Nina tabia ya kuahirisha mipango(plans)

Nina tabia ya kuahirisha mipango(plans)

boyson onlye

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2015
Posts
1,108
Reaction score
1,404
Habarini

Blood group yangu ni O

Ninatabia ya kutokamilisha mipango yangu, yaani naweza nikapanga jambo/biashara/masomo then nikaanza utekelezaji nikifika njian kwenye utekelezaji naghairi kabisa, ni mwepesi sana wa kukatishwa tamaa, nafikia hatua najichukia kabisa, sioni shida kuacha kitu nilichokianzisha hata kama nimetumia gharama, lakini nikikaa huwa nakuwa na mipango mizur sana,

Naweza nikawaza kufanya biashara flani nikafanyia research kila kitu ila mtu akija na wazo la biashara nyingine basi hili la kwanza naliweka kapuni mda huohuo



Wakuu naombeni msaada wenu hii hali ya kutopambana na kitu ninachokianzisha mpaka kiishe inaniumiza sana, nawaza vitu vingi sana na nataka nivifanye kwa pamoja, najaribu kujizuia nashindwa

Najikuta napoteza mda mwingi bila kufanya chochote

Msaada wa kimawazo jinsi gani niitawale akili yangu na kusimamia mawazo yangu
 
Mkuu pole sana,unaumwa mwagonjwa mawili ya kisaikolojia ambayo ni "procastination" na "perfectionism",procastination ni tabia ya kupenda kuairisha mambo unayokuwa umepanga kufanya na perfectionisma ni tabia ya kupenda ukamilifu kwenye kila jambo unalotaka kulifanya,Magonjwa haya yanawatesa wengi sio wewe peke yako,Tiba zipo ila hapa sitoweza kueleza kila kitu nacho kushauri,weka nia ya kubadilika na uanze kutoarisha mipango yako midogo midogo hiyo itakujengea tabia ya kutoarisha hata mipango yako mikubwa na upende kuwa na vipaombele vya mipango yako ya maisha huwezi kufanya kila kitu kwa wakati mmoja na vikafanikiwa sana!
 
Back
Top Bottom