Miss Halima
JF-Expert Member
- Aug 4, 2026
- 307
- 682
Lorna Fidelia hufanya kazi ya kuwabebea wengine uja uzito. Amewahi kubeba mimba ya pacha watatu miaka michache iliyopita na sasa anatafuta kubeba mtoto mwingine.
Lorna ni miongoni mwa wanawake waliokumbatia kazi hii ili kuzisaidia familia ambazo zimekosa kupata watoto .
Nilikaa chini nikawaza nimekuwa single mother miaka mingi. Nikakaa nikafikiria mimi niko na hawa watoto Ninafanya kazi hata pesa haitoshi lakini kuna mtu ambaye hana watoto ako na provision anaweza afford rent, food , shule na hana mtoto. Nikaona naweza kusaidia mtu hana watoto at the same time anisaidie mimi na Watoto wangu" Lorna Fidelia
Kabla ya kukubalika kubeba uja uzito, anayebeba mimba na wazazi wa toto huandikishana mkataba wa kisheria. Katika mkataba huo, wanakubaliana malipo na vipengee kama vile anayebeba mimba kutokuwa na haki ya kumchukua mtoto anayezaliwa.
Baada ya hapo , mchakato mzima huanza hospitalini ambapo mtaalamu wa mayai ya uzazi huwapima wazazi husika na kutoka mayai ya kiume na ya kike kabla ya kupima afya ya anayebeba mimba alafu kufanya upandikizaji
Daktari Susan Karanja ni mtaalamu wa upandikizaji mimba katika hospitali ya Nairobi West jijini Nairobi anasema nchini Kenya anayebebea wengine mimba anafaa kuwa kati ya umri wa miaka 25 hadi 45 na hufanyiwa vipimo vya afya kabla ya kukubalika.
'Huyu surrogate anapitia mchakato wa uchunguzi wa kiafya. Anaangaliwa kama yuko sawa, je damu yake iko sawa tukishamaliza daktari anaangalia nyumba ya mtoto kama iko sawa. Tukishatoa yale mayai mume anatoa mbegu zake tunachukua zile mbegu na mayai ya mke tunakutanisha alafu tunamuwekea huyo surrogate anayebeba mimba kwenye nyumba ya uzazi.'
Baada ya upandikizaji, anayebeba mimba hupumzika bila kufanya kazi ngumu ili asihatarishe uja uzito.
Lorna ni miongoni mwa wanawake waliokumbatia kazi hii ili kuzisaidia familia ambazo zimekosa kupata watoto .
Nilikaa chini nikawaza nimekuwa single mother miaka mingi. Nikakaa nikafikiria mimi niko na hawa watoto Ninafanya kazi hata pesa haitoshi lakini kuna mtu ambaye hana watoto ako na provision anaweza afford rent, food , shule na hana mtoto. Nikaona naweza kusaidia mtu hana watoto at the same time anisaidie mimi na Watoto wangu" Lorna Fidelia
Kabla ya kukubalika kubeba uja uzito, anayebeba mimba na wazazi wa toto huandikishana mkataba wa kisheria. Katika mkataba huo, wanakubaliana malipo na vipengee kama vile anayebeba mimba kutokuwa na haki ya kumchukua mtoto anayezaliwa.
Baada ya hapo , mchakato mzima huanza hospitalini ambapo mtaalamu wa mayai ya uzazi huwapima wazazi husika na kutoka mayai ya kiume na ya kike kabla ya kupima afya ya anayebeba mimba alafu kufanya upandikizaji
Daktari Susan Karanja ni mtaalamu wa upandikizaji mimba katika hospitali ya Nairobi West jijini Nairobi anasema nchini Kenya anayebebea wengine mimba anafaa kuwa kati ya umri wa miaka 25 hadi 45 na hufanyiwa vipimo vya afya kabla ya kukubalika.
'Huyu surrogate anapitia mchakato wa uchunguzi wa kiafya. Anaangaliwa kama yuko sawa, je damu yake iko sawa tukishamaliza daktari anaangalia nyumba ya mtoto kama iko sawa. Tukishatoa yale mayai mume anatoa mbegu zake tunachukua zile mbegu na mayai ya mke tunakutanisha alafu tunamuwekea huyo surrogate anayebeba mimba kwenye nyumba ya uzazi.'
Baada ya upandikizaji, anayebeba mimba hupumzika bila kufanya kazi ngumu ili asihatarishe uja uzito.