Nimemwambia simtaki tena, lakini....................!

Nimemwambia simtaki tena, lakini....................!

Sinai

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2011
Posts
288
Reaction score
47
Habari wana JF! Mimi ni mwanaume, nimekuwa na mahusiano ya kimapenzi (mchumba na mali nimetoa kwao) na mdada mmoja hivi kwa muda wa miaka mitatu sasa, yeye ni mwanachuo hapo UDSM na kwa sasa ndo anamalizia degree yake. Last weekend niliamua kumtembelea huko hostel kwake bila kumjulisha, ilikuwa jumamosi nikiwa na lengo la kwenda kumchukua ili tutoke kidogo! Cha ajabu huyo binti sikumkuta, nilipo jaribu kumuuliza mwenzake anaeishi nae chumba kimoja kasema aliondoka tangu jana yake jioni (ijumaa) na hakurudi hadi mida ya saa 10 jioni ambayo mimi nilipofika pale! Nikaamua kumpigia simu, kwavile yeye alikuwa hajui kama mimi nipo pale hostel, akawa ananidanganya eti yupo hostel na tena ameboreka sana, analalamika eti nimemtosa hata simu kutwa nzima sijampigia na mambo mengi! Mimi niliamua kuondoka huku nikiwa nimekasirika sana bila kumwambia kama mimi nimefika pale hostel! Jumapili aliporudi hostel akaambiwa kuwa mimi nilifika na nilimpigia simu nikiwa pale, binti amechanganyikiwa, analia hovyo na anaomba msamaha, tena amemwambia hadi mama yake na dada yake, leo jioni dada yake anataka kuonana na mimi, wadau mnanishaurije? Nimpotezee huyu dada? Kwani mimi nimesha amua kumwacha kabisaa huyo binti, na mali niliyotoa kwao nipo tayari kusamehe!
 
Kosa moja haliachi mke.Mkanye na umchunguze kama amebadilika.
 
Umeshahamuwa kumuacha sasa hapa unahitaji kipi cha nyongeza? au ukiambukizwa ukimwi utarudi tena hapa kutuuliza kwamba utumie ARV au usitumie?
 
songa mbele kaka, maisha hayasimami......ila usiitese roho yako.....kama umeganda.... gandamizia kabisa....
 
Embu waza wewe kosa ni kudanganya au kutokulala hostel au kutokukwambia alipolala... uongo kama huo ni wa kawaida sanaa... kama humpendi muache tuu., umejisaprize mwenyewe.. hahaha!!! toa taarifa unaenda banaa, izo saprize waachie wazungu..
 
Embu waza wewe kosa ni kudanganya au kutokulala hostel au kutokukwambia alipolala... uongo kama huo ni wa kawaida sanaa... kama humpendi muache tuu., umejisaprize mwenyewe.. hahaha!!! toa taarifa unaenda banaa, izo saprize waachie wazungu..
alilala wapi? suprize ndo mpango mzima hata mimi nilienda kwa x wangu nikakuta watu bed na aliniambia amesafiri mimi nilikuwa nimefata tu vitu vyangu nilisahau huko. ZA muongo mwisho 40
 
Namchukia mtu muongo, namchukia mtu asiye muaminifu. Kwa vile roho yako ishaingia kinyongo, basi ni vyema umuache; kipindi cha uchumba maana yake ni kuchunguzana tabia so mshukuru Mungu kwa kukuonesha tabia ya mchumbao.
 
Namchukia mtu muongo, namchukia mtu asiye muaminifu. Kwa vile roho yako ishaingia kinyongo, basi ni vyema umuache; kipindi cha uchumba maana yake ni kuchunguzana tabia so mshukuru Mungu kwa kukuonesha tabia ya mchumbao.
huo wote unafiki tu dada! nachukia question mark kichwani kwangu kwa kweli!
 
alilala wapi? suprize ndo mpango mzima hata mimi nilienda kwa x wangu nikakuta watu bed na aliniambia amesafiri mimi nilikuwa nimefata tu vitu vyangu nilisahau huko. ZA muongo mwisho 40

haya asante.. kumbe ushang'atwa na nyokaa...
 
Habari wana JF! Mimi ni mwanaume, nimekuwa na mahusiano ya kimapenzi (mchumba na mali nimetoa kwao) na mdada mmoja hivi kwa muda wa miaka mitatu sasa, yeye ni mwanachuo hapo UDSM na kwa sasa ndo anamalizia degree yake. Last weekend niliamua kumtembelea huko hostel kwake bila kumjulisha, ilikuwa jumamosi nikiwa na lengo la kwenda kumchukua ili tutoke kidogo! Cha ajabu huyo binti sikumkuta, nilipo jaribu kumuuliza mwenzake anaeishi nae chumba kimoja kasema aliondoka tangu jana yake jioni (ijumaa) na hakurudi hadi mida ya saa 10 jioni ambayo mimi nilipofika pale! Nikaamua kumpigia simu, kwavile yeye alikuwa hajui kama mimi nipo pale hostel, akawa ananidanganya eti yupo hostel na tena ameboreka sana, analalamika eti nimemtosa hata simu kutwa nzima sijampigia na mambo mengi! Mimi niliamua kuondoka huku nikiwa nimekasirika sana bila kumwambia kama mimi nimefika pale hostel! Jumapili aliporudi hostel akaambiwa kuwa mimi nilifika na nilimpigia simu nikiwa pale, binti amechanganyikiwa, analia hovyo na anaomba msamaha, tena amemwambia hadi mama yake na dada yake, leo jioni dada yake anataka kuonana na mimi, wadau mnanishaurije? Nimpotezee huyu dada? Kwani mimi nimesha amua kumwacha kabisaa huyo binti, na mali niliyotoa kwao nipo tayari kusamehe!
kwanini ulitoa MALI badala ya kutoa MAHARI?
 
Habari wana JF! Mimi ni mwanaume, nimekuwa na mahusiano ya kimapenzi (mchumba na mali nimetoa kwao) na mdada mmoja hivi kwa muda wa miaka mitatu sasa, yeye ni mwanachuo hapo UDSM na kwa sasa ndo anamalizia degree yake. Last weekend niliamua kumtembelea huko hostel kwake bila kumjulisha, ilikuwa jumamosi nikiwa na lengo la kwenda kumchukua ili tutoke kidogo! Cha ajabu huyo binti sikumkuta, nilipo jaribu kumuuliza mwenzake anaeishi nae chumba kimoja kasema aliondoka tangu jana yake jioni (ijumaa) na hakurudi hadi mida ya saa 10 jioni ambayo mimi nilipofika pale! Nikaamua kumpigia simu, kwavile yeye alikuwa hajui kama mimi nipo pale hostel, akawa ananidanganya eti yupo hostel na tena ameboreka sana, analalamika eti nimemtosa hata simu kutwa nzima sijampigia na mambo mengi! Mimi niliamua kuondoka huku nikiwa nimekasirika sana bila kumwambia kama mimi nimefika pale hostel! Jumapili aliporudi hostel akaambiwa kuwa mimi nilifika na nilimpigia simu nikiwa pale, binti amechanganyikiwa, analia hovyo na anaomba msamaha, tena amemwambia hadi mama yake na dada yake, leo jioni dada yake anataka kuonana na mimi, wadau mnanishaurije? Nimpotezee huyu dada? Kwani mimi nimesha amua kumwacha kabisaa huyo binti, na mali niliyotoa kwao nipo tayari kusamehe!

Naomba Mungu tu Lara 1 asiione hii, maana sijui atacomment nini!
 
Kosa moja haliachi mke.Mkanye na umchunguze kama amebadilika.
Huyo sio mkewe soma tena topic. hata hivyo hawala hana talaka ukimtaka unampata. Angempotezea tuu lakini asingemtamkia kuwa 'baaasi' ili abaki kuwa spea tuu siku akikwama aende kujipoza kama vicheche wengine tuu. hakuna future hapoo.
 
Huyo sio mkewe soma tena topic. hata hivyo hawala hana talaka ukimtaka unampata. Angempotezea tuu lakini asingemtamkia kuwa 'baaasi' ili abaki kuwa spea tuu siku akikwama aende kujipoza kama vicheche wengine tuu. hakuna future hapoo.

Siyo mke kwa sababu hajakabidhiwa bado?Msichana ukishamtolea mahari tayari ni mke kimila,unasubiri tu baraka za kanisa au bomani.
 
Nadhani mchumba wako bado ana mambo ya kurukaruka wakati alijua wazi ana mchumba
Kama alitaka Mhogo angekwambia sasa kaenda
sijui kujiuza.


Ni vema ukawa na msimamo wa kumuacha tu.
 
sitira yake nafuu,mwambie lilo na sahihi
ajue pate fahamu,ajue mali na sio mahari
jipe kazi ya mwalimu,mjuze apate akili
naamini kwako si gumu,mjibu na ajue hili.
Sinai kakengeuka kama sio kukengeushwa
Binti alompata mahaba hanayo ila mali alotoa
Mwanazuoni anamkumbatia kwa uongo chuo amalize
Penzi litapukutika pindi mlimbwende kazi atapata
snowhite wewe wito lukuki wa wale wa CWT
Mimi hakika nimekwama, elimu kuachilia
Kaunga na gfsonwin hawa ni malenga wabobevu
elimu ya mahari watatoa vijana wasikanganyikiwe

hapa sio ukomo, si kitambo jukwaani tena nitazama
 
huo wote unafiki tu dada! nachukia question mark kichwani kwangu kwa kweli!

Halafu mtu kama huyo anakuja na thread, "simuelewi huyu mwanaume au mchumba wangu kanitosa" inaudhi kwa kweli.
 
Back
Top Bottom