Mwenzenu kuna mambo huwa yananitokea nikiyawaza najihisi nina tatizo ila suluhu yake ndo shida kwangu. Naombeni ushauri nifanyeje niwe na positive mind kila wakati.
- Nikikosana na shemeji yenu, na/au ikitokea nimekaa muda mrefu bila kupata huduma ninakuwa na hasira za ajabu ajabu. Siku hiyo ofisini ninaofanya nao kazi inabidi wawe careful au akija mteja nimhudumie basi nakuwa na majibu ya mkato na ghadhabu mpaka watu wananiogopa. Mtu akichemsha kidogo tu naweza mtoa baru. Baadaye nikija kuongea na mtu in a very polite way, au nikimtokea mtu nimempenda, jambo la kwanza ananiambia mbona wewe mkali sana. Hii kitu inaniumiza.
- Kuna wakati nakuwa mpole sana kuliko maelezo. Ninakuwa very charming, very positive and you can really enjoy kuwa na mimi. Hapo nikianza kupigisha story siishiwi iwe siasa, dini, elimu, mapenzi, biashara au chochote.
- Kuna wakati ninakuwa na hali ya kupenda sana yaani inakuwa tabu kweli. Nikimtokea mtu nimempenda hapo i can do anything.
- Kuna wakati nawachukia wanawake wote kasoro mama yangu. Najikuta sina hamu ya mapenzi, alafu nikikumbuka michepuko niliyowahi kutoka nayo najiona ----- kweli. Sasa wakati huo ikitokea kuna mchepuko ananitaka nitoke naye anaweza akajuta kunifahamu. Hapo nawaza maisha yangu tuu, na sitaki mtu anisemeshe. Ila baadaye hii hali ikipita nakuja kumuomba msamaha.
- Kuna wakati narudia mambo ya Mungu, nakwenda kanisani nafanya kila niwezalo, natubu dhambi zangu zote, naimba kwaya, natoa michango, yaani mpka naona raha.
- Kuna wakati huko kanisani nako kunaanza kuboa, najikuta narudi mawazo ya mwanzo, especially nikiona huko kanisani yanayofanyika ndivyo sivyo. Hapo ni rahisi sana kurudia kule kwa michepuko.