Nina mashaka, Pengine Lowassa ndio 'Goli la Mkono'

Nina mashaka, Pengine Lowassa ndio 'Goli la Mkono'

Critical kwelikweli, anyway in the end Lowassa hamaanishi anachokitafuta na yeye analielewa vyema hilo
 
Uchaguzi huu ni kati ya ccm na cuf . Hakuna cha CHADEMA wala nccr au NLD.
Ccm - pombe, lowasa na Samira
Cuf- Duni haji , maalim seif

CHADEMA wanacheza vibwagizo mziki Wa ccm wa tunaimani na lowasa. Hii imani na lowasa ilianza lini ?

Ni maoni Yangu msije mkaanza kuniponda mawe humu .
 
Ndo maana nikasema hii nchi ni rahisi mno kuudhoofisha upinzani sema hakuna strategic plans za kufanikisha hilo sababu wenye hiyo dhamana ni wavivu wa kufikiri.

Tuseme zengwe lote la kumkata Lowassa na hata kabla ya hapo limepangwa then anapewa kupeperusha bendera ya UMOJA WA VYAMA VYA UPINZANI. then jamaa anajitoa na kutambaa zake majuu kama Balali hayo mawe yenu mtampigia wapi na saa ngapi?

Huu walioufanya jamaa ni uzembe wa daraja la kwanza pamoja na rundo la wasomi wenye njaa kali wanaoenda kwa mazoea tu kwamba giza likiingia ni kulala.
 
Ndo maana nikasema hii nchi ni rahisi mno kuudhoofisha upinzani sema hakuna strategic plans za kufanikisha hilo sababu wenye hiyo dhamana ni wavivu wa kufikiri.

Tuseme zengwe lote la kumkata Lowassa na hata kabla ya hapo limepangwa then anapewa kupeperusha bendera ya UMOJA WA VYAMA VYA UPINZANI. then jamaa anajitoa na kutambaa zake majuu kama Balali hayo mawe yenu mtampigia wapi na saa ngapi?

Huu walioufanya jamaa ni uzembe wa daraja la kwanza pamoja na rundo la wasomi wenye njaa kali wanaoenda kwa mazoea tu kwamba giza likiingia ni kulala.

Unawaza kama niwazavyo! Upinzani wanatakiwa wa take note kwa kweli.. Kipindi hiki hawakupaswa kucheza kamari ngumu namna hii! Ngoja tuone..
 
Ahsante Dr slaa nadhani kwa hili watu watakuelewa nn ulikuwa unamaanisha kwa mbaali naona u prof wa UDSM unakujia bila ya tafiti hii ni kutokana na maono yako na kuitendea haki taaluma yako
 
Nilikuwa nikifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu na Mgombea uraisi pia na kauli za Mwenyekiti CCM nilishindwa kujua kama walikuwa wanamaanisha maana sikuona umakini katika swala hili maana walionekana kuchoka kabla ya safari!
Je ni nini kimewapata?maana hata mbwembwe hakuna! Maana akiondoka NEC inaruhusu kuweka mgombea mwingine hapo ndo hapo CCM watakuwa wamebug
 
hatimae c.c.m imesimamisha wagombea wawili wa urais

Kinana amesema, kuna CCM safi, na CCM Makapi.. Wananchi watachagua CCM Safi! Mwaka huu, ushindani mkali kwenye Uchaguzi Mkuu Oktoba ni kati ya CCM dhidi ya CCM..

Kama si kichekesho ni nini?!
 
Wakuu,

Haya ni maoni binafsi na yanaongozwa na hisia za ndani nisizoweza kuzi-control bali kuzishirikisha kwenu nanyi mtazame;

Kutokana na kasi ya Upinzani kushamiri bila kuchoka tangu Mwaka 2005, ambayo ilisababisha CCM kupata mtikisiko mkubwa na kukaribia kuachia madaraka kwenye Uchaguzi mkuu wa 2010, katu haiwezekani wakawa wame-relax na kurudia makosa..

Ninachojaribu kusema, vuguvugu na nguvu ya upinzani katika Bunge la 10, Muungano wa vyama vya Upinzani vyenye nguvu miaka michache baada ya uchaguzi mkuu wa 2010, Uenezi usio na shaka Upinzani kwenye majimbo mengi zaidi nchini na mikakati imara ya kisiasa waliiyonayo Upinzani , CCM haiweze kurelax na kurudia makosa...

Imetengenezwa Sinema, ya kutuaminisha kwamba Mheshimiwa Lowassa, one of the prominent political figures from CCM, is no more 'wanted' in the Party despite nguvu kubwa ya ushawishi aliyonayo ndani na hata nje ya chama.. CCM haitaki tena kurelax na kurudia makosa..

This to me feels like a bail ambayo wapinzani wameshindwa kuing'amua na mpaka sasa wanacheza ngoma ya Chama tawala, ambacho kimekoma kurelax na kurudia makosa..

Hisia zangu zinachagizwa na Matamshi ya katibu wa Uenezi na hata Mwenyekiti wa CCM - Taifa, kwamba CCM itashinda hata kwa 'Goli la Mkono'.

Bahati mbaya, tafsiri ya Goli la mkono mpaka sasa wengi wameiona kama 'wizi wa kura', lakini kwangu ni zaidi ya hivyo; Safari hii naamini inatumika njia ya ku-win trust ya wapinzani kwa mtu wao (pandikizi), kupitia movie iliyotungwa na kuanza kutekelezwa kwa muda mrefu nao CCM - Hili ndio Goli la Mkono haswaaa!

Hisia zangu zisipuuzwe!

Haiwezekani kuwa goli la mkono, EL, katukanwa sana na NAPE pamoja na MAKONDA. Hii ni move ya kweli mdau.
 
Kama kweli vile

Yah ni kweli, CCM wamesimamisha wagombea wawili wa urais..... acha tuendelee kuangalia hii movie tuone mwisho wake oct 25
 
Lowassa kaenda chadema kuwavuruga. Hiyo ni trick ya ccm...lowasa awavuruge weeee washindwe kufanya la maana. Ukawa nao hawajashtuka tu...
 
Haiwezekani kuwa goli la mkono, EL, katukanwa sana na NAPE pamoja na MAKONDA. Hii ni move ya kweli mdau.

Katukanwa lakini hakufikishwa mahakamani. Je, kama ni njia inayotumika kutulisha imani kwao zaidi?

Tuendelee kutafakari mkuu..
 
Katukanwa lakini hakufikishwa mahakamani. Je, kama ni njia inayotumika kutulisha imani kwao zaidi?

Tuendelee kutafakari mkuu..

CCM sio chama cha siasa ni dola kwa wenye akili na uelewa hatujipi presha ya uchaguzi na ukawa.
 
Inawezekana. Lakini uthibitisho ndo mgumu. Hebu tusubiri tuone
 
ndo mnashtuka leo sio low-hasa peke yake hata huyo kamanda mkuu pia ni wa cicemu. wajanja wametulia pembeni tu wanaangalia hii tamthilia inavyoendeshwa
 
Back
Top Bottom