Nimetapeliwa na aliyekuwa mpenzi wangu

Soma maelezo yake vizuri hii n stor katunga tu .lengo ANAHITAJI msaada Ivo kailjificha kwenye kivuli Cha utapeli
Kama ni tapeli basi anazingua na watu wa hivi ndio wanasababisha wenye shida kweli wasisaidiwe
 
Ukihitaji mganga wa kumfanyia namna gani huyo tapeli wako, nishtue niko tayari muda wowote

NB:police kesi za mwanamke kwenda kumshtaki mwanaume kwamba amekutapeli au kukuibia bila kuwa na vivid examples na reference Hakuna kesi hapo na vibao unapigwa
 
Post zangu almost zote nimepost on behalf.Vijana wengi baada ya kufanya kazi zangu huhitaji kuendelea kufanya kazi,nami nina limit ya vijana/staff that's why nakuja kuwatangazia huku JF na kwingineko.
Mm nimeacha kuajiriwa zaidi ya miaka 7 iliyopita.
Kwenye ajira zangu zote zilizopita nilikuwa kwenye senior position.
Sasa hivi ni Owner wa some projects.
Karibu PM kama hutajali..!
Aku sitafuti kamseleleko.

kamselele. 😂😂🙊🙊
 
Pole sana, unaonaje ukirudi nyumbani kwa mama hadi biashara yako ikisimama tena.
Maana utasaidiwa kodi ya mwezi mmoja, na miezi inayofata itakuaje
Natamn kumwambia mama ukweli ila naogopa maana hiyo hela ya mtaji aliuza mbuzi alizokuwa amefugia kwa mjomba. Sasa nikimwambia sina chochote sijui itakuwaje. Ila wazo la kuuza vitu vyangu vyote ndilo lililobaki ili nianze upya basi. Asante kwa ushauri
 
Habari ya saizi waungwana?? Naamini mu wazima wa afya kabisa. Bila kupoteza muda niingie kwenye maada.

Kwanza kabisa. Mimi ni binti wa miaka 28, sijaolewa bado na mahusiano yangu yamevunjika wiki tatu zimepita na ndicho chanzo cha mkasa wangu.

Hapo nyuma wakati nipo home mama alinipa sh lak tatu nifanye biashara maana aliamini nina mkono wa biashara na kiukweli nilipoaanza kuuza sendo za kimasai zile niliuza kwa mafanikio makubwa. Tuachane na hilo.

Wakati nafanya biashara nilikutana na boyfriend ambaye tulijikuta tunapendana kweli kweli. Huyu bwana alikuwa muuza urembo. Tumedumu nae kwa muda wa miaka mitatu. Alikuwa na wivu mno hadi alivunja laini zangu na kunisajiria mbili kwa majina yake yeye.

Mwaka jana aliniambia tununue uwanja tujenge nikaona wazo zuri, akaniambia bei ya uwanja akapendekeza tuchangiane, kweli nilichangia kiasi fulani hivi tukapata uwanja. Mwaka huo huo akasema tujenge msingi, tukajenga. Na mwaka huu tulikuwa tunamalizia kuijenga.

Mimi kulingana na mtaji wangu na hela niliyotumia kujengea nyumba nikaishiwa kabisa na yeye akaniahidi kunipa mtaji mwingine tena maana alitaka tuchukue mkopo benki kwa dhamana ya nyumba mimi nikagoma kabisa.

Basi majukumu yangu yote akayavaa yeye kuanza kunilisha, kodi ya nyumba na vingine vingi maana mimi niliishiwa hela. Shida imekuja baada ya kodi kuniishia mimi nikamwomba awekee milango nyumba yetu ili mimi nihamie akasema kwa sasa hana hela, nikamwomba basi anilipie kodi sh elfu 75 tena akaanza kalenda.

Nilivyombana sanaa akawa mkali ndipo akafunguka sasa. Kumbe ile nyumba na uwanja si vyetu tena, alikuwa anamsaidia rafiki yake mwanajeshi, kwa hiyo yeye alikuwa msimamizi tu. Hela nilizokuwa natoa mimi sijui alichozifanyia na alivyoona nimekuwa mkali akakimbia na kwenda huko kusikojulikana.

Kwa hiyo nimetapeliwa na huyu bwana kwa namna hiyo. Sasa saizi mwenye nyumba kanibana ananipa vitisho vya kunitimua nami hapa sijabaki na hela. Nimesharipoti polisi kuhusu kutapeliwa na bado anatafutwa kubaini aliko.

Mwisho, naombeni msaada wa hali na mali jamani niweze kulipa kodi ya chumba sh 75,000. Na pili naomba ushauri wenu nifanyaje zaidi ili niweze kurudishiwa hela nilizotaperiwa na je siwezi kusimamisha ile nyumba kuguswa na mtu hadi kibari cha mahakama kitoke kwa maridhiano?

Naomba kuwasilisha.
Tangu ujiinge JF of GT's una miezi mitano tu unaanza kubomu. Nenda kakae kwa mama yako bado yupo na chumba chako kipo.
 
Asante kwa USHAURI wenu. Kuna kitu nimejifunza, sijawajibu maswali yenu mlio wengi but yamejubiwa na members wengine humu humu ndani. Kuna walionidhihaki na wengine wameniita taperi na mimi. Hainiumizi akili kwa maana palipo na wengi pana mengi.

Lakini pia jana ile nilibahatika kupata namba ya huyo mjeshi nikamwambia A-Z yaliyonikuta. Na yeye ameniambia baadhi ambayo sikuwa nayajua ikiwemo kutaperiwa na yeye na huyohuyo bwana, almalfu kwa jina la ABEIDNYO. Ila jina lake kamili ni Abeid. Mjeshi huyo kasema aliambiwa nyumba itakula tofali elf 11 lakini kiuhalisia ata elfu nane hazifiki, mbao hivohivo na mabati pia. Yan alikuwa anaongeza idadi. Ila kaniahidi kesho kunisaidia kodi ya miezi miwili wakati tukiendelea na uchinguzi aliko huyo bwana.

Nashukuruni sanaaa. Sijapokea hela yoyote toka kwa mtu yeyote humu jf na nasikitika kusema walioniomba namba wameishia kunitongoza tu bila msaada wowote. Narudia tena mimi siyo taperi. Kama kuna mtu nimemjibu vibaya basi anisamehe tu.

ASANTENI SANAAA
 
Asante kwa USHAURI wenu. Kuna kitu nimejifunza, sijawajibu maswali yenu mlio wengi but yamejubiwa na members wengine humu humu ndani. Kuna walionidhihaki na wengine wameniita taperi na mimi. Hainiumizi akili kwa maana palipo na wengi pana mengi.

Lakini pia jana ile nilibahatika kupata namba ya huyo mjeshi nikamwambia A-Z yaliyonikuta. Na yeye ameniambia baadhi ambayo sikuwa nayajua ikiwemo kutaperiwa na yeye na huyohuyo bwana, almalfu kwa jina la ABEIDNYO. Ila jina lake kamili ni Abeid. Mjeshi huyo kasema aliambiwa nyumba itakula tofali elf 11 lakini kiuhalisia ata elfu nane hazifiki, mbao hivohivo na mabati pia. Yan alikuwa anaongeza idadi. Ila kaniahidi kesho kunisaidia kodi ya miezi miwili wakati tukiendelea na uchinguzi aliko huyo bwana.

Nashukuruni sanaaa. Sijapokea hela yoyote toka kwa mtu yeyote humu jf na nasikitika kusema walioniomba namba wameishia kunitongoza tu bila msaada wowote. Narudia tena mimi siyo taperi. Kama kuna mtu nimemjibu vibaya basi anisamehe tu.

ASANTENI SANAAA
naelewa vzr hali unayopitia pole sana
 
Back
Top Bottom