwenza wa kusukuma muda,sisi bado kidogo kufikia hiyo status.
Asante sana. Lengo kubwa ni kuwa na kampani tu ya kupeana mawazo ya hapa na pale. Unajua tuna watoto ila watoto nao wanakuwa na wanatoka mikononi mwako na unabaki mwenyewe nyumbani. Kwa misingi hii life partner ni zaidi ya watu wanavyofikiria kuwa ni ngono pekee. La hasha, hata kuwa na social interactions nyinginezo ambazo kwa watu wa umri mkubwa ni muhimu mno kupita mambo mengine yote. Kwa misingi hii ninaomba watu waelewe tu hivyo. Kama ni suala la ngono ninaweza kuamua kumpata mahali popote tu na ninaendelea na upwekwe wangu but maisha ya utu uzima ni zaidi ha hapo.
 
Uenipata ila kigezo ambae ajaoa du,mie sijaoa ila na watoto 3 kama utapenda,maisha nayamudu nimwajiliwa serikalini,nipo serious
 
Uenipata ila kigezo ambae ajaoa du,mie sijaoa ila na watoto 3 kama utapenda,maisha nayamudu nimwajiliwa serikalini,nipo serious
Hongera sana kwa kuwa baba wa Watoto watatu. Ninajiuliza hao Watoto mama zao au mama yao imekuwaje tena usimuoe?
 
Back
Top Bottom