Nimkubali huyu mwanamke au?

Nimkubali huyu mwanamke au?

KENZY

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2015
Posts
35,772
Reaction score
86,459
Yeye ni mzuri tu anashepu wenyewe wanaita utamu kunoga! Guu nikisema la bia nitakuwa simtendei haki, mtoto anaguu la whisky.

Shingo ndo tusiseme wanaita shingo la mnazi! Kwenye chuchu naomba nisiseme nitanogesha Mambo. Kiuno dondola si dondola nyigu si nyigu labda tu niseme Kama kilamba mwiko. Tuachane na hayo niende kwenye mada.

Weekend iliyoisha huyu kiumbe alinifata akanikuta nimeketi zangu nakunywa juisi kola yangu baridi nawaza nitabidisha vipi hicho kinywaji kiwe balimi! Alivyokuja tukasalimiana baada ya maongezi mawili matatu akatulia tuli then akaanza kuniuliza unakunywa nini?

Nikamwambia ni fanta akabisha. Mara akaomba nikamkatalia yeye alikuwa akisema anasikia harufu ya juisi kola!.. Anyway tuachane na hilo nililimaliza kiinjinia na alielewa si juisi kola japo alikubali kishingo upande.

Shida iliyokuwa imemleta alikuwa amekuja kuniambia kuwa ananipenda! Wala sikushangaa kwani hakuanza siku hiyo alianzaga na barua ila sikumjibu! So anachodai yeye ni kuwa anaona sitaki kumkubali kwakuwa nafikiri kuwa ati atakuwa akiniomba hela! Hili si tatizo bali tatizo kaniambia ati nisijali yeye hataniomba hata mia yangu atajitegemea. Sasa najiuliza huyu bibie anataka kuniweka kwenye mtego au?

Ushauri wenu wakuu isijekuwa ndo naenda kutolewa meno hivi hivi.
 
Hahah jiandae kisaikolojia hapo...Hana mume lakini, usije kupigwa mate ya unyolo ukachezea ukuni!

Kuwa nae makini, anajitegemea kwa shughuli gani anayofanya hapa mjini?
Mkuu hii ni lugha au duh! Ye yupo single kuhusu hilo sina hofu tatizo Hilo tego..
 
mkuu ujue siku zote vya bure vinamadhara, nakutahadharisha tu usijesema wajumbe hawakunambia.
 
Fuata moyo wako unahitaji kipi, maan wee ndo uliyependwa. Uamuzi wowote utakaochukua uta reflect matakwa yako.
Huu ndo ushauri Sasa mkuu popote ulipo kunywa juisi kola ntakuja kulipa..😅
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom