Kipeperushi
Senior Member
- Aug 17, 2011
- 167
- 33
Habari zenu wakuu wa janvi... Kimsingi bado sijapata picha kuhusu mrembo huyu. Kama ni member wa jf nitafurahi kama na yeye ata-coment, naamini nitamsoma tu kulingana na coment yake. Stori nzima iko hivi:- Niliwahi kupewa contact ya mrembo moja na rafiki yangu kwa ajili ya kujenga urafiki na binti huyu ambaye by that time alikuwa ni mkazi wa Mjini Magharibi, huko Zenj. Kwa kweli nia ya kujenga urafiki nae ilikuwa ni kwamba hatimae aje kuwa mke wangu. Idea hii niliipata toka kwa huyo rafiki yangu kwa sababu huyo mrembo alikuwa rafiki wa mke wa huyo rafiki yangu. Rafiki yangu alishawishika kuniunganisha na mrembo huyo kutokana na mapenzi ya binti huyo kutaka kuwa na mume ambae ni rafiki wa karibu na yeye (rafiki yangu). Baada ya kuanza mahusiano ya simu, mahusiano ambayo yalichukua takribani mwaka mmoja na zaidi kidogo kabla hatujaonana na huyo mrembo, hatimae huyo mrembo alinialika nimtembelee Zenj. Ki msingi wakati huo hali yangu ya kiuchumi haikuwa nzuri sana kwa sababu nilikuwa nje ya kazi kwa muda mrefu kidogo. Lakini kutokana na kampani ya marafiki zangu nilifanikiwa kudondoka Mjini Magharibi. Bahati nzuri wakati haya yote yanaendelea nilijitahidi kumwekea wazi mrembo huyo kuhusu hali halisi ya maisha yangu ilivyo. Mrembo huyo ambae kiasili ni mzaliwa wa Tanzania Bara, alikuwa anaishi Zenji kikazi. Jambo la ajabu ni kwamba wakati naelekea Zenji kwa mwaliko wake huyo bibie, nikiwa najua kama yeye ndie mwenyeji wangu, mrembo huyo alikataa kata kata nisifikie nyumbani kwake. Hivyo nililazimika kufikia hoteli, ambapo kutokana na gharama za kimaisha za huko Zenji nililazimika pia kufupisha muda wa ziara yangu toka wiki moja hadi 24hrs. Kwa kusema kweli nilitokea kumpenda sana huyu bibie, hasa kwa sababu hata yeye pia alionyesha kunipenda sana hata kabla hatujaonana. Baada ya muda kupita tukiwa tunaendelea na mawasiliano yetu kama kawaida tulipanga kukutana tena Dar es Salaam mimi nikiwa natokea Mbeya na yeye akiwa anatokea Zenji, ili tujadiliane mpango wa awali wa ndoa yetu, ikiwa ni pamoja na mimi kwenda kutambulika rasmi kwa wazazi wake Dodoma, nilichelewa kumlaki airport Dar. Kwa kweli sababu ya msingi ilikuwa ni mipango ya kipesa tu, ndio ilinichelewesha, kwakuwa katika ujio wake safari hii yeye ndiye alikuwa mwalikwa na mimi ndiye mwenyeji wake, na bahati mbaya kutokana na kuchelewa kwangu kufika Dar toka safari yangu ya Mbeya, mipango ya kipesa ilikuwa haijakaa sawa mpaka muda ambao ndege aliyosafiria huyo bibie ilipowasili Dar. Hata hivyo niliwasiliana nae na bahati nzuri baadae tulikutana nae baada ya yeye kuja mwenyewe kwa daladala. Baada ya tukio hilo mawasiliano yetu yamedhoofika kwa kiasi kikubwa kiasi kwamba hata dalili za maendeleo ya mipango yetu ya ndoa zimepotea kabisa...! Ndugu zangu wanaJf, nimeuleta uzi huu hapa jamvini kwa sababu naamini kwamba hiki ni kiwanja cha watu wenye fikra pevu. Naomba mawazo yenu, lengo langu ni kurudisha uhusiano wangu na huyo bibie, tatizo langu ni kwamba nahisi mrembo amenidharau.