Nimelikosea Wapi? Naomba Mawazo Yenu.

Kipeperushi

Senior Member
Aug 17, 2011
167
33
Habari zenu wakuu wa janvi... Kimsingi bado sijapata picha kuhusu mrembo huyu. Kama ni member wa jf nitafurahi kama na yeye ata-coment, naamini nitamsoma tu kulingana na coment yake. Stori nzima iko hivi:- Niliwahi kupewa contact ya mrembo moja na rafiki yangu kwa ajili ya kujenga urafiki na binti huyu ambaye by that time alikuwa ni mkazi wa Mjini Magharibi, huko Zenj. Kwa kweli nia ya kujenga urafiki nae ilikuwa ni kwamba hatimae aje kuwa mke wangu. Idea hii niliipata toka kwa huyo rafiki yangu kwa sababu huyo mrembo alikuwa rafiki wa mke wa huyo rafiki yangu. Rafiki yangu alishawishika kuniunganisha na mrembo huyo kutokana na mapenzi ya binti huyo kutaka kuwa na mume ambae ni rafiki wa karibu na yeye (rafiki yangu). Baada ya kuanza mahusiano ya simu, mahusiano ambayo yalichukua takribani mwaka mmoja na zaidi kidogo kabla hatujaonana na huyo mrembo, hatimae huyo mrembo alinialika nimtembelee Zenj. Ki msingi wakati huo hali yangu ya kiuchumi haikuwa nzuri sana kwa sababu nilikuwa nje ya kazi kwa muda mrefu kidogo. Lakini kutokana na kampani ya marafiki zangu nilifanikiwa kudondoka Mjini Magharibi. Bahati nzuri wakati haya yote yanaendelea nilijitahidi kumwekea wazi mrembo huyo kuhusu hali halisi ya maisha yangu ilivyo. Mrembo huyo ambae kiasili ni mzaliwa wa Tanzania Bara, alikuwa anaishi Zenji kikazi. Jambo la ajabu ni kwamba wakati naelekea Zenji kwa mwaliko wake huyo bibie, nikiwa najua kama yeye ndie mwenyeji wangu, mrembo huyo alikataa kata kata nisifikie nyumbani kwake. Hivyo nililazimika kufikia hoteli, ambapo kutokana na gharama za kimaisha za huko Zenji nililazimika pia kufupisha muda wa ziara yangu toka wiki moja hadi 24hrs. Kwa kusema kweli nilitokea kumpenda sana huyu bibie, hasa kwa sababu hata yeye pia alionyesha kunipenda sana hata kabla hatujaonana. Baada ya muda kupita tukiwa tunaendelea na mawasiliano yetu kama kawaida tulipanga kukutana tena Dar es Salaam mimi nikiwa natokea Mbeya na yeye akiwa anatokea Zenji, ili tujadiliane mpango wa awali wa ndoa yetu, ikiwa ni pamoja na mimi kwenda kutambulika rasmi kwa wazazi wake Dodoma, nilichelewa kumlaki airport Dar. Kwa kweli sababu ya msingi ilikuwa ni mipango ya kipesa tu, ndio ilinichelewesha, kwakuwa katika ujio wake safari hii yeye ndiye alikuwa mwalikwa na mimi ndiye mwenyeji wake, na bahati mbaya kutokana na kuchelewa kwangu kufika Dar toka safari yangu ya Mbeya, mipango ya kipesa ilikuwa haijakaa sawa mpaka muda ambao ndege aliyosafiria huyo bibie ilipowasili Dar. Hata hivyo niliwasiliana nae na bahati nzuri baadae tulikutana nae baada ya yeye kuja mwenyewe kwa daladala. Baada ya tukio hilo mawasiliano yetu yamedhoofika kwa kiasi kikubwa kiasi kwamba hata dalili za maendeleo ya mipango yetu ya ndoa zimepotea kabisa...! Ndugu zangu wanaJf, nimeuleta uzi huu hapa jamvini kwa sababu naamini kwamba hiki ni kiwanja cha watu wenye fikra pevu. Naomba mawazo yenu, lengo langu ni kurudisha uhusiano wangu na huyo bibie, tatizo langu ni kwamba nahisi mrembo amenidharau.
 
katafute pesa kwanza....

no finance no romance......

no money no honey.....

get it?
Pesa iko mbaya sana mkuu. Tatizo sio pesa, tatizo ni vipi narudisha uhusiano wetu kwenye nguvu yake ya awali. Mwanzoni alijua sina pesa na alinielewa, na sasahivi anjua nina pesa lkn kapoa kabisa, unanisoma vizuri the boss?
 
Habari zenu wakuu wa janvi... Kimsingi bado sijapata picha kuhusu mrembo huyu. Kama ni member wa jf nitafurahi kama na yeye ata-coment, naamini nitamsoma tu kulingana na coment yake. Stori nzima iko hivi:- Niliwahi kupewa contact ya mrembo moja na rafiki yangu kwa ajili ya kujenga urafiki na binti huyu ambaye by that time alikuwa ni mkazi wa Mjini Magharibi, huko Zenj. Kwa kweli nia ya kujenga urafiki nae ilikuwa ni kwamba hatimae aje kuwa mke wangu. Idea hii niliipata toka kwa huyo rafiki yangu kwa sababu huyo mrembo alikuwa rafiki wa mke wa huyo rafiki yangu. Rafiki yangu alishawishika kuniunganisha na mrembo huyo kutokana na mapenzi ya binti huyo kutaka kuwa na mume ambae ni rafiki wa karibu na yeye (rafiki yangu). Baada ya kuanza mahusiano ya simu, mahusiano ambayo yalichukua takribani mwaka mmoja na zaidi kidogo kabla hatujaonana na huyo mrembo, hatimae huyo mrembo alinialika nimtembelee Zenj. Ki msingi wakati huo hali yangu ya kiuchumi haikuwa nzuri sana kwa sababu nilikuwa nje ya kazi kwa muda mrefu kidogo. Lakini kutokana na kampani ya marafiki zangu nilifanikiwa kudondoka Mjini Magharibi. Bahati nzuri wakati haya yote yanaendelea nilijitahidi kumwekea wazi mrembo huyo kuhusu hali halisi ya maisha yangu ilivyo. Mrembo huyo ambae kiasili ni mzaliwa wa Tanzania Bara, alikuwa anaishi Zenji kikazi. Jambo la ajabu ni kwamba wakati naelekea Zenji kwa mwaliko wake huyo bibie, nikiwa najua kama yeye ndie mwenyeji wangu, mrembo huyo alikataa kata kata nisifikie nyumbani kwake. Hivyo nililazimika kufikia hoteli, ambapo kutokana na gharama za kimaisha za huko Zenji nililazimika pia kufupisha muda wa ziara yangu toka wiki moja hadi 24hrs. Kwa kusema kweli nilitokea kumpenda sana huyu bibie, hasa kwa sababu hata yeye pia alionyesha kunipenda sana hata kabla hatujaonana. Baada ya muda kupita tukiwa tunaendelea na mawasiliano yetu kama kawaida tulipanga kukutana tena Dar es Salaam mimi nikiwa natokea Mbeya na yeye akiwa anatokea Zenji, ili tujadiliane mpango wa awali wa ndoa yetu, ikiwa ni pamoja na mimi kwenda kutambulika rasmi kwa wazazi wake Dodoma, nilichelewa kumlaki airport Dar. Kwa kweli sababu ya msingi ilikuwa ni mipango ya kipesa tu, ndio ilinichelewesha, kwakuwa katika ujio wake safari hii yeye ndiye alikuwa mwalikwa na mimi ndiye mwenyeji wake, na bahati mbaya kutokana na kuchelewa kwangu kufika Dar toka safari yangu ya Mbeya, mipango ya kipesa ilikuwa haijakaa sawa mpaka muda ambao ndege aliyosafiria huyo bibie ilipowasili Dar. Hata hivyo niliwasiliana nae na bahati nzuri baadae tulikutana nae baada ya yeye kuja mwenyewe kwa daladala. Baada ya tukio hilo mawasiliano yetu yamedhoofika kwa kiasi kikubwa kiasi kwamba hata dalili za maendeleo ya mipango yetu ya ndoa zimepotea kabisa...! Ndugu zangu wanaJf, nimeuleta uzi huu hapa jamvini kwa sababu naamini kwamba hiki ni kiwanja cha watu wenye fikra pevu. Naomba mawazo yenu, lengo langu ni kurudisha uhusiano wangu na huyo bibie, tatizo langu ni kwamba nahisi mrembo amenidharau.

tulia tafuta kazi, ukisha pata kibarua ndo mtafute, kwa sasa huwezi kumwelewa kwakuwa una mambo mengi kichwani. lakini kwanini usiongee na huyo aliyekuunganishia huyo mchumba? wao wanafahamiana hivyo aweza saidia zaidi , kuliko hapa JF
 
He he he he, mrembo kajilipia ndege afu unampandisha daladala?
Ni sawa na kula msosi saafi afu unakula desert ya nhundwa, the ugliest fruit huko nakotoka.
 
Mkuu Nakushauri tafuta ajira kwanza! Maisha ni pamoja na pesa, hawa wenzetu wanaangalia sana security yao hasa mshiko wako.
Ukpata kazi nzuri mtafute utasikia visingizio mia kidogo
 
...'they say woman never goes back financially, while man never goes back romantically'....land job/b'ness earn some dough, take her out...atleast she'll feel secure and jet to your strip for good...
 
Mkuu huyo atakuwa ameweka hela mbele kuliko kitu chochote kile so kuwa makini sana na ikiwezekana haraka sana iwezekavyo mpotezee sio lazima umuowe yeye,out there kuna wanawake wengi sana tena sana wanatafute waume wa kuwaowa jaribu ku play nao vizuri tu,achana na huyo atakuumiza kichwa tu hapo,.....
 
he he he pole ndugu ila punguza jazba,kumbuka mtu asiyeweza kukuvumilia wakati una matatizo hakufai.....anyway,man up andf call her umuulize imekuwaje amebadilika gafla.inawezekana ana mwengine tayari
 
Kama ishu yako ya kifedha haikumsumbua tangu mwanzo, (maana aliamua mwenyewe kujisafirisha kuja kukuona pamoja na kwamba alijua hujakaa vizuri kwenye maswala ya pesa) jua hajaridhika na kile alichokiona.
Kwa kiasi fulani watu wanaokua wameingia kwenye mahusiano kabla ya kuonana hua hawaendelee kama walivyokua mwanzo baada ya kuonana uso kwa uso.Sijui kama mlishatumiana picha au la, ila jua kwamba kama hamkua mmetumiana basi ile picha aloyojijengea kichwani mwake haifanani kabisa na wewe ulivyo.Na kama mlishatumiana basi picha yako ilimpa picha ambayo ni tofauti kidogo na ulivyo. Kwa ufupi ni kwamba muonekano wako sio sawa na vile alivyotarajia.

Na kama hiyo ndio hali halisi hamna unachoweza kufanya, labda kama unaweza kubadili muonekano wako ili umpe furaha ya macho kama ulivyompa ya moyo mpaka akaja kukuona.
 
Tatizo lako nadhani ni kutokuwa responsible.Kwanza huwezi kung'ang'aniza kukutana na demu kwake wakati hamjuani na ndiyo kwanza mnakutana uso kwa uso.Inaelekea ulishawahi kumuonyesha vitabia vingine kama hivi kabla.Kama mlipanga muda mrefu umpokee airport halafu wewe unachelewa mpaka bibiye akapanda daladala,huoni kwamba umeshindwa kuonyesha tabia ya ukomavu?Inawezekana demu anapenda ku keep time na siyo kuwekana wekana mahala bila mpango.Kwako inaweza kuwa sababu ndogo lakini kuna watu hiki ni kigezo tosha cha kukuona hufai kuwa naye katika mahusiano.
 
yaani mtu kaja na ndege we ukamuacha apande daladala
na unasema pesa unayo?
ama sielewi au we muongo au huyo mdada ndo aliona humjali kabisa
 
Kawaida kama ulianza uhusiano na mwanamke/mwanaume mapema may be tokea primary ila zinakuwa zile za kitoto toto lakini urafiki wenu unaendelea kudumu mwishowe mnapozidi kukua ndivyo na uhusiano/urafiki wenu unazidi kukua pia then mnakuja kujikuta mmekuwa wapenzi, hapa huwa kuna asilimia kubwa ya penzi lenu kuwa la dhati hata kama mmoja wapo hana standard nzuri ya maisha coz mlifahamiana mapema LAKINI ndugu yangu KIPEPERUSHI huyo binti ulimtamani kwanza kwasababu si rahisi kupenda kitu 100% kabla ya kukiona na inapelekea kushirikisha moja kati ya milango ya fahamu...so mwanzoni wewe haikuwa hivyo, pengine mwenzio alisha kujengea picha flani huyu mtu yuko hivi na vile so alivyo kuta haviko kama ile Imagination yake ni rahisi sana wewe kuwekwa pending..Kumbuka dimbwi la maji halipimwi kwa kuzamisha mguu... Umesha dumbukia sasa inakuwa tabu kwako kujiokoa ila Usikatee tamaa itajipa tu pengine si chaguo lako.

"Is Not Easy by Lucky Dube"
 
Kama ishu yako ya kifedha haikumsumbua tangu mwanzo, (maana aliamua mwenyewe kujisafirisha kuja kukuona pamoja na kwamba alijua hujakaa vizuri kwenye maswala ya pesa) jua hajaridhika na kile alichokiona.
Kwa kiasi fulani watu wanaokua wameingia kwenye mahusiano kabla ya kuonana hua hawaendelee kama walivyokua mwanzo baada ya kuonana uso kwa uso.Sijui kama mlishatumiana picha au la, ila jua kwamba kama hamkua mmetumiana basi ile picha aloyojijengea kichwani mwake haifanani kabisa na wewe ulivyo.Na kama mlishatumiana basi picha yako ilimpa picha ambayo ni tofauti kidogo na ulivyo. Kwa ufupi ni kwamba muonekano wako sio sawa na vile alivyotarajia.

Na kama hiyo ndio hali halisi hamna unachoweza kufanya, labda kama unaweza kubadili muonekano wako ili umpe furaha ya macho kama ulivyompa ya moyo mpaka akaja kukuona.

Mmh, umenitisha kwa hiyo statement maana mi pia inanihusu, but kwa upande wangu we do exchange pichaz na kila siku we skype everyday
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom