Nimrod Mkono aitisha CCM

Nimrod Mkono aitisha CCM

Kimbunga

Platinum Member
Joined
Oct 4, 2007
Posts
14,952
Reaction score
10,037
Nimesikia kupitia magazeti kwamba Nimrod Mkono (Mbunge wa Musoma Vijijini - CCM), akisema kwamba ameshtushwa na taarifa kupitia vyombo vya habari kwamba jina lake limeenguliwa toka katika watu wanaogombea Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi. Amesema kama kweli jina lake limeenguliwa basi CCM patakuwa hapatoshi.

Hivi CCM niliyokuwa naijua imefikia kiasi cha kutishwa kiasi hicho na wanachama wake? Kweli CCM imekuwa kama kambale: Baba sharubu, mama sharubu na watoto sharubu.

Mkuu Mchambuzi CCM imefikia hatua ya kutishwa na kila mtu. Watishaji wana moral authority kweli ya kuitisha CCM au ndio kusema CCM imekosa watu wenye moral authority ya kukemea?
 
Nimrod Mkono Mbunge wa Musoma Vijijini ametishia chama chake endapo kitamtosa mpaka mwisho kwenye kinyang'anyiro cha Ujumbe wa NEC. Amesema hayo baada ya kutoswa kwenye mchakato wa awali.

Source: Mwananchi

Karibu TLP Fisadi, Chadema huna nafasi
 
Nimrod Mkono Mbunge wa Musoma Vijijini ametishia chama chake endapo kitamtosa mpaka mwisho kwenye kinyang'anyiro cha Ujumbe wa NEC. Amesema hayo baada ya kutoswa kwenye mchakato wa awali.

Maneno ya mkosaji! Ana ubavu gani wa kutishia Magwanda?
 
Ukikubali kula vya watu lazima nawe uliwe...ndio matunda ya CCM kuendeshwa na mafisadi
 
teheteh kwani ana hati miliki nndani ya Magamba? ni lazima na yeye awepo ndo chama kisonge mbele? hakuna fikra mpya huko magamba jamani khaaaaaaaaaa
 
Wameona hana sifa za kugombea ndo maana wamemchuja
 
Labda wamemuengua kwa kuwa alitia sihihi kwenye daftari la zitto kabwe za kumtoa waziri mkuu. ameonekana hawezi kulinda chama. watakuwa wanamuona kama msaliti. mia
 
Penye kufuka moshi ni dalili ya ...........tusubili hiyo ni kama barafu lililochomoza kidogo tu juu ya maji ilhali huko chini ni kubwa balaa limefichwa kwa kufunikwa na maji.

ccm wanahitaji kamanda wa vitendo na mwenye kuchukuwa hatua kukirudisha chama kwenye mstari, vinginevo ni kama barafu kitayeyuka taaratibu na kutoweka.
 
Labda wamemuengua kwa kuwa alitia sihihi kwenye daftari la zitto kabwe za kumtoa waziri mkuu. ameonekana hawezi kulinda chama. watakuwa wanamuona kama msaliti. mia
Kweli inawezakana hili liliwaudhi jamaa zake na sasa wameamua kumtosa! Ila patakuwa hapakiliki huko Magambani maana jamaa anajua masiri yao kibao
 
Labda wamemuengua kwa kuwa alitia sihihi kwenye daftari la zitto kabwe za kumtoa waziri mkuu. ameonekana hawezi kulinda chama. watakuwa wanamuona kama msaliti. mia

Aaaaaa ndio inawezekana. hiyo inaitwa zunguka nikuzunguka.
 
fisadi tu huyo hana cha kuitisha ccm, naye ataingia mitini kama alivyofanya kigwangala.
 
Back
Top Bottom