Django doer
JF-Expert Member
- Jun 30, 2023
- 723
- 2,003
Wakuu za usiku .
Leo baada ya kutoka kwenye mihangaiko yangu nikaamua kupanda daladala za kwenda Makumbusho.
Sasa siti zilikuwa zimeisha nikaamua kusimama tu, cha kushangaza aliyekuwa amekaa kwenye siti alikuwa anatazama JF😅 nilishtuka na kufurahi pamoja na kushangaa sana 🤣.
Maana kwangu mimi JF ni kama sehemu zangu za siri, hakuna rafiki au ndugu anayenijua kuwa niko humu.
Hata nikitumiaga JF naitumiaga gizani au sehemu isiyokuwa na watu.
Sasa we mama uliyekuwa unakunywa juisi ya miwa na biskuti nakushauri tu ujifunze kujisitiri ndio maana tunatumia fake IDs humu.
Si vyema ukatumia huu mtandao mbele za watu maana huwezi jua nyampara ni nani 💂💂💂🧑✈️.
Yangu ni hayo tu wakuu.
Leo baada ya kutoka kwenye mihangaiko yangu nikaamua kupanda daladala za kwenda Makumbusho.
Sasa siti zilikuwa zimeisha nikaamua kusimama tu, cha kushangaza aliyekuwa amekaa kwenye siti alikuwa anatazama JF😅 nilishtuka na kufurahi pamoja na kushangaa sana 🤣.
Maana kwangu mimi JF ni kama sehemu zangu za siri, hakuna rafiki au ndugu anayenijua kuwa niko humu.
Hata nikitumiaga JF naitumiaga gizani au sehemu isiyokuwa na watu.
Sasa we mama uliyekuwa unakunywa juisi ya miwa na biskuti nakushauri tu ujifunze kujisitiri ndio maana tunatumia fake IDs humu.
Si vyema ukatumia huu mtandao mbele za watu maana huwezi jua nyampara ni nani 💂💂💂🧑✈️.
Yangu ni hayo tu wakuu.