Ngalikihinja
JF-Expert Member
- Sep 1, 2009
- 34,637
- 37,960
Nadhani fanya hivi.....Natumai wazima wote..
Naomben mawazo yenu hasa wanawake mlioko kwenye ndoa
Mi nipo ndoan miez michache tu nimeolewa baada ya miez 2 akaja mtoto wa wifi yangu naishi nae hapa
Sasa Kuna vitabia anavyo ambavyo kweli kibinadamu vinanikwaza ila navumilia sababu najua tumetoka familia tofauti na tumelelewa malezi tofauti......
Vingi napotezea tu sababu najua may be utoto au
Bint Anamika 25 tabia yake kubwa inayonikera nikuingia chumbani kwangu yeye anachumba chake lkn akiwa nashida anaingia tu haijalishi atanikutaje labda navaa wala hajali binafsi naona kitu Cha ajabu sababu tulivyokua chumba Cha baba na mama Cha kuheshim na tulikua tunaingia kwa emergency, nilimuita nikamwambia ukiwa na shida chumbani niambie au bisha hodi lkn haiajsaidia ...
2) tabia ya pil anafanya vitu anavyotaka yeye mfano akitaka kupika haulizi tunapika Nini anapika anavyojisikia na anavyotaka yeye unakuta hela niliyoachiwa ikiisha naulizwa Mimi nashindwa kumwambia mjomba ake napotezea tu.... Kila siku anakuja na marafiki wapya hata anitambulishi Wala siwajui napishanao tu naweza kutana na mtu jikon au chumbani kwake hata cjui Ni Nan serious nakosa Amani nashindwa nifanyeje
Kibaya mjomba wake anaamini huyu bint yuko parfect 100% hata akikosea anaogopa kumwambia so nashindwa nifanyeje
1. Mwambie mumeo hizo tabia. lakini kama huwa anadhani huyo binti ni 100% perfect, tegemeo ubishi, lakini ukizidi, siku apika chochote, mtengee mumeo, au akimaliza, we wala usihangaike kupika, subiri hadi atakaporudi mwambie kuwa vimeisha
2. Unaweza mtafuta mtu unayeelewana naye kwenye familia yao. Mwite aje kwako kama kutembea au kusailimia then mpe taarifa hiyo ili yeye aseme na binti. Akae hapo kwenu siku kadhaa ambazo atazitumia kuchunguza na atakapoona kimojawapo au vyoite vimetokea amkalishe binti huyo na kumweleza. AKibisha yeye ndo amwambie mumeo
3. Jenga tabia ya kufunga chumba chako (kama hufanyi hivyo). Tembea na ufunguo kila unapokwena, VIle vile hakikisha kila unapokuwa chmbani, umejifungia kwa ndani
4. Fanya mpango siku moja binti aingie ndani then amkute mjomba chumbani….
5. HATUA YA MWISHO NI KUMFUKUZA, LAKINI BAADA YA KUJARIBU HAYO YA JUU