Baada ya kukaa mda mrefu bila kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi,nimejikuta naangukia penzi la kaka mmoja tuliyefahamiana miaka mitatu iliyopita, huyu kaka aliniambia kwamba ananipenda toka mwanzo tuliponana, nikampotezea ,hakukata tamaa amekuwa akinisumbua sana kwa simu, sms, email mpka nilipoamua kumkubalia mwishoni mwa mwezi wa pili. Toka tulivyokubaliana kuanzisha urafiki, mawasiliano akawa hataki i tena, yaani atapiga simu siku anayotaka kuonana na mimi tu, hilo lilinikera sna nikaamua kuwa nampigia mimi,mesage nikituma hajibu, baada ya week mbili kupita nikiwa nikipiga simu hapokei kabisa nikamtumia mesage ya kumbembeleza sana kwa nini hapokei simu akasema kwamba mda mwingi huwa anakuwa hana simu, anaweza kuwa ameichana kwenye gari,au kaisahau nyumbani,
Baada ya kuniambia hivyo nikaamua kuwa nampigia na line nyingine tofauti cha ajabu akawa anapokea mda wowote ntakao piga, sema nikawa siongei nakata simu,
nikagundua kuwa hataki tu kupokea simu zangu, kitu kingine nilichofanya nikajoin facebook kwa username nyingine, nikamtumia request na message kwamba nimependa relationship status yake kwani aliandika yupo single na ningependa kuwa girlfriend wake. Lol jinsi alivyorepond sikutarajia kwanza alikubali kuwa mi ntakuwa mpenzi wake na mungu akijaalia ntakuwa mke wake, tulivyokuwa tunaendelea kuchat nikamuuliza una mchumba ama girlfriend akasema yeye yupo single na nisiwe na shaka kabisa, akaniomba number ya simu ili anitafute akitoka kazini, nikapiga chenga chenga sikumpa number siku ya kwanza, siku ya pili nikakuta message nyingi sana zikinisihi nimpe number ya simu kwani ana hamu sana ya kuongea na mimi, ndipo nilipoamua kumwandikia number yangu,sasa tangu nimempa number yangu hajatuma ujumbe tena facebook na mimi sijawasiliana nae week ya pili hii.
Wanajamii hivi huyu kijana ananipenda au nichape lapa tu kabla sijainvest mapenzi mazito kwake, kuumizwa na mapenzi tena sipo tayari
Baada ya kuniambia hivyo nikaamua kuwa nampigia na line nyingine tofauti cha ajabu akawa anapokea mda wowote ntakao piga, sema nikawa siongei nakata simu,
nikagundua kuwa hataki tu kupokea simu zangu, kitu kingine nilichofanya nikajoin facebook kwa username nyingine, nikamtumia request na message kwamba nimependa relationship status yake kwani aliandika yupo single na ningependa kuwa girlfriend wake. Lol jinsi alivyorepond sikutarajia kwanza alikubali kuwa mi ntakuwa mpenzi wake na mungu akijaalia ntakuwa mke wake, tulivyokuwa tunaendelea kuchat nikamuuliza una mchumba ama girlfriend akasema yeye yupo single na nisiwe na shaka kabisa, akaniomba number ya simu ili anitafute akitoka kazini, nikapiga chenga chenga sikumpa number siku ya kwanza, siku ya pili nikakuta message nyingi sana zikinisihi nimpe number ya simu kwani ana hamu sana ya kuongea na mimi, ndipo nilipoamua kumwandikia number yangu,sasa tangu nimempa number yangu hajatuma ujumbe tena facebook na mimi sijawasiliana nae week ya pili hii.
Wanajamii hivi huyu kijana ananipenda au nichape lapa tu kabla sijainvest mapenzi mazito kwake, kuumizwa na mapenzi tena sipo tayari