Nimemuelewa Halima Mdee. Amekubali makosa, anataka maridhiano; yuko tayari kujirudi na kurekebisha mambo chamani mwao

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Leo, kama Mtanzania wa kawaida nisiye mwanachama wa chama chochote cha siasa nchini na kwingineko, nimepata bahati ya kumsikiliza Mhe. Halima Mdee aliyekuwa mzungumzaji mkuu kwenye mkutano wao na waandishi wa habari.

Mhe. Mdee alikuwa mzungumzaji mkuu wa waliofukuzwa uanachama wa CHADEMA. Ni wale 19 walioapishwa kama Wabunge wa Viti Maalum wa CHADEMA. Nimemsikiliza na kumuelewa. Unataka maridhiano, anataka amani na upatano ndani ya CHADEMA.

Kwakuwa Mhe. Mdee ni Mwanasheria kama mimi, ni wazi kuwa anajua mambo yafuatayo. Mosi, Katiba ya Tanzania ni sheria mama na ni lazima matakwa ya kikatiba yalindwe na kutekelezwa. Pili, Katiba na Sheria haziwezi kuzidiwa nguvu na kauli ya yeyote yule ndani au nje ya Tanzania.

Tatu, kwamba kuna aina za Wabunge wafuatao: (i) Wabunge wa Majimbo (ii) Wabunge wa Viti Maalum (iii) Wabunge 10 wa kuteuliwa na Rais (iv) Wabunge watano wanaochaguliwa na Baraza la Wawakilishi kutoka miongoni mwao (v) Mwanasheria Mkuu wa Serikali (vi) Spika wa Bunge kama hatokani na Wabunge.

Nne, ni Wabunge 10 tu wanaoteuliwa na Rais pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndiyo ambao si lazima wapendekezwe na kudhaminiwa na chama cha siasa katika kupatikana kwao. Waliobakia ni lazima wapendekezwe na kudhaminiwa na chama cha siasa katika kupatikana kwao na kuwa Wabunge.

Tano, iko wazi kikatiba (na haijalishi kauli ya yeyote yule) kuwa Mbunge anapopoteza uanachama wa chama kilichompendekeza na kumdhamini, ubunge wake hukoma pia. Hivyobasi, kwa kufukuzwa uanachama wao (kwakuwa uamuzi wa CHADEMA bado haujabadilishwa au kubadilika) Mhe. Halima Mdee na wenzake 18 walikoma kuwa Wabunge kikatiba na kisheria.

Sita, ubunge wa Viti Maalum una mchakato na utaratibu wake wa kikatiba, kisheria na kiutaratibu wa ndani ya vyama husika. Na kwamba Katiba, sheria na taratibu lazima zifuatwe ili kuhalalisha ubunge huo.

Kiukweli, namsifu Mhe. Halima Mdee kwa kuzungumza kwake kwa staha, busara na hekima kubwa hasa kuhusu chama chake cha zamani CHADEMA na viongozi wake. Najua bila shaka kuwa Mdee na wenzake wanajua taratibu za kufuata ili kuubadili uamuzi wa CHADEMA ndani na nje ya chama hicho.

Kwa ilivyo sasa, Mhe. Halima Mdee na wenzake 18 ambao wamefukuzwa uanachama wa CHADEMA, kikatiba na kisheria, si Wabunge. Kwa busara na staha walioionyesha Leo, wapewe nafasi ya kurekebisha mambo ndani ya CHADEMA na kusonga mbele pamoja!
 
Hapo kuweka mambo sawa ni wao kujiuzulu kwanza kwakuwa wamekiri hawakufuata taratibu za chama. Kama mchakato wa kuteua wabunge wengine wa viti maalumu utafuata sheria na kanuni za chama.

Lakini kuendelea kuwa mbunge huku anasema anaipenda CHADEMA ni kuwahadaa wanachama na wapenzi wa CHADEMA ama kuendekeza njaa tu
 

Alidhiane na nani? Hawa walishindwa. Taasisi imara ni rahisi sana kutengeneza watu imara na wapya wakati wote...

Pia taasisi ni kubwa kuliko mtu
 
Aandike barua kwa spika, amweleze hawezi kuwa mbunge viti maalumu sababu hana chama, hivyo atangaze kujiuzulu ubunge viti maalumu hadi watakapopata baraka za chama. Hapo atakuwa ameyataka maridhiano
Nimeipenda hii sana pia asome na Warumi 1;26-28 itamsaida pia kwa kuwa ametuambia tusome zaburi ya 35.
 
Nimeipenda hii sana pia asome na Warumi 1;26-28 itamsaida pia kwa kuwa ametuambia tusome zaburi ya 35.
Warumi 1 26
Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili;

Warumi 1 27
wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.

Warumi 1 28
Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.

Warumi 1 29
Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya,

Warumi 1 30
wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao,

Warumi 1 31
wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema;

Warumi 1 32
ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.
 
Leo, kama mtanzania wa kawaida nisiye mwanachama wa chama chochote cha siasa nchini na kwingineko, nimepata bahati ya kumsikiliza Mhe. Halima Mdee aliyekuwa mzungumzaji mkuu kwenye mkutano wao na waandishi wa habari...
Kwa hiyo Mdee bado anaweza kurudi bungeni pale rais akiamua kumchagua kuwa miongoni mwa watu 10 anaoruhusiwa kuwachagua? au ni lazima watu k10 amaowachagua raisi ni lazima watoke katika chama tawala?
 
Aandike barua kwa spika, amweleze hawezi kuwa mbunge viti maalumu sababu hana chama, hivyo atangaze kujiuzulu ubunge viti maalumu hadi watakapopata baraka za chama. Hapo atakuwa ameyataka maridhiano
Halima angekuwa na unyenyekevu wa kiwango hicho wala asingekata rufaa Mkutano Mkuu wa Chama. Hukumu anayotamani kupata huko ni kuruhusiwa kuendelea na ubunge japo kakiuka taratibu za kuupata ubunge wenyewe!
 
Hatua ya kwanza kuelekea maridhiano wanatakiwa wote kujivua ubunge wa Ndugai kwanza ili rufaa iwe na mashiko.

Vinginevyo hata balaza kuu watakutana na rungu hilo hilo au baya zaidi ya lile la mwanzo.
Kikatiba hao siyo wabunge tena wa bunge la JMT,mara tu baada ya kuvuliwa uanachama
 
Halima angekuwa na unyenyekevu wa kiwango hicho wala asingekata rufaa Mkutano Mkuu wa Chama. Hukumu anayotamani kupata huko ni kuruhusiwa kuendelea na ubunge japo kakiuka taratibu za kuupata ubunge wenyewe!
Hilo alifute mwenyewe kichwani mwake mapeema kabla ya kuingia kwenye hicho kikao
 
Halima Mdee ni Mwanasiasa kweli kweli, hongera Bibie , Hongera Mbunge wangu wa Kawe kwa miaka 10
Ajabu kuwa huyu ni mwanasheria lakini alishau kabisa jambo muhimu la kumshitumu mtu - ushahidi. Huyu bibi alisema ameona kwa macho yake karatasi feki za kura katika jimbo lake.

Lakini akiwa kama mwanasheria alishindwa kuwashirikisha askari au kuchukuwa ushahidi na kuufikisha kwa NEC, polisi au hata mahakamani.

Ajabu sana hakuja na picha au clip zake yeye binafspamoja na hizo karatasi, hakuja na majina ya watu waliokuwepo huko alikozikuta hizo karatasi feki ila alikuja ma neno tu. Halafu sasa anageuka na kukubali kufanya kazi na wale wale aliowaita wezi.
 
Aandike barua kwa spika, amweleze hawezi kuwa mbunge viti maalumu sababu hana chama, hivyo atangaze kujiuzulu ubunge viti maalumu hadi watakapopata baraka za chama. Hapo atakuwa ameyataka maridhiano
Akifanya hivyo, atakuwa "anaruhusu kingi kwa kugawa kete tatu"!
 
Back
Top Bottom