Nimesikitishwa na Watanzania!


Let's be realistic here! Watz tunapenda ku-overstate mambo! Na kama Reverend Masa alivyosema, MAMBO YA MAENDELEO hayapewi umuhimu kama misiba na sherehe (au Usimba na Uyanga). Ita watu uwaombe wakuchangie ukasome uone kitakachokutokea!

Guys, nchi yetu si maarufu duniani kama tunavyoaminishwa, marehemu Kanumba mchango wake ni mostly 99.9% local! Najua kuna elements za foreign recognition, lakini sidhani ina-justify ku-discredit maoni ya Rev Masa.
 
in the office watching clouds tv. Or if your office is media regulatory authority!!!

mimi nimekwama kuingia mjini sababu njia hazipitiki.....kuuliza naambiwa msiba wa kanumba.......kwa nini hakuzikwa jana kuondoa adha kwa wengine?
 
Mimi napenda tu kuwaambia magamba kuwa upendo kwa serikali yao hauji kwa kudandia misiba isiyowahusu ila ni kwa kutatua matatizo ya watanzania. nimeshangaa sana watu niliwaona kwenye msiba huu wakati naangalia TV ya magamba Clouds TV. Nape, Mukama, Tibaijuka, Membe, Bilal, Mama Salma, Mwenda, na wengine magamba wengi tu. yaaini wameteka msiba wa vijana wasanii na kuufanya wao. wanaongea wao tu na wanaonekana wao tu hii ni hatari sana sijui kwenye ofisi zao yupo nani. Just imagine eti Mkama na Nape wanaenda kutoa speech kwa mantiki ipi kama si cheap politics? Tuamke watanzanjia tusitetee tu vitu vya ajabu ajabu ni kweli upendo katika misiba na kufarijiana ni utamaduni wetu sisi watanzania lakini kwa haya niliyaona leo sidhani kama ni upendo tu bali kuna watu kutaka kuchukua umaaurufu kwa kigezo cha msiba huu. Tuwaachie vijana msiba wao wamzike mpendwa wao bwana na wao leo ni wakati wao wa kuuza sura na sio kila seheme tuuze sura sisi tu HAPANA
 

Mchungaji naona kama umekurupuka hivi............
Hivi wewe huudhurii misiba ya watu wakati wakazi?
 
90% ya waliopo hapo hawana kazi rasmi wanaishi mjini kiusanii tu kwa hiyo kwa siku ya leo hiyo ndio kazi yao. Kweli Laigwanan alivyosema kuwa tatizo la ajira ni bomu linalongoja kuripuka nimeamini leo. Hivi unaaga vipi ofisini kwako kwenda kwenye msiba wa Kanumba? Unachukua likizo ya siku moja au? Laigwanan for CCM chairman, but, not for president
 
Mchungaji naona kama umekurupuka hivi............
Hivi wewe huudhurii misiba ya watu wakati wakazi?

Rudia kusoma nilichoandika and come back ! Don't be insane tusufate Mkumbo watz tuheshimu kazi Mch siwezi kwenda msiba wa kisanii Kama huu
 
Kilichoniudhi mimi ni kumnyima baba yake haki kumzika mwanae, haki ambayo inalingana na ile ya kumzaa. Kisa watu watafune michango yote ya msiba kisha wazazi wabaki watupu. Usanii ni balaa kama ilivyo SIASA nchi hii!
 

Ur mentally sick buddy! Point yako I wapi? Msome Mh Kigogo hapo juu

Tatizo ni hapo kwenye red you are also participating through TV!!! anyway ngoja niwajibike nitarui jioni hapa
 
Rev huwa sikubaliani na wewe kivile lakini leo umesema kweli mama yangu ni mzee amesema hebu wamzike mtoto wa watu apumzike tuendelee na kazi nyingine kweli watu wameyakuza sana.
 
hii ni kali kwani hata vipindi vya Radio mbalimbali vimekuwa adjusted kwa hii kitu. Sijui akifa na msanii mwingine ghafla itakuwaje?

Tushapoteza wasanii wengine but haikuwa hivi. Nadhani kila mmoja sinema ya maisha yake inaonekana ktk tukio kama hili wether aliishi vyema au si vyema
 
mimi nahisi mpaka ndugu zake hawakuwa na privacy ya kumlilia ndugu yao.kila kitu kimetekwa.lakini watanzania na sisi mmh,wangapi hizo kazi hawafanyi ofisini kutwa wapo mitandaoni tu
 


Rais Kikwete akiongea na wanakamati ya msiba wa marehemu.
 

Mchango wa movie za mapenz na uchawi?
ama kweli watanzania ni tanzia!
 
Rudia kusoma nilichoandika and come back ! Don't be insane tusufate Mkumbo watz tuheshimu kazi Mch siwezi kwenda msiba wa kisanii Kama huu
Mkuu nimekuuliza tu wewe huendi kwenye misiba wakati wa kazi?
Kama huendi then huwezi kuona sababu ya wanaokwenda huko, hapo sina matatizo na wewe.

Lakini kama unakwendaga basi ujue na wao wametumia grounds hizo hizo
Sasa kama misiba unayokwenda mnaendaga kuzika mkiwa watu kumi hiyo usilaumu msiba wa Kanumba maana inategemea na influence ya Marehemu

BTW, kama upo likzo its ok..........lakini kama unaheshimu kazi kama unavyotaka waTz tuheshimu then hukustahili hata kuja JF kupost msiba wa kanumba badala ya kufanya kazi
Kunya anye bata akinya kuku kaharisha....................hii ni Tz zaidi uijuavyo
 
Tushapoteza wasanii wengine but haikuwa hivi. Nadhani kila mmoja sinema ya maisha yake inaonekana ktk tukio kama hili wether aliishi vyema au si vyema
Akina Mzee Jongo, Mzee Kipara, Tx Moshi William,... Kadhia hii imechangiwa na "brain-washing" inayofanywa na media zetu zikiongozwa na Clouds.
 
Utakuwa umelogwa wewe AMA unapepo! I'm talking from economic point of view! Ujinga Huu watz hao walio leaders hajafanya kazi yeyote ya kuzalisha

Rev hii nchi bwana ukikomaa sana kutafakari unaweza kudata, kuanzia mkuu wa nchi mpaka wananchi sehemu kubwa hawana mipangilio maalumu ya mambo yao hebu fikiria msiba wa Kanumba mtu unafunga ofisi ukashiriki, na haionekani kwamba ni ajabu kwa sababu hata kiongozi wa nchi naye anahisi hii ni ishu ya yeye kuhudhulia kama muwakilishi wa serikali, sijui akina Nchimbi wafanye nini sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…