mng'oa kucha
Senior Member
- Jul 31, 2013
- 150
- 179
Nimetoka kibaruani kufanya kazi ngumu nimepewa ujira ambao sina uhakika kama unaendana na kazi niliyofanya, nimeweka kiasi honcho cha pesa kwenye mfuko wa mbele wa suruali (siyo jeans) wakati bado Nina msongo nisijue kiasi hicho cha nitakipangilia vipi akatokea mtu mmoja akaingiza mkono wake mfukoni Mwangu,, niliudaka ule mkono akajaribu kunishambulia nilifanikiwa kumzidi nguvu nilimpiga ngumi ya mdomo nikampasua mdomo wa chini alining'ang'ania huku akipiga makelele kwa lengo la kunikaba koromeo nilichukua jiwe kubwa na kumpiga utosini RIP sikuwa na muda wa kusubiri maana wale jamaa wana maswali wanaweza kukuuliza kwa nini hukumleta kituoni (angali mtu amekukaba koo)