Nimemtimua kuchota maji aliyevaa nguo ya CCM

Nimemtimua kuchota maji aliyevaa nguo ya CCM

Status
Not open for further replies.

The Businessman

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2014
Posts
7,397
Reaction score
9,263
Amani iwe kwenu,

Binafsi isitafsiliwe kama chuki ila kiukweli nimetokea kutopendezwa kabisa na rangi ya KIJANI. Kwangu vaa nguo ya kijani hata salamu yangu sikupi.

Nipo Kijijini huku, na kwa maeneo haya pekee shambani kwangu nina kisima cha maji na ndio karibu kijiji kizima wanategemea hapa. Wabunge wa CCM wanapita wanahahidi wataleta maji wanapita wanaondoka.

Sasa jana narudi kutoka mjini namkuta baba mmoja ambaye sikuwahi kumuona pale amevaa kapelo na shati kuukuu la CCM anachota maji yangu, nilichofanya nikamuita mama watoto nilitee panga hapo ndipo ugonvi ulipoanza na yule bwana, kwanini unachota maji yangu?... hana jibu nikamuelesha lakini nikaja kugundua ni mfia bendera ..timua toka nyumbani kwangu na marufuku mwana CCM kuja kuchota maji hapa.

Napata shida sana watu wanaoshabikia CCM, anaimba #HAPA KAZI TU na wakati hata maji tu kwake ni tatizo.

CCM IMEWEKEZA KWENYE UMASKINI WA WATANZANIA
 
Kwahiyo umekichukuliaje hicho kitendo kwa maana kwamba kinafaa kuigwa au hakifai kuigwa?
 
Kinafaa sana hicho ili kupata maji walioahidi maana usipofanya hivyo utakuwa hujamsaidia ndugu kapelo kukuu ya ccm kuhoji ahadi ya maji na kuchukua hatua
 
hujatenda ubinaadam siasa siyo chuki.dada akiwa ccm wewe cdm pendaneni na mshindane kwa hoja chuki na kuona mwenzio hafai kupenda kile anachoamini ni ufinyu wa akili.
vijana tunafanya siasa zisizo na tija kwa taifa letu.leo wewe umemtimua kwasababu kavaa kijani kesho wewe unaweza ukatumbukia kwenye hicho kisima na wakukusaidia ni huyo jirani yako badilika.
 
HII inaonyesha namna akili yako ndogo NA ulivyo NA roho mbaya NA WATU wakikuendekeza iko siku KAMA wewe ni mkristo au mwislamu hamtashirikiana NA ubaguzi huo utaendelea kikabila rangi etc.NA HII hajaanza lea ndiomaana tunasema cdma ni wabaguzi.njoo kwangu nitakupa siomaji tu hata chakula ccm hoye
 
Kwahiyo umekichukuliaje hicho kitendo kwa maana kwamba kinafaa kuigwa au hakifai kuigwa?

Ndio ni cha kuigwa, kwa sababu mmewalisha ujinga watu mnawapa 5000 wawapigie kura huku mkiwahahidi huduma muhimu baada ya miaka mitano mnarudi tena na ahadi ile ile. Na nimebandika bango kabisa marufuku kuja kwangu umevaa matambala ya CCM.
 
hujatenda ubinaadam siasa siyo chuki.dada akiwa ccm wewe cdm pendaneni na mshindane kwa hoja chuki na kuona mwenzio hafai kupenda kile anachoamini ni ufinyu wa akili.
vijana tunafanya siasa zisizo na tija kwa taifa letu.leo wewe umemtimua kwasababu kavaa kijani kesho wewe unaweza ukatumbukia kwenye hicho kisima na wakukusaidia ni huyo jirani yako badilika.

Siasa sio ushabiki wa Simba na Yanga siasa ni maisha, na sipendi mtu anayeshabikia Siasa kama mpira, mpira hauna athari ila Siasa zina athari.
Kijijini kwangu kuna shida ya Maji toka Uhuru wagombea wanapita hawa hawa wanaopewa mashati na 5000 wanawachagua wanaondoka baada ya miaka miaka mitano tena wanarudi na ahadu ile ile.
 
Mkuu umefanya vizuri kabisa ata Mungu mwenyewe anasema "watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa" huyo mzee wa kapelo kuu kuu hana akili kichwani kwani badala ya kujiuliza hao anaowashabikia wanaishi maisha ya anasa adi wana kinai na huku yeye ata maji ya kunywa hana, umefanya la maana sana kama ana maarifa akajitafakari.
VIVA UKAWA!!!!
 
Hukumtendea haki. Jua alichokosa huyo bwana ni elimu ya uraia ambayo amenyimwa na ccm kwa makusudi ili aendelee kuwa mtaji wao.

Ulichotakiwa kufanya ni kum-elimisha ajue ubaya wa ccm pia akija kuchota maji asivae hayo matambara. MAJI NI UHAI tusinyimane
Uhai sababu ya wajinga wa ccm walioko madarakani.
 
hujatenda ubinaadam siasa siyo chuki.dada akiwa ccm wewe cdm pendaneni na mshindane kwa hoja chuki na kuona mwenzio hafai kupenda kile anachoamini ni ufinyu wa akili.
vijana tunafanya siasa zisizo na tija kwa taifa letu.leo wewe umemtimua kwasababu kavaa kijani kesho wewe unaweza ukatumbukia kwenye hicho kisima na wakukusaidia ni huyo jirani yako badilika.


Ninyi mnapowajaza ujinga ni ubinadamu ningekuwa Mimi ningemkalia kooni sana
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom