Nimempenda kuliko wote. Lakini hanipendi.

Nimempenda kuliko wote. Lakini hanipendi.

MwanaHaki

R I P
Joined
Oct 17, 2006
Posts
2,401
Reaction score
710
Waungwana.

Mimi ni Mkristo. Nina ndoa. Miaka 10. Kila ndoa ina tatizo. Haikosi. Ninampenda sana mke wangu mpaka nahisi najipendekeza kwake. Namuombea sana kwa Mungu ili abadilike. Siwezi kukata tamaa.

Lakini wahenga walinena: Maji yakimwagika hayazoleki.

Je, nifanye nini?

Hakosi upendo toka kwangu. Kila kitu ndani ya nyumba. Nguo, chakula, mapenzi, pesa, vyote anavyo. Lakini kasema amechoka.

Nibwage manyanga huku nikijua namkosea Mungu au niende kwa Baba Paroko nikatake msaada wa Kanisa? Sisi wote Wakatoliki.

Nasubiri ushauri wenu. Nampenda. Sitaki kumuacha.
 
sekta zote umezitaja lakini sijaona sekta nyeti ya perfomance kwa bed,umejaribu kuzungumza nae kujua tatizo ni nini?ukute mwenzio ana makubwa na mazito yanayomsibu moyoni mwake,njia pekee ni kuvunja ukimya zungumza na mwenzio kwa hisani ya wamarekani ili kujua kiini cha tatizo kabla hujaenda kwa baba paroko.Ukute vyote unampa lakini kuna vitabia vyako ni kero kwake na hutaki kubadilika na wala huna mpango hivyo anahisi ameelemewa na kachoka totally.
 
Hebu tueleze huwa anakwambia "amechoka", je ushawahi kumdadisi amechoshwa na kitu gani?
 
Waungwana.

Mimi ni Mkristo. Nina ndoa. Miaka 10. Kila ndoa ina tatizo. Haikosi. Ninampenda sana mke wangu mpaka nahisi najipendekeza kwake. Namuombea sana kwa Mungu ili abadilike. Siwezi kukata tamaa.

Lakini wahenga walinena: Maji yakimwagika hayazoleki.

Je, nifanye nini?

Hakosi upendo toka kwangu. Kila kitu ndani ya nyumba. Nguo, chakula, mapenzi, pesa, vyote anavyo. Lakini kasema amechoka.

Nibwage manyanga huku nikijua namkosea Mungu au niende kwa Baba Paroko nikatake msaada wa Kanisa? Sisi wote Wakatoliki.

Nasubiri ushauri wenu. Nampenda. Sitaki kumuacha.

Hakuna marefu yasiyo na ncha. Nakushauri kaa naye chini na muombe akueleze ukweli wa nini kilichomchosha. Inawezekana ikawa ni tabia zako, au kuna fununu kasikia sehemu kuhusu wewe au unaweza ukakuta kuna jambo jingine tofauti kabisa na vile tunavyofikiria linamtatiza na kumfanya aone uhusiano wenu hauna maana.

Usikate tamaa, nafasi bado unayo ya kuitengeneza ndoa yenu. Ndoa hujengwa na nyie wawili ndani ya ndoa na kitendea kazi muhimu kabisa kwenye ujenzi wenu ni mawasiliano. Anza sasa huku ukiendelea kumuomba Mungu naamini mambo yako yatakaa sawa.

All the best,
HP
 
kipindi cha nyuma hujawahi kumuumiza?
coz mke akuchukie tu from no wre
asiwe na mapenzi na ww ngumu
wewe labda kuna ambayo ulishamfanyia ya kumuumiza!
matatizo ya saikolojia hayo!poleee

 
kabla ya kufika kwa baba paroko kaeni wawili muyazungumze penda kujua tatizo nini je anachoshwa na nini hapo ndipo pakuanzia......jaribu nawe kujichunguza kuna kitu labda kinamkera muda na hutaki kubadili
 
Huyo anatingisha kibiriti, aliyechoka hasemi angeshaondoka kitambo. Simama kwenye nafasi yako kama baba wa nyumba, fanya yote yanayostahili wewe ufanye na usisite kumwambia awe huru kuondoka au kukaa.
 
Mbona waliochangia wengi wanawake? Nimefarijika sana..!!! Mkuu mwanamke ni zaidi ya ulivyotaja, sometimes they need to be treated like children..! So just seat down n talk to her friendly..!!!
 
sekta zote umezitaja lakini sijaona sekta nyeti ya perfomance kwa bed,umejaribu kuzungumza nae kujua tatizo ni nini?ukute mwenzio ana makubwa na mazito yanayomsibu moyoni mwake,njia pekee ni kuvunja ukimya zungumza na mwenzio kwa hisani ya wamarekani ili kujua kiini cha tatizo kabla hujaenda kwa baba paroko.Ukute vyote unampa lakini kuna vitabia vyako ni kero kwake na hutaki kubadilika na wala huna mpango hivyo anahisi ameelemewa na kachoka totally.

Kama idara zote sawa..hilo la kwa bed ndo tatizo..
Kama tatizo sio tendo la ndoa basi ur workaholic..mpe muda mwenzio.
na kama sio hayo basi utakuwa unamnyanyasa either ana elimu ndogo au hafanyi kazi.
Fanyia kazi hapo
 
Jamani pole kaka usimwache hakuna mwanamke asiyependa kufanyiwa yote hayo uliyoyasema there must b something wrong somewhere c bure kaka yangu kaa chini zungumza nae atililike safi sana kwa macare hayo big up

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
muulize anahitaji nauli kiasi gani kumfikisha anakokwenda,,, au anahitaji msaada gani akaanze new life.............huyo wako haendi popote... mbwembwe tuu.
 
Jamani kaka pole na matatizo,mimi naona kaa naye ongea naye kirafiki, muulize amechoshwa na nini?huduma zote anapata huwezi jua upande wa kitandani humfurahishi pia muombe mungu akusaidie swala hili watu wanaona dogo sana,lakini lina sumbua sana akili,,tumuombee atabadilika chaooooooo
 
Jamani asanteni sana kwa michango yenu yote. Nitaitilia maanani na nitaifanyia kazi. Mmenisaidia sana. Kumbe kweli WanaJF wote ni ndugu!

Bwana Awabariki!

Amina!
 
duh pole broo, kwani toka umuoe hiyo tabia anayo toka mwanzoni mwa ndoa yenu?
 
Jamani asanteni sana kwa michango yenu yote. Nitaitilia maanani na nitaifanyia kazi. Mmenisaidia sana. Kumbe kweli WanaJF wote ni ndugu!

Bwana Awabariki!

Amina!
Wakati mwingine huwa ni pepo, jaribu kupata spiritual deliverance kwa wote wawili. Pole sana, usiache kufunga na kuomba!
 
Waungwana.

Mimi ni Mkristo. Nina ndoa. Miaka 10. Kila ndoa ina tatizo. Haikosi. Ninampenda sana mke wangu mpaka nahisi najipendekeza kwake. Namuombea sana kwa Mungu ili abadilike. Siwezi kukata tamaa.

Lakini wahenga walinena: Maji yakimwagika hayazoleki.

Je, nifanye nini?

Hakosi upendo toka kwangu. Kila kitu ndani ya nyumba. Nguo, chakula, mapenzi, pesa, vyote anavyo. Lakini kasema amechoka.

Nibwage manyanga huku nikijua namkosea Mungu au niende kwa Baba Paroko nikatake msaada wa Kanisa? Sisi wote Wakatoliki.

Nasubiri ushauri wenu. Nampenda. Sitaki kumuacha.

Stori yako ngumu kushauri maana iko one sided sana,umezungumzia yanayokusibu wewe tu,hatuna undani wa mke wako. ngoja waje wataalam,lkn nionavyo mimi tatizo linaweza kuwa kwako...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom