Nimemtimua kuchota maji aliyevaa nguo ya CCM

Nimemtimua kuchota maji aliyevaa nguo ya CCM

Status
Not open for further replies.
hujatenda ubinaadam siasa siyo chuki.dada akiwa ccm wewe cdm pendaneni na mshindane kwa hoja chuki na kuona mwenzio hafai kupenda kile anachoamini ni ufinyu wa akili.
vijana tunafanya siasa zisizo na tija kwa taifa letu.leo wewe umemtimua kwasababu kavaa kijani kesho wewe unaweza ukatumbukia kwenye hicho kisima na wakukusaidia ni huyo jirani yako badilika.

Kupata maji safi na salama kwa mujibu wa ahadi za ccm ni tendo na siyo hoja. Wameshindwa kuleta maji alafu wewe unakuja kunitambia na liccm lako lililoishiwa pumzi lazima nikufanyizie.
 
Yaani ina maana unataka kuniambia haukumsindikiza na kelebu hata tatu tuu.
 
Bavicha at its best!

Sometimes you will never know the value of your ignorance and stupidity, until it becomes open secret
 
kwa hiyo hapo umesolve tatizo mkuu? Hujui kama katiba inamruhusu mtu kuwa huru kumchagua na kumsaport mtu yeyote? any way mkapa hakukosea kabsa kuwaita lile jina manaake leo umeudhihirisha mwenyewe ujinga na ulofa wako humu. Tena bila aibu unakuja humu majesticaly et nimemtimua na panga, shame upon you!.
 
Siasa sio ushabiki wa Simba na Yanga siasa ni maisha, na sipendi mtu anayeshabikia Siasa kama mpira, mpira hauna athari ila Siasa zina athari.
Kijijini kwangu kuna shida ya Maji toka Uhuru wagombea wanapita hawa hawa wanaopewa mashati na 5000 wanawachagua wanaondoka baada ya miaka miaka mitano tena wanarudi na ahadu ile ile.

toa darasa wakija hapo kwenye kisima kabla hajachota maji mwambie dada hiki kisima kilitakiwa kichimbwe na serikali lakini kutokana na uhuni wao wameshindwa sasa mimi ninakuomba badilika ili hivi visima vije vichimbwe na serikali nyingine mbona rahisi tu.
 
kama huwataki bora uwaue wote ubaki peke yako, hiyo siyo akili wala democrasia..kwa nn mnalazimisha watu? too much!
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom