Da Pretty
JF-Expert Member
- Dec 9, 2010
- 3,059
- 1,153
Hongereni kwa kuingia mwaka mpya.
Nina jambo limetokea leo ambalo ni mfululizo wa mambo mengi yaliyokua yakitendeka siku zilizopita.
Ni story ndefu ntajitahidi kuifupisha.
Ninaishi kwenye nyumba ndogo na mdogoangu mwanafunzi na mtoto wa 4yrs ambaye ni mtoto mdogoangu mwingine na msichana wa kusaidia kazi ukizingatia nina huyu mtoto mdogo nami ni mfanyakazi.
Leo nikiwa kazini nimepigiwa simu na tax driver wa pale jirani na kwetu kua msichana wangu ameonekana na begi anaondoka,na ameenda kuchukua tax pale ndio wakawa wanamuhoji maana kuna wanaomfahamu(mara nyingi nikiwa kazini kama kuna kinachotakiwa nyumbani nawaomba hao madereva wanifikishie hivyo humkuta yeye).
Nikawaambia wamzuie,nikamtuma mdogoangu aende akaongee na huyo binti amuulize kwanini alitoroka badala ya kuaga?
Binti akahojiwa,hakutoa jibu lolote,akasachiwa eti kabeba laptop,camera na perfume(nimeshangaa,nilitegemea atabeba nguo na labda simu!) akasemwa pale,akanyang'anywa alivyochukua nikawaambia wamruhusu aende maana nisingeweza kukaa nae tena,akaruhusiwa akaenda.
Sasa jioni hii narudi nyumbani nikapita kwa wale madereva waliyoniambia yamenichosha!!
Wanasema walipomuuliza anaenda wapi akasema kuna dada anafanya kazi salon kwangu,anaishi kinyerezi ndio waliongea kua aondoke atamsubiri tabata asubuhi ile (hajataja tbt ipi) ni kweli nina salon hapa jirani na ninapoishi na kuna mfanyakazi anaishi kinyerezi(naamini hawa madereva hawamfahamu) nae anatafuta housegirl.
Nimeshindwa kuelewa namfanyaje huyu dada wa salon.
Na siku za nyuma nilikua na binti ambae alikuja kwangu akiwa mjamzito nikampokea vizuri,
haohao wafanyakazi wa salon kwangu (wa kinyerezi)wakaanza kumzonga na maneno akawa ananiambia hadi tumbo limekua ndio wakawa wanashangaa eti ana mimba nimuondoe atanitia mzigo(wakati nilijua mapema) binti kaenda kwao kujifungua,huyu kaja tar 30 Dec washamchukua.
Hivi niwafanyeje hawa wafanyakazi wa salon kwangu??
Nina jambo limetokea leo ambalo ni mfululizo wa mambo mengi yaliyokua yakitendeka siku zilizopita.
Ni story ndefu ntajitahidi kuifupisha.
Ninaishi kwenye nyumba ndogo na mdogoangu mwanafunzi na mtoto wa 4yrs ambaye ni mtoto mdogoangu mwingine na msichana wa kusaidia kazi ukizingatia nina huyu mtoto mdogo nami ni mfanyakazi.
Leo nikiwa kazini nimepigiwa simu na tax driver wa pale jirani na kwetu kua msichana wangu ameonekana na begi anaondoka,na ameenda kuchukua tax pale ndio wakawa wanamuhoji maana kuna wanaomfahamu(mara nyingi nikiwa kazini kama kuna kinachotakiwa nyumbani nawaomba hao madereva wanifikishie hivyo humkuta yeye).
Nikawaambia wamzuie,nikamtuma mdogoangu aende akaongee na huyo binti amuulize kwanini alitoroka badala ya kuaga?
Binti akahojiwa,hakutoa jibu lolote,akasachiwa eti kabeba laptop,camera na perfume(nimeshangaa,nilitegemea atabeba nguo na labda simu!) akasemwa pale,akanyang'anywa alivyochukua nikawaambia wamruhusu aende maana nisingeweza kukaa nae tena,akaruhusiwa akaenda.
Sasa jioni hii narudi nyumbani nikapita kwa wale madereva waliyoniambia yamenichosha!!
Wanasema walipomuuliza anaenda wapi akasema kuna dada anafanya kazi salon kwangu,anaishi kinyerezi ndio waliongea kua aondoke atamsubiri tabata asubuhi ile (hajataja tbt ipi) ni kweli nina salon hapa jirani na ninapoishi na kuna mfanyakazi anaishi kinyerezi(naamini hawa madereva hawamfahamu) nae anatafuta housegirl.
Nimeshindwa kuelewa namfanyaje huyu dada wa salon.
Na siku za nyuma nilikua na binti ambae alikuja kwangu akiwa mjamzito nikampokea vizuri,
haohao wafanyakazi wa salon kwangu (wa kinyerezi)wakaanza kumzonga na maneno akawa ananiambia hadi tumbo limekua ndio wakawa wanashangaa eti ana mimba nimuondoe atanitia mzigo(wakati nilijua mapema) binti kaenda kwao kujifungua,huyu kaja tar 30 Dec washamchukua.
Hivi niwafanyeje hawa wafanyakazi wa salon kwangu??