Nimeondolewa kwenye Tarrif 0 [Tanesco]

Nimeondolewa kwenye Tarrif 0 [Tanesco]

ndio maana unakwenda TANESCO wanai-set mita
hmm, hapana hakuna mita inayosetiwa, wana monitor matumizi yako PALE unaponunua umeme
ndiyo maana wanaweza kukuchomoa kwenye T0 ( au kukurudisha ) hukohuko uliko

kuna nyumba naijua wako kwenye T0 , tena ni ya wapangaji, wanachofanya ni kwamba, 69 zikiisha njiani, wanalala giza siku zilizobaki mpaka mwezi utimie ( siku 30 wanaongeza na siku 1 ) ndiyo WANANUNUA tena, unaona kiuhalisia hawa matumizi yao siyo 69 kwa mwezi
 
Hii 0 tarrif imetengenezewa mazingira ya kuwanyanyasa walaji, kwanini wanaweka visheria vya kikandamizaji namna hiyo kwa watu masikini!!

Ningekuwa MD wa hilo shirika ninge automate huo mfumo ufanye wenyewe kila kitu, ni suala la kuweka condition tu kama ikizidi kiasi X kwa mtu wa tariff Y mfumo usipokee fedha au upokee fedha na kupeleka salio lililozidi mwezi wa mbele lakini wanatumia umasikini wa waTz kuwahangaisha na vimasherti vya kijingakijinga visivyo na maana

Kweli kabisa aisee,kuna watu mna mawazo mazuri kuliko hata wataalamu wote wa TANESCO akiwepo waziri wao
 
hmm, hapana hakuna mita inayosetiwa, wana monitor matumizi yako PALE unaponunua umeme
ndiyo maana wanaweza kukuchomoa kwenye T0 ( au kukurudisha ) hukohuko uliko

kuna nyumba naijua wako kwenye T0 , tena ni ya wapangaji, wanachofanya ni kwamba, 69 zikiisha njiani, wanalala giza siku zilizobaki mpaka mwezi utimie ( siku 30 wanaongeza na siku 1 ) ndiyo WANANUNUA tena, unaona kiuhalisia hawa matumizi yao siyo 69 kwa mwezi
Hayo mateso yote ya nini?
 
hmm, hapana hakuna mita inayosetiwa, wana monitor matumizi yako PALE unaponunua umeme
ndiyo maana wanaweza kukuchomoa kwenye T0 ( au kukurudisha ) hukohuko uliko

kuna nyumba naijua wako kwenye T0 , tena ni ya wapangaji, wanachofanya ni kwamba, 69 zikiisha njiani, wanalala giza siku zilizobaki mpaka mwezi utimie ( siku 30 wanaongeza na siku 1 ) ndiyo WANANUNUA tena, unaona kiuhalisia hawa matumizi yao siyo 69 kwa mwezi
Ndo nimemaanisha hicho ulichoandika, nilivyosema mita ina setiwa ndo hicho ulichosema wana monitor wenyewe ila ili uwe monitored lazima uombe kuwekwa tarriff 0 na ndio maana ukinunua umeme 9150 inakuja 69 unit wakati mtu mwingine akinunua 9150 anapata kama 26 unit (hiyo ndo mita kusetiwa) kikubwa ni vigezo na masharti wa kuweka umeme mwingine baada ya mwezi
 
Jana walikata na kuwasha umeme mfululizo kama mara 3. Waliporudisha mara ya mwisho line moja yenye nyumba kama 5 ilikuwa haina umeme. Kupigiwa simu hotline yao, jamaa wakaja lakini wakasema wapewe hela ya mafuta ndio warekebishe.

Watu walikitaa kutoa mpaka mzee mmoja akajitolea 5000 ndio wakarekebisha. Hili shirika limejaa uozo toka juu mpaka chini.
Haya hatukuyaona enzi za Prof.Muhongo na yule aliyemfuatia.
Kaja January Makamba huu uhuni umerudi tena.

Mh. Samia kama upo kwa ajili yetu wananchi uondoe huu uhuni TANESCO.
Muoindo na Maharage sijui Chande ni bure kabisa hao jamaa.
 
hatufanani uchumi mzee
Tatizo la Tariff zero ni hayo mashart lukuki, watu zaid ya wawili mkimiliki fridge fasta mmeondolewa..nadhani ni aina ya umeme unao wafaa watu wenye kipato cha chini ambao hawamiliki vifaa vingi vya umeme..lakini bahati mbaya watu wanao taka kutumia tarrif zero ni wale wenye mavifaa yanayo kula umeme mwingi.
 
watu wenye kipato cha chini
na hili hasa ndiyo lengo na tanesiko, ndiyo maana sharti la kwanza uwe 'kijijini'

bahati mbaya watu wanao taka kutumia tarrif zero ni wale wenye mavifaa yanayo kula umeme mwingi.
sasa hawa ni wale ving'ang'anizi wengine walio town

friji pekee la 'nyumbani' linalamba karibia 70 units kwa mwezi hapo hujawasha taa, na takataka zingine
 
na hili hasa ndiyo lengo na tanesiko, ndiyo maana sharti la kwanza uwe 'kijijini'


sasa hawa ni wale ving'ang'anizi wengine walio town

friji pekee la 'nyumbani' linalamba karibia 70 units kwa mwezi hapo hujawasha taa, na takataka zingine
Hapa nadhani tuko pamoja mkuu,,watu wapewe hii elimu..badala ya kulalamika hovyo.
 
Hayo mateso yote ya nini?
Sema tu hiyo ni ya wapangaji ila kama ni nyumba ya familia una enjoy sana, mie fridge ilikuwa 24/7 plus kutumia heater maana kila mwezi kuna unit zinabaki 15 au 20 unakuta zinaji-accumulate yaani kuna kipindi huwa unakuwa na unit mpaka 150. Ndo walivyobadilisha mita tu na huduma ikaenda
 
na hili hasa ndiyo lengo na tanesiko, ndiyo maana sharti la kwanza uwe 'kijijini'


sasa hawa ni wale ving'ang'anizi wengine walio town

friji pekee la 'nyumbani' linalamba karibia 70 units kwa mwezi hapo hujawasha taa, na takataka zingine
na hili hasa ndiyo lengo na tanesiko, ndiyo maana sharti la kwanza uwe 'kijijini'


sasa hawa ni wale ving'ang'anizi wengine walio town

friji pekee la 'nyumbani' linalamba karibia 70 units kwa mwezi hapo hujawasha taa, na takataka zingine
Na mie ni miongoni mwa ving'ang'anizi nimetumia 4 years nikawa nina note kabisa tarehe ya kununua, uzuri ukiweka taa za LED unakuta taa ya watt 5 ina mwanga sawa na energy saver ya 11 au 18 watts.Unakuta kwa siku unacheza na unit 2 average na fridge linawaka japokuwa kuna siku inakuwa zaidi ila uki-control miezi 2 ya mwanzo unakua na balance ya umeme wa kutosha. Ila ndo hivyo tena walivyobadilisha mita na huduma ikaenda na maji
 
Sababu za kuondolewa ni kununua umeme wa elfu 10 ili itakapokatwa kodi ya makazi ibaki elf 9 ndo iwe malipo ya umeme. Sijui hata nifanyeje jamani maskini mimi
Ukinunua Tena,wanakurudisha lakini lazima urudi kwenye hesabu zilezile
 
Ilitokeaga hii kwangu wakaniambia nitumie umeme kwa miezi3
 
Sababu za kuondolewa ni kununua umeme wa elfu 10 ili itakapokatwa kodi ya makazi ibaki elf 9 ndo iwe malipo ya umeme. Sijui hata nifanyeje jamani maskini mimi
Walewafanyakazi wa solar unahisi watalipwaje mkuu n sisi kwa ss
Jiongezee m taney na makato yake nshasahau natumia mara moja moja sana
 
Hiyo ndo nitolee, kukurudisha tena labda Mkurugenzi Mkuu awe ndugu yako, ukienda utaambiwa huduma haipo wakati kiutaratibu ni ipo ndo maana hata kwenye website yao wameweka. Ukiwaandikia email au malalamiko wanapiga kimya. Mie mita iliharibika nikabadilishiwa mita ambayo automatically haipo hiyo tarriff. Nikaomba wanihamishie balance za unit zangu za mita iliyopita na kuiweka mita mpya kwenye tarriff wakapiga kimya.Nikazama kwenye website nikarusha email waka respond kwenye balance ya LUKU huku kwenye tarriff wakapiga kimya japo nimewakumbusha mara 2.Ungenunua ile ile 9150 upate 69 units
Mkuu kuna kitu haujakieleza vizuri nikakifahamu!..." ungenunua ile ile 9150 upate 69 units" unamaanisha nini?

Si anasema washamtoa, atapataje units hizo kwa bei hiyo?

Mimi msala umenitokea jana tu!

Nikawa nimejisahau sikuangalia kalenda na kengele la mita likawa linadai hadi kero!

Nikarusha ka9150, ikaja unit 21 nikatahayari!

Kuangalia angalia nikakuta kalenda bado linasoma Jan31 nikaishiwa pozi!

Kumbe walishategesha kosa lolote tu wanakurudisha kundini automatic!
 
Sababu za kuondolewa ni kununua umeme wa elfu 10 ili itakapokatwa kodi ya makazi ibaki elf 9 ndo iwe malipo ya umeme. Sijui hata nifanyeje jamani maskini mimi
Mbona mimi nanunua umeme wa Alf kumi napewa 73 units ila Kila mwezi. Wewe imekuaje kwako?
Labda matumizi yalizidi ukanunua mara 2 Kwa mwezi
 
Back
Top Bottom