Deodat
JF-Expert Member
- Sep 18, 2008
- 1,274
- 272
Mimi niko hapa ughaibuni (nchi kapuni - for security reasons), kama wengi mnavyojua mara nyingi ukiwa huku nje ndugu, jamaa na marafiki kule nyumbani bongo huwa wanaomba kila siku ‘uwavute' nao waje huku (bila kujali si rahisi kihivyo). Mwaka jana rafiki yangu kipenzi (tumesoma pamoja tangu shule ya msingi mpaka chuo kikuu pale mlimani) aliniomba nimsaidie kumfanyia mpango mkewe aje hapa kufanya masters degree, nilijitahidi kwa nguvu zangu zote hata kuingia gharama nyingi na hatimaye shemeji yangu kipenzi akafika hapa.
Hapa tulipo sio mji mkubwa sana, una watu elfu 25 tu na watanzania tuko wachache sana na tunafahamiana kwa kiasi kikubwa. Mara nyingi huwa tunakutana na kupiga soga, kunywa na kula pamoja huku tukikumbushana haya na yale hasa kuhusu nyumbani. Hatuna chama rasmi cha watanzania lakini tunashirikiana vizuri sana na tumekubaliana hatutaanzisha chama kwakuwa mara nyingi mkishakuwa na vyama ndio majungu na ufisadi vinaanza na pia tumekubaliana hatutafungua tawi la nje la chama cha siasa (hasa CCM) labda Chadema tutafikiria.
Stori iko hivi: Katika sisi watanzania tulio hapa kuna jamaa mmoja yeye ni mkongwe hapa, ameeishi kwa miaka saba sasa, ameajiriwa na kitengo kimoja cha serikali kama Strategic Analyst (ana pesa nzuri tu) na ni mtu mkarimu sana kiasi kila mtanzania anayefika hapa huwa anamu-appreciate sana jamaa. Huyu jamaa hana mke, sasa shemeji yangu alipofika nilimtambulisha kwa watanzania wengine akiwepo huyu jamaa, wakazoeana sana, siku za mwanzo nilijua ni kawaida tu lakini baadae niligundua wameanza mahusiano, na kwa hivi sasa napoongea shemeji keshahama hostel anaishi kwa jamaa, wanapika na kupakua.
Hicho kitu kimeniumiza sana hasa ukifikiria ni mke wa rafiki yangu. Kwasababu alijua anachokifanya, shemeji sasa ananionea aibu sana kiasi kwamba hata nikimpigia simu hapokei. Wakati naendelea kutafakari nini cha kufanya, nikapokea simu kutoka kwa huyo rafiki yangu (mwenye mke) akinituhumu kuwa mkewe kampigia simu kuwa mimi nimemtongoza na nataka niwe na mahusiano naye kimapenzi, kwakuwa jamaa anamuamini sana mkewe na anampenda mno, amefedheheshwa sana na taarifa hizo hasa ukizingatia sisi ni marafiki wa siku nyingi, jamaa ameapa ‘kunichinja' siku tukionana. Nimejaribu kumuelewesha jamaa haelewi.
Wandugu nifanyeje?
(Samahani sana kwa kuweka stori ndeeeefu lakini ilibidi nifanye hivi ili issue iwe clear kidogo)
Hapa tulipo sio mji mkubwa sana, una watu elfu 25 tu na watanzania tuko wachache sana na tunafahamiana kwa kiasi kikubwa. Mara nyingi huwa tunakutana na kupiga soga, kunywa na kula pamoja huku tukikumbushana haya na yale hasa kuhusu nyumbani. Hatuna chama rasmi cha watanzania lakini tunashirikiana vizuri sana na tumekubaliana hatutaanzisha chama kwakuwa mara nyingi mkishakuwa na vyama ndio majungu na ufisadi vinaanza na pia tumekubaliana hatutafungua tawi la nje la chama cha siasa (hasa CCM) labda Chadema tutafikiria.
Stori iko hivi: Katika sisi watanzania tulio hapa kuna jamaa mmoja yeye ni mkongwe hapa, ameeishi kwa miaka saba sasa, ameajiriwa na kitengo kimoja cha serikali kama Strategic Analyst (ana pesa nzuri tu) na ni mtu mkarimu sana kiasi kila mtanzania anayefika hapa huwa anamu-appreciate sana jamaa. Huyu jamaa hana mke, sasa shemeji yangu alipofika nilimtambulisha kwa watanzania wengine akiwepo huyu jamaa, wakazoeana sana, siku za mwanzo nilijua ni kawaida tu lakini baadae niligundua wameanza mahusiano, na kwa hivi sasa napoongea shemeji keshahama hostel anaishi kwa jamaa, wanapika na kupakua.
Hicho kitu kimeniumiza sana hasa ukifikiria ni mke wa rafiki yangu. Kwasababu alijua anachokifanya, shemeji sasa ananionea aibu sana kiasi kwamba hata nikimpigia simu hapokei. Wakati naendelea kutafakari nini cha kufanya, nikapokea simu kutoka kwa huyo rafiki yangu (mwenye mke) akinituhumu kuwa mkewe kampigia simu kuwa mimi nimemtongoza na nataka niwe na mahusiano naye kimapenzi, kwakuwa jamaa anamuamini sana mkewe na anampenda mno, amefedheheshwa sana na taarifa hizo hasa ukizingatia sisi ni marafiki wa siku nyingi, jamaa ameapa ‘kunichinja' siku tukionana. Nimejaribu kumuelewesha jamaa haelewi.
Wandugu nifanyeje?
(Samahani sana kwa kuweka stori ndeeeefu lakini ilibidi nifanye hivi ili issue iwe clear kidogo)