bobby dolat
Senior Member
- May 18, 2015
- 167
- 263
Nimedhamiria mkuuha ha nimependa bandiko lako
Yap michango ya harusi inaumiza sanaNakuunga mkono mkuu
Hata mm nilishtuka siku nyingi sana shida ikawa ni implementation, maana koo zingine zina lawama sana, hivyo nikawa nashindwa ila sasa nimeazimia moja kwa mojaPOLE MKUU..WENZIO TULISHASTUKIA HIYO KITU KITAMBO SANA...NACHANGIA HARUSI 3 TU KWA MWAKA NAZO NI KIWANGO CHA TSH LAKI MOJAMOJA...NA HIZI ZINGINE HUWA HATA AHADI SITOI NAWAAMBIA NITATOA NITACHOPATA ILA SITOI PLEDGE NGOOO.
Hata mm nilishtuka siku nyingi sana shida ikawa ni implementation, maana koo zingine zina lawama sana, hivyo nikawa nashindwa ila sasa nimeazimia moja kwa moja
Kweli kabisa, kati ya harusi 10 ulizochangia ndani ya miaka 2-3 Unakuta sita kati ya hizo harusi kumi zimesambaratikaJamani hii michango ishakua dhiki sasa,unachangia harusi na wanandoa hawakai na wenzao mara wameachana,mbali na hilo kuharibiana bajeti ndio mbaya zaidi..
Hapana ndugu yangu harusi zimekua nyingi mno, hivi Kuna maana yeyote mambo mengine kwenye maisha yakwame kisa harusi?Tusiache kufadhiri wengine kwenye jambo hili la kheri na la kishujaa. Mleta mada pole sana ila usiache fanya unapokuwa na nafasi ya kufanya na Mungu atakubariki. Ujue hatukuja na kitu duniani na Mungu ndiye mpaji atuapaye riziki hivyo kugomea jambo la baraka kama hili ni kumkufuru muumba kama hutotoa kwenye harusi utatoa kwingine ambako hutopata baraka na hutothubutu kuja kutuambia hapa. Tufadhilini wanaooa na kuolewa hasa tunapopata nafasi.
Mkuu umeoa?. Wewe ulichangiwa ama hukuchangiwa?. Na waliokuchangia unajua ni wangapi walijinyima hata hiyo 5000 haikuwa pesa kwa wakati huo?. Kikubwa ukipata nafasi na amani ya rohoni toa hata mimi siko vizuri sana ila ikitokea kuna ninazochanga na nyingine nashindwa ila sitokuja kutoa kauli ya kugoma kutoa kisa majukumu. Majukumu yakizidi sitoi ama natoa kiasi.Hapana ndugu yangu harusi zimekua nyingi mno, hivi Kuna maana yeyote mambo mengine kwenye maisha yakwame kisa harusi?
Kuhusu suala la nafasi, kadri miaka inavyosonga mbele ndivyo majukumu yanaongezeka, hivyo nafasi haitakaa ipatikane maana kila pesa ina kazi
Kwani kuna sehem Mungu alisema harusi ziwe za gharama, pombe nyingi, hotel kali, sijui sare, honey moon mwende visiwani, maharusi wanataka zawad ya kiwanja tena siku hizi wengine wanasema hata msafara wa magari ni aina fulani tu kama ni Benz basi hakuna aina tofauti na benzi. Kwanini ndoa zisifungwe bila gharama au gharama ibebwe na mhusika mwenyewe?Tusiache kufadhiri wengine kwenye jambo hili la kheri na la kishujaa. Mleta mada pole sana ila usiache fanya unapokuwa na nafasi ya kufanya na Mungu atakubariki. Ujue hatukuja na kitu duniani na Mungu ndiye mpaji atuapaye riziki hivyo kugomea jambo la baraka kama hili ni kumkufuru muumba kama hutotoa kwenye harusi utatoa kwingine ambako hutopata baraka na hutothubutu kuja kutuambia hapa. Tufadhilini wanaooa na kuolewa hasa tunapopata nafasi.
Hakuna justification ya suala hiliMkuu umeoa?. Wewe ulichangiwa ama hukuchangiwa?. Na waliokuchangia unajua ni wangapi walijinyima hata hiyo 5000 haikuwa pesa kwa wakati huo?. Kikubwa ukipata nafasi na amani ya rohoni toa hata mimi siko vizuri sana ila ikitokea kuna ninazochanga na nyingine nashindwa ila sitokuja kutoa kauli ya kugoma kutoa kisa majukumu. Majukumu yakizidi sitoi ama natoa kiasi.
Hongera sana ingawa umechelewa sana kufanya uamuzi huo maana ndio hasa msingi wa maendeleo ya binadamu.Habari wadau
Katikati na mwishoni mwa miaka ya tisini tulikua tukichangia harusi 5000 unapata single card na 10,000 unapewa bibi na bwana
Mwanzoni mwa miaka ya 2000 hadi Katikati mwa 2000 tulikua tukichangia harusi 20,000 single na double 30-40 k
Michango ya harusi ikaenda inapanda hivyo hivyo, hadi 2010 ilikua 50-70 single na double ni kuanzia 100 k
Hivi navyoandika 2016 harusi ya jamaa yangu iliyoisha nimechangia 200k, hivyo tunaweza kusema sasa harusi nyingi Michango ni kuanzia 150-200 k na kuendelea
Kwa Hali hii naweza kusema Bila kupepesa macho Michango ya harusi za kileo imechangia kunirudisha nyuma maendeleo yangu binafsi kwa kiasi kikubwa
Mwezi Feb nilichangia harusi 4, each 100,000=
Mwezi huu wa Tatu nimechangia 2 tayari zote zinafanyika wiki hii, moja Thursday na nyingine siku ya pasaka wanabariki ndoa, zile ndoa nyingi zinazofungwa kwa pamoja
Kama mjuavyo koo zetu za wachaga ni kubwa mno, kama ukoo wetu roughly tunaweza kufikia watu 400 tuliopo dar, sasa kwa hali hii unaweza kukuta kila miezi 3 Kuna harusi kwenye ukoo huu, bado harusi za kazini, mtaani na alumni society, nimejaribu kupiga hesabu ya harusi nilizoandika kwenye diary tangu 2006 hadi sasa, jumla kuu niliyopata ningekua na nyumba zingine mbili ambazo ningekua nachukua kodi mbali na hii ninayoishi na familia yangu au ningekua hata na dala dala mbili zinazoleta hesabu
Au, ningeamua kufungua akaunti ya ada za watoto basi watoto wangu wangesoma miaka mingi sana Bila mm kuwazia ada, tofauti na sasa ikifika January ya kila mwaka kichwa kinauma
Naweka azimio, baada ya pasaka sichangii tena harusi, Bahati nzuri watu wangu wa karibu wote yaani tumbo letu tumeshamaliza suala hili , watoto wangu bado ni wadogo wapo primary school, hadi waje wafikie hatua ya harusi sio leo sichangii harusi iwe ndani au nje ya ukoo, sitawatamkia maneno haya bali nitakua nawazungusha tu hadi harusi inapita
Mungu nisaidie niweze kutimiza azimio hili kikamilifu, isiwe kama mara ya mwisho nilipoazimia nikashindwa
Amen