Nimepeleka zawadi: Mume kaichoma moto!

Mkuu kama umekaa na watu miaka miwili kwa ukaribu huu na hujaweza kuelewa kwamba zawadi ya kitenge kwa mama mtu itazua makubwa, basi wengine ambao hawakuwepo kwenye hiyo nyumba wakiuliza mahusiano yalikuwaje huwezi kuwalaumu kwa nini hawaelewi.

Shida yangu mimi ni unajuaje kuwa kama ningepeleka nepi asingezichoma? Kama ningepeleka hela, tuseme, 10,000 au 20,000, ambayo ni zaidi ya thamani ya kitenge unajuaje kuwa asingitupa hiyo hela? Mimi nadhani hapo ni tabia ya mtu tu.

Pengine labda niseme kitu ambacho sikupenda kukiongelea hapa. Kwamba jamaa ni mtu wa totoz tena kwa sana tu, nadhani hilo ndo linalomsumbua-huenda nahisi yale anayoyatenda huenda mkewe anatendewa pia.

Alishawahi kumzushia dada wa mwenye nyumba eti anatembea na shamba boy wa mwenye nyumba, lakini cha ajabu huyo dada wa mwenye nyumba alipoondoka, jamaa ameanza kumsalandia huyo dada wa mwenye nyumba. Sasa mwenye nyumba amejua kuwa jamaa ameshaimbisha dada yake.

Ni ujinga tu mkuu, utoe zawadi ya hela, nguo za mtoto au hata ukimnunulia yeye mume nguo bado atahoji tu na pengine kuzichoma tu moto.
 
Kwa mwendo huu watu hawakawii kutaka kupima DNA ya mtoto kuhakikisha baba wa kibaiolojia ni nani.
 
Binafsi naona hukukosea kupeleka zawadi, ila ulichokosea ni kumnunulia mzazi zawadi instead of mtoto, ulitakiwa upeleke zawadi ya mtoto na si zawadi ya mama, ila wakati wa kuondoka sasa ungetoa pesa may be sh 5000 au elfu kumi na ungesema jamani hii itasaidia kununua supu kwa ajili ya mzazi halafu ungesepa zako
 
kama ni ukaribu ulikuwa mkubwa sana ndo maana nashangaa huyo mtu ambaye tulikuwa tunakaa hata ndani kwake kuangalia mpira, ktk hili ka-behave kikengekenge

Nimegundua kitu fulani toka kwako ...chunga sana jifunze kutokana na mazingira
Wewe mkubwa na hiyo tabia hata mwenyewe unaijua
 
Sio wanaume wote wenye uelewa na zawadi ila ulichokosea ni kumpa zawadi bila kupitia kwa mmewe. Hata ingekuwa ni mimi haiwezekani ukamletea zawadi mke wangu baada ya kujifungua bila mimi kunishirikisha.
Ni zawadi aliyoamua kuwapelekea na siyo deni, amshirikishe mume kwa lipi? isitoshe alipeleka zawadi na mume alikuwepo, mi nafikiri ni wivu usokuwa na mpango, aachane nao asijepata kisu cha mgongo.
 
Ni zawadi aliyoamua kuwapelekea na siyo deni, amshirikishe mume kwa lipi? isitoshe alipeleka zawadi na mume alikuwepo, mi nafikiri ni wivu usokuwa na mpango, aachane nao asijepata kisu cha mgongo.

afadhali ya hicho kisu cha mgongo mzee hata wanao wakijua haina shida kuliko cha ma.kalio wanao wakijua heshima itashuka sana
 
Jamani mbona sijaona mahali popote , Ndyoko ameonyesha kama ni mwanaume?? Naona mmechangia kama ni mwanaume au nyie mnamjua ni mwanaume, basi ndyoko pengine kuna watu wanakufahamu kitabia...

Lakini kama ungekuwa mwanamke isingekuwa tatizo.

Kwa mwanaume, huwezi kutoa zawadi kwa mke wa mtu na hasa kama suala ni amejifungua. Navyojua, kwa ujumla sisi wanaume hawapi wanawake wa wengine zawadi, pengine utaitoa kwa umoja wetu ukiwa na mkeo. Hivyo na wewe ulitakiwa uende na mkeo.

Kama hujaoa, hayo mambo yako mbali sana na wewe .
 
Just for curiosity, hiko kitenge ulinunua wewe au mkeo? Manake ushahidi wote wa kimazingira unakutia hatiani na adhabu aliyochukua jamaa ni ndogo.

Sababu:
  • Wrong choice ya zawadi, wakati na place
  • Protocal haikufuatwa kabisa mpangaji ni wewe na mume wa mzazi
  • Na kwanini zawadi asipate mtoto au baba
  • Hakunaga urafiki wa njemba na mke wa mtu manake matokeo yanatabirika na hakuna anayetaka itoke
Wakati mwingine utakuja kupasuka ukiingia katika maguu ya watata.
 
Mwanamke akijifungua wewe kama rafiki yake unatakiwa umpongeze mumewe (mpelekee mvinyo ama msokoto wa bhange) ama upeleke zawadi ya mtoto. Kumnunulia nguo na chakula (usije ukapeleka mchele ama nyama) ni jukumu la mumewe
Wazo la pembeni: ama kitenge ulichonunua kilikuwa sub-standard ama kimezidi sana std yake hata mume akasirike.

kila siku unazidi kunishangaza aisee!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom