Kuna mambo mawili yanaweza kuhusishwa:
1: Matatizo ya mzio/allergy
Hii inaweza kuwa ni tatizo, lakini pamoja na tiba unakuwa unaendelea kutumia vitu vinavyosababisha tatizo husika. Vitu hivyo ni kama: kutumia vitu vya baridi, feni, Ac, maji ya baridi au vinywaji, matumizi ya mafuta au pafyum zenye harufu kali, vyakula vyenye rangi zisizo za asili kama ubuyu wa rangi, juice za viwandani, maeneo yenye vumbi kwa wingi nk.
2: Uwezekano wa kuwa na acid reflux
Hii ni hali ya vitu vya tumboni kuweza kupanda na kuunguza njia ya chakula na kuathiri koo pia. Wakati mwingine hali hii huchanganywa na pumu. Kwa mazingira hayo kuna mambo yanahitajika kuzingatiwa pia pamoja na upataji wa tiba sahihi. Hivyo, kunakuwa na haja ya kuonana na daktari ili kutanabaisha ni nini hada tatizo.