Nimepoteza Pete ya ndoa, ushauri wa haraka

Nimepoteza Pete ya ndoa, ushauri wa haraka

Habari za humu wanajamiiForums,

Tangu saa 10 jioni nikiwa njiani kuelekea nyumbani kutoka kazini baada ya kumaliza kazi za leo, nimejikuta ghafla sina pete ya ndoa na katika kumbukumbu zangu nikakumbuka kuwa niliivua nikiwa ofisini nikageuza gari kurudi kazini kwa ajili ya kwenda kuichukua.

Nimefika ofisini nimetafuta pete mpaka muda huu saa 2 usiku sijafanikiwa kuipata kwa bahati mbaya mke wangu bado sijamjulisha. Kwa bahati mbaya maduka muda huu Karikoo yamefungwa.

Naombeni ushauri kwani nahisi nikifika nyumbani mambo yanaweza yasiwe sawa kutokana na;

1. Nimezoea kurudi mapema nyumbani kufikia 12 jioni huwa tayari nimefika nyumbani na leo hii kuchelewa halafu sina pete.

2. Siku za hivi karibu mke wangu amekuwa akihisi natoka nje ya ndoa hivyo tumekuwa na kamvutano ka chinichini.

3. Narudi bila pete ya ndoa
mkuu kwani cheti cha ndoa huna??

Pete ina vunja ndoa au???

mbona mnakua watumwa wa akili

apo utakuta ni mtu mzima 50s unawaza sana kupoteza Pete
 
Wewe mwanaume unamuona kabisa si mwaminifu, leo hii arudi nyumbani pete hana na akuambie sababu ni alivua ili aioshe, tangu amekuoa leo ndio pete imechafuka?? Ni rahisi kuelewa pale tu mtu una imani nae.. Utamu wa ngoma huwez kuuelewa had uingie ucheze

Wako ndio haaminiki mpnz
 
'Ukageuza gali.' Ebu nambie gali ya aina gani. Maana ndolilikua lengo. Ina CC ngapi, model gani
'Akageuza gari' sio gali

Mkuu what's the big deal kuhusu yeye kumiliki gari?mbona ni kawaida tu na haijaonekana kama anajaribu kushow off?

Mpe ushauri tu
Hizo habari za CC na model ipi kamuulizie PM
 
Habari za humu wanajamiiForums,

Tangu saa 10 jioni nikiwa njiani kuelekea nyumbani kutoka kazini baada ya kumaliza kazi za leo, nimejikuta ghafla sina pete ya ndoa na katika kumbukumbu zangu nikakumbuka kuwa niliivua nikiwa ofisini nikageuza gari kurudi kazini kwa ajili ya kwenda kuichukua.

Nimefika ofisini nimetafuta pete mpaka muda huu saa 2 usiku sijafanikiwa kuipata kwa bahati mbaya mke wangu bado sijamjulisha. Kwa bahati mbaya maduka muda huu Karikoo yamefungwa.

Naombeni ushauri kwani nahisi nikifika nyumbani mambo yanaweza yasiwe sawa kutokana na;

1. Nimezoea kurudi mapema nyumbani kufikia 12 jioni huwa tayari nimefika nyumbani na leo hii kuchelewa halafu sina pete.

2. Siku za hivi karibu mke wangu amekuwa akihisi natoka nje ya ndoa hivyo tumekuwa na kamvutano ka chinichini.

3. Narudi bila pete ya ndoa
Hayo maneno kamwambie mkeo atakuelewa
 
Wewe mwanaume unamuona kabisa si mwaminifu, leo hii arudi nyumbani pete hana na akuambie sababu ni alivua ili aioshe, tangu amekuoa leo ndio pete imechafuka?? Ni rahisi kuelewa pale tu mtu una imani nae.. Utamu wa ngoma huwez kuuelewa had uingie ucheze
Uzuri sitagundua kama hana hiyo pete kidoleni coz sitamkagua vidole

Labda nione dalili nyingine

Kwa hiyo wewe ukiona ana pete kidoleni maana yake ni mwaminifu?
 
Pete ya ndoa ni agano wewe na mkeo.....

Huwezi jua alochukua ataitumiaje

Hivyo mweleze mkeo..... yake pia aivue mnunue pete mpya mkazibariki mvae.... ya mkeo akachonge hereni
 
Uzuri sitagundua kama hana hiyo pete kidoleni coz sitamkagua vidole

Labda nione dalili nyingine

Kwa hiyo wewe ukiona ana pete kidoleni maana yake ni mwaminifu?
Mimi mume wangu akirudi nampokea mimi, chumbani naenda nae mimi, nguo za haraka navua mimi kama koti, kuna vitu nitagundua tu kwa haraka kwa kua ntakua nae bzy anaporudi, kama sitagundua pete kwa muda huo kesho anapoenda kazini nitajua tu hana.
 
Uzuri sitagundua kama hana hiyo pete kidoleni coz sitamkagua vidole

Labda nione dalili nyingine

Kwa hiyo wewe ukiona ana pete kidoleni maana yake ni mwaminifu?
Hakuna kitu kinachotambulisha mtu ni mwaminifu zaid ya tabia, ila kuvaa pete yako ni seemu ya heshima kwako na kwake pia
Mimi mume wangu akirudi nampokea mimi, chumbani naenda nae mimi, nguo za haraka navua mimi kama koti, kuna vitu nitagundua tu kwa haraka kwa kua ntakua nae bzy anaporudi, kama sitagundua pete kwa muda huo kesho anapoenda kazini nitajua tu hana.
 
Back
Top Bottom