Nimempa mimba, ananichukia hataki hata kuniona

Nimempa mimba, ananichukia hataki hata kuniona

Kitaalamu hakuna uhusiano kati ya mimba na kumchukia mtu....au kiburi..sasa mwambie aache hizo tabia,kama vip piga chini tafuta mwingine
 
Hyo ni kawaida kwa hali aliyo nayo kwa ushauri itakuwa vyema kama utapata elimu mwanamke mjamzito tabia zao na mengineyo
 
Jamani, mnijuzeni mwenzenu mpenzi wangu tulikuwa tumeamua kuishi pamoja kabla ya kuhalalisha kwa watumishi wa Mungu.

Wakati huo tunasubiria tukawa tunamega taratibu tunda la mti wa katikati, ghafla mwenzangu mara kavimbiwa, kichefuchefu mara woohh....(katapika) alipoenda kupima akakuta amenasa.

Sasa shida ananichukia vibaya mno na sasa hivi yuko na kisirani na kiburi, ananiangalia kwa jicho la dharau sana!

Na mimi nimeona isiwe shida nimehama zangu nikarudi makazi yangu ya mwanzo, analalamika nirudi na mimi nimegoma.

Anataka nikajitambulishe kwao na mimi nikifikiria anavyonichukia nimemwambia kamwe siendi na pia ana kitabia cha kunishurutisha mara kwa mara kwa kunitumatuma ovyo..." Sielewi kapatwa na nini?

Ushauri jamani.

ushauri unaoomba ni wa nini hasa?....kama "UMEMPA MTU KITU NA ANAKUZINGUWA"...."MNYANGANYE TENA KWA NGUVU ZOTE ATIE DISIPILINI"
 
Kama unajua tabia za mwanamke mjamzito wala usingehama, coz inatakiwa the more anakuchukia the more unamwonyesha mapenzi, coz si yeye ni hormones zinafanya kazi.
 
Wanaume waelewa wa haya mambo ni wachace sana. Mtafute daktari wa akina mama akupe somo likuingie vizuri, uache kumtesa huyo dada.
 
Anakutuma hoyo tabia kaanza b4 hajavimbiwa au alivyovimbiwa?
 
hahahaha hiyo ni psychology tuuu kutokana na hali yake ...so jua hali hiyo umchukulie tuuu...cheza na mazingira tuu ila usikimbie mazima akizaa atakupenda sana n hali tuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom