Nimrod Mkono: Atumia BILIONI 90 kujenga shule 7

Nimrod Mkono: Atumia BILIONI 90 kujenga shule 7

mkono.JPG



Kwa maana hiyo BILIONI 90 ni kwa ajili ya construction ya shule na kujaza fenicha na kila kitu

sasa watu wa huko kwao wanasema BILIONI 90 NI ESTIMATE ZA CHINI mno

Sina picha za hizo shule lakini kama kweli kaiba na kisha mapesa yenyewe kajenga shule Tanzania na inasemekana kazikabidhi serikali ambayo imeshindwa kuziendesha....mnasemaje wakuu?

sasa kama mapesa yote hayo yametolewa kwa wananchi jiulizeni kiasi gani jamaa kaweka nje ya nchi?

Hivi kweli mtu kama Ndesamburo anaweza kumfikia Mkono kwa investment ya elimu aliyofanya huko Musoma?

mkipata picha zileteni


Ohh I should point out ni PESA ZAKE BINAFSI....na kwa sababu hajawahi kuhukumiwa na chombo chochote cha sheria I assueme ni pesa halali

Mimi sikubaliani na maelezo haya kuhusu kiasi kilichotumika (billioni 90). Haiwezekani hata kudogo. shule hizi ni za kawaida kabisa. sio za gorofa. Ujenzi wa mtu binafsi ni tofauti kabisa na ujenzi wa serikali ambapo bei ya kitu inazidishwa hata mara 3.

Bwana Mkono alijenga kama mtu binafsi, hivyo gharama zake za ujenzi zilikuwa za chini hata kama alitumia contractor. Mimi sio mtaalamu wa ukadiriaji majengo lakini ukweli unabaki kuwa sio fedha nyingi kiasi hicho kilichotumika.

Bado siamini kama kila shule ilitumia bilioni moja. Ndugu zangu kama zile shule zimetumia kiasi hicho cha pesa basi yule bwana anayemiliki St. Mathew iliyoko Kongowe atakuwa trilionea.

nazifahamu shule tatu zinazozungumziwa ni uzushi wa ajabu. naweza kukubali tu kama utasema shule moja imetumia millioni 90. hapo ni pamoja na kuweka vifaa vyote. tazameni majengo hayo kwenye website yake ya http://www.musomarural.org
 
Mkuu hapo kwenye red hilo si jimbo lake, jimbo lake ni musoma vijini ambako kuna wazanaki wengi, ila musoma mjini yupo kamanda Vicent Nyerere kutoka Chadema.
Mkuu nalijua sana hilo. Kulikuwa na makubaliano fulani kati ya CDM na Mkono. Kwamba CDM waachie Musoma Vijijini na yeye awasaidie kule Musoma Mjini ili Vicent amshinde Manyinyi. Kulikuwa na tetesi kuwa Manyinyi na Mkono hawaelewani hivyo ikawa ni kukomoana! Hukumbuki CDM walisema wanaweka pingamizi baada ya ati Mgombea wao kuhongwa; pingamizi liliishia wapi? Hii ndio siasa ya nchi hii. Unaweza kutokwa na mapovu kumbe wenzio wanakutana kwenye mesa ya duara na kumaliza mambo.
 
Robin Hood is welcome in Tanzania. Unfortunately, we only have lawyers with briefcases.
 
Mkono katika hili la maendeleo hasa elimu, nampa pongezi sana.He has done a lot to be remembered.Iwapo alikwiba kweli na sasa anarudisha kwa njia ya kutoa huduma kwa jamii i better give him big up. Rostam asingeshindwa kujenga hizi shule Igunga ila kwa sababu hakuwa Mzalendo kuendelea kuiba kwake ilikuwa motto.
 
Billion 90 shule 7! Au billion 9? Wewe mleta habari unajua thaman halisi ya bn 90 au ndo zile za ccm za kujenga tundu la choo kwa min 700?
 
vijisenti aliweka pesa zake uk one million pound zikiendeleza uchumi wa wazungu wakati wamatumbi wanakoeshwa kwa riba yaaslimia 16 , alichofanya mkono ni uzalendo hata pesa iwe imetoka wapi , iliwasaidia wazalendo , VIJISENTI & CO , MAPESA YAO WAMEIBA NA WANHONGA KWENYE CHAGUZI TUU,
 
Mkuu nalijua sana hilo. Kulikuwa na makubaliano fulani kati ya CDM na Mkono. Kwamba CDM waachie Musoma Vijijini na yeye awasaidie kule Musoma Mjini ili Vicent amshinde Manyinyi. Kulikuwa na tetesi kuwa Manyinyi na Mkono hawaelewani hivyo ikawa ni kukomoana! Hukumbuki CDM walisema wanaweka pingamizi baada ya ati Mgombea wao kuhongwa; pingamizi liliishia wapi? Hii ndio siasa ya nchi hii. Unaweza kutokwa na mapovu kumbe wenzio wanakutana kwenye mesa ya duara na kumaliza mambo.
Kaka pale Musoma mjini ilikuwa Vicent VS Manyinyi au Vicent VS Mathayo, na kwamba Mathayo ilikuwa lazima abwagwe kwa garama yoyote.Sijajua hapo Mkono kwa Mkono aliusika vipi? Hiyo M CDM kupewa bashasha nimeisikia pia.
 
Mbona shule zenyewe ni za kawaida tu? I heard aliwekeza kwenye maabara na vifaa vya ICT. Labda pengine ndo sababu ya kuwa na hela hizo Bil. 90. But all in all, huyu bwana alikuwa wapi enzi za Nyerere maana kulikuwa na kesi analipwa toka miaka ileee....after all, going back to Mario Puzo's Godfather...A lawyer with a briefcase can steal more than a hundred men with guns!


mkuu hiyo bold underlined nimeipenda sana!
 
Shule zilizojengwa na huyu fisadi ukiziona, utazikubali. Majengo yake ni ya kiwango cha hali ya juu na shule zote zimekamilika kwa vifaa vya kufundishia na vitabu.
Pamoja na yote hiyo bei mmetia chumvi sana, 90billion kwa sasa inaweza kujenga 5star hotel mbili fully furnished zenye vyumba visivyopungua 150 kila moja, ukweli ni kwamba shule zimejengwa tena kisasa ila hazijafika hata robo ya hiyo 90bil, wakati moja inafunguliwa japo sikumbuki kwa usahihi ilikuwa kama 2bil pamoja na nyumba za walimu na vifaa vya ict na maabara.
 
Mtoa mada katia chumvi. Bil 90 ni kiasi kikubwa sana na hizo shule ni za kawaida. Kwa wale wanaoifahamu Mabibo Hostel ile hostel ya UDSM, NSSF walisema ilijengwa kwa jumla ya bil. 26 ikiwa ni pamoja na vifaa vyote vya ndani. Block moja nadhani unaweza kujenga shule tatu za Mkono.
 
Kaka pale Musoma mjini ilikuwa Vicent VS Manyinyi au Vicent VS Mathayo, na kwamba Mathayo ilikuwa lazima abwagwe kwa garama yoyote.Sijajua hapo Mkono kwa Mkono aliusika vipi? Hiyo M CDM kupewa bashasha nimeisikia pia.
Mkuu hiyo gharama yoyote sasa ndio Mkono wa Mkono! Siasa bwana tamu kweli. Mathayo Manyinyi alipiga mayowe wee acha tu! Mkono alikorofishana na Mathayo akaamua kumpelekea kijana wa nyerere kumkomesha yule mkurya.
 
hicho kikofia cha tarabushi cha huyo mzee sijui kina siri gani ya urembo .... sijawahi kuona kakivua hata siku moja
 
vijisenti aliweka pesa zake uk one million pound zikiendeleza uchumi wa wazungu wakati wamatumbi wanakoeshwa kwa riba yaaslimia 16 , alichofanya mkono ni uzalendo hata pesa iwe imetoka wapi , iliwasaidia wazalendo , VIJISENTI & CO , MAPESA YAO WAMEIBA NA WANHONGA KWENYE CHAGUZI TUU,
Kama anavyofanya ENL kwa kuanzisha vitegauchumi hapa nchini na vijana kupata ajira! Au hilo hulitaki?
 
Bilioni au Milioni 90? Kama ni shula za kisasa zenye maabar inawezekana. Congrats mzee, unajua kuteka akili za Wakurya.

Nimebahatika kuziona hizo shule, ni nzuri na za kuvutia lkn shule 7 hazifiki hiyo thamani ya bil 90, hiyo ni exegaration!
Na ni mali binafsi za Mkono
 
Mkuu hivi kuna yeyote kweye hii list aliyejenga shule za kiasi hicho au hata kwenye charitable organisation
Isitoshe hizo pesa hata yeye mwenyewe hana
https://www.jamiiforums.com/busines...194654-forbes-releases-african-rich-list.html
Jina lake humu hamna hata ukienda TRA kuna watu kibao wanalipa kodi kumshinda yeye
F*** ck you all mnaosapoti huu ujinga
mkuu umewahi kufika ofisini kwake pale PPF Tower? Inawezekana hiyo pesa iliyotajwa si sahihi lakini mzee ana vijisenti.
 
Kajenga hizo skuli bila kushurutishwa na kwa faida ya wananchi katika jimbo lake bila kuwadai fidia,ninampongeza kwa hilo.Maadamu zinakidhi viwango vya msingi kwa maana ya shule na si mambo ya 5 star hotel.Hakuna haja ya kumkatisha tamaa.
 
kweli Tanzania hatutaendelea vurugu tupu, Golikipa anaenda kufunga magoli striker anaenda kushika kibendera vurugu tupu! Kazi ya Member of Parliament hiyo kujenga shule!!!???? na District Executive Director, Minister of Local Governments na Minister of Education wafanye nini!!!! valu valu!! Bungeni ameenda kufanya nini!!! Ndo mambo kama ya Mrema waziri wa Mambo ya Ndani anakuwa mpaka wa ustawi wa jamii yeye RC yeye, vuluvulu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom