bampami
JF-Expert Member
- Nov 5, 2011
- 5,697
- 4,107
Wakuu ushauri naomba,
Hapa ninapokaa tupo kama watu 12 hivi, sasa nina jirani yangu (Mke na Mme na watoto wawili) wamehamia siku si nyingi. Sasa tuliwakaribisha vizuri nami ninaishi mwenyewe familia iko mbali.
Leo nimerudi, wakati nasalimia nikasikia "samahani jirani, Nguo ulizoanika kwenye kamba zilianguka zikalowana na matope, nimekufulia zote". Katika hizo kuna boxer zangu nne, Taulo mbili na Underwear moja Eti nazo alizifua. Dah...nimeshtuka lakini nikabaki kumshukuru sana...
Mlangoni niliacha rubber zangu asubuhi huwa nafanya jogging kidogo kujiimarisha kiafya. Nimekuta nazo zimeoshwa zinang'aa kweli kuzidi mke wangu anavyooshaga. Yaani nimepata mshtuko sana kiasi nikashindwa kabisa namna ya kushukuru kwa kujishtukia. Nimeingia ndani bado natafakari hili lilotokea ni jambo zuri lakini limepitiliza mno.
Nimepigwa butwaa hata sielewi inakuwaje hii,kutoka nje sasa hivi naogopa najishtukia sana.
Hapa wapendwa nifanyeje maana hili tukio kwangu si la kawaida kufuliwa hadi nguo za ndani na kuoshewa viatu kwangu si la kawaida. Naogopa Mme wake akijua hilo si litaleta sintofahamu wakati mimi kabisa na mawazo yafananayo na urafiki na huyo mke wa mtu??!!!
Je, Ni UPENDO wa kijirani ama ninini?
Je,Mumewe akisikia itakuwaje jamani wooooooohiii Mungu wangu nyieee....Ntaweka wapi sura yangu ikatokea nimehukumiwa kosa ambalo hata mpango wa kulifanya sipo nao????
Msaada wakuu
Hapa ninapokaa tupo kama watu 12 hivi, sasa nina jirani yangu (Mke na Mme na watoto wawili) wamehamia siku si nyingi. Sasa tuliwakaribisha vizuri nami ninaishi mwenyewe familia iko mbali.
Leo nimerudi, wakati nasalimia nikasikia "samahani jirani, Nguo ulizoanika kwenye kamba zilianguka zikalowana na matope, nimekufulia zote". Katika hizo kuna boxer zangu nne, Taulo mbili na Underwear moja Eti nazo alizifua. Dah...nimeshtuka lakini nikabaki kumshukuru sana...
Mlangoni niliacha rubber zangu asubuhi huwa nafanya jogging kidogo kujiimarisha kiafya. Nimekuta nazo zimeoshwa zinang'aa kweli kuzidi mke wangu anavyooshaga. Yaani nimepata mshtuko sana kiasi nikashindwa kabisa namna ya kushukuru kwa kujishtukia. Nimeingia ndani bado natafakari hili lilotokea ni jambo zuri lakini limepitiliza mno.
Nimepigwa butwaa hata sielewi inakuwaje hii,kutoka nje sasa hivi naogopa najishtukia sana.
Hapa wapendwa nifanyeje maana hili tukio kwangu si la kawaida kufuliwa hadi nguo za ndani na kuoshewa viatu kwangu si la kawaida. Naogopa Mme wake akijua hilo si litaleta sintofahamu wakati mimi kabisa na mawazo yafananayo na urafiki na huyo mke wa mtu??!!!
Je, Ni UPENDO wa kijirani ama ninini?
Je,Mumewe akisikia itakuwaje jamani wooooooohiii Mungu wangu nyieee....Ntaweka wapi sura yangu ikatokea nimehukumiwa kosa ambalo hata mpango wa kulifanya sipo nao????
Msaada wakuu