Nimekuta kinyesi cha binadamu mlangoni kwangu

Nimekuta kinyesi cha binadamu mlangoni kwangu

Habari za mchana jamani.

Leo nimeamka nimekuta kinyesi cha binadamu tena mtu kanya usiku kiko fresh kabsa, nikiwaza ilivyo ngumu mtu kuingia ndan ya compound au kuruka geti na kuingia na kisha kunya hapo ndo nawaza,kwa sababu ni ngumu sana,nilijaribu kuwashirikisha wapangaj wenzangu nao wanaduwaa ila kuna mmoja kanieleza hyo hali ni ushirikina.

Nakuja kwenu najua watu humu mna elimu mbalimbal naombe mnieleze kwa wanaojua implication ya kukuta mtu kanya mlangoni. Cc mshana jr na wengine
Tendo hilo hufanywa na wezi ambao huwa wanaamini kwa kufanya hivyo hakuna mtu anaweza kuamka na kuwafukuzia. Hakuna zaidi ya hilo na ni common hata huku kaskazini
 
Mkuu hicho ni kinyesi kama kinyesi kingine chochote. Muhimu tafuta aliyefanya hicho kitendo na sii vinginevyo. Ukiruhusu hisia za kichawi na ushirikina kuingia kwenye akili yako utajichanganya. Ujue nguvu ya "UCHAWI" inategemeana na nguvu ya imani yako katika UCHAWI.
 
95% ya watanzania wanaamini na kushiriki mambo ya kishirikina.

95% ya watanzania wanaamini na kushiriki ibada za dini mbalimbali..
 
Ndo umeogopa hata kupiga picha..ungeweka picha wataalam wa mambo humu wengi ujue!!wangechunguza rangi, kiasi, ukubwa na angle mzigo ulipo, wangekupa majibu zaidi
 
Weka majivu na kuyazoa wala usimalize pesa zako kwa waganga waogo. Mwisho hakuna binadamu mwenye uwezo wa kupindisha malengo ya mungu aliyokupangia. Jamii yetu ina imani ya kishirikina hata watakaochangia uzi wako utawaona walivyo na imani za kishirikina
 
Matatizo ya kuisha vibaya na jamii inayokuzunguka.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom