Habari wana MMU!
Pamoja na kwamba ni member jf na msomaji wa maoni yanayotolewa hapa MMU lakini sikuwahi kupost chochote hapa MMU,lakini leo nimekuja kwenu kuomba ushauri.
Mimi ni kijana niliye na mke na watoto wawili mapacha ingawa bado sijafunga ndoa.Huyu mke alikuwa ni mpenzi wangu wa siku nyingi. Baada ya mimi kumaliza chuo nikawa nimepata kazi mkoa tofauti na aliko mpenzi wangu,sasa katika kuondoa upweke nikawa namtumia nauli anakuja kunitembelea.Baada ya muda akiwa amerudi kwao akaniambia ana ujauzito, kwa kweli sikubisha ingawa kuoa nilikuwa bado hii inatokana na kuwa nilikuwa bado sijajipanga kabisa.
Baada ya kama wiki moja hivi akaniambia anataka atoe ule ujauzito mimi nilimkatalia na bahati nzuri certificate yake aliyokuwa anasomea alikuwa ametoka kufanya mtihani wa mwisho,ikabidi nimwambie aje kwangu. kipindi ninaye sasa akawa anatafutwa na baba yake ingawa mama yake alikuwa anajua na hii inatokana na kwamba baba mkwe na mama mkwe walishatengana kwa hiyo wako mikoa tofauti, na mimi nilikuwa nawasiliana na mama mkwe ila baba mkwe nilikuwa siwasilani naye kutokana na kuogopa, ila mama mkwe akawa ananisisitizia niende nikajitambulishe na nili mhakikishia mama mkwe kuwa nitaenda.
Baada ya miezi tisa mke wangu akajifungua mapacha na wakati huo baba mkwe alishajua mtoto wake yuko kwa mwanaume na akawa anawasiliana na mtoto wake huku akimwambia anipeleke nikajitambulishe.
Ikabidi tupange kuwa watoto wakikomaa inanilazimu niende kwa baba mkwe na hii ilikuwa tumepanga mwezi december 2013.Ghafla kwa bahati mbaya mama watoto akafiwa na baba mdogo wake kwa hiyo hapa sikuwa na jinsi ikabidi tuongozane wote kwenda msibani huku mawazo tele nikimwogopa baba mkwe.
Baada ya kufika msibani huku nikiwa nimeongozana na kaka yangu pamoja na watu wengine watatu tulipokelewa vizuri.Baada ya muda ukaanza utambulisho, watu wangu wakajitambulisha kuwa sisi ndo tumezaa na mwanao na ndo tunakaa naye, upande wao wakakubali na tukaweka bahasha yenye pesa ndani.
Sasa akili yao yote kutokana na kuwa nimekaa na mtoto wao kwa muda kama mwaka mmoja na nusu bila kujitambulisha basi wakajua nimekwenda kumaliza kila kitu yaani mahari wakati mimi haikuwa hivyo ila nilijua watanipimia kiasi cha mahari halafu ndo tujadiliane muda wa kutoa.
Baada ya muda wakaja na kiasi cha jumla ya shilingi milioni 4 .Tukawaambia hatujajiandaa kwa kutoa mahari, tuliwaambia hivi tukitaka kwanza watupe muda halafu baada ya hapo ndo tujitetee kiasi hicho kipungue,lakini wakaja juu huku wakisema tuna wadharau.Ikabidi tuwape akina shangazi mtu ambao ndo walikuwa wako juu kiasi cha sh. elfu 50 kama tu kupooza.
Baada ya hapo ikabidi watuambie mwakani(2014) mahari tunatakiwa kutoa, kutokana na hali ilivyokuwa pale ikabidi tukose hata kujitetea ikabidi tukubali tu. Baada ya kama siku mbili nikamfuata mke wangu na nikarudi naye sehemu ninayofanyia kazi huku baba mkwe akisisitiza mahari.
Sasa 2014 ndo imeingia na baba mkwe anataka mahari lakini kwa kiasi cha sh.milioni 4 ni nyingi sana na nimejaribu kumuuliza mke wangu kuwa labda aongee na akina shangazi lakini jibu alilo nipa mke wangu kwa kweli lilinihuzunisha.
Mke wangu ananiambia nitajuana na ukoo wangu hapa akimaanisha kuwa eti mahari labda nitalipiwa na mtu yeyote kwenye ukoo wangu,wakati siyo kweli ,mke wangu anajua hali halisi kuwa mahari itatokana na mshahara wangu kwa kuwa baba alishafariki.
Kwa hiyo wana MMU ninaomba ushauri nianzie wapi ili hicho kiasi kiweze kupungua angalau hata milion 2.
Pamoja na kwamba ni member jf na msomaji wa maoni yanayotolewa hapa MMU lakini sikuwahi kupost chochote hapa MMU,lakini leo nimekuja kwenu kuomba ushauri.
Mimi ni kijana niliye na mke na watoto wawili mapacha ingawa bado sijafunga ndoa.Huyu mke alikuwa ni mpenzi wangu wa siku nyingi. Baada ya mimi kumaliza chuo nikawa nimepata kazi mkoa tofauti na aliko mpenzi wangu,sasa katika kuondoa upweke nikawa namtumia nauli anakuja kunitembelea.Baada ya muda akiwa amerudi kwao akaniambia ana ujauzito, kwa kweli sikubisha ingawa kuoa nilikuwa bado hii inatokana na kuwa nilikuwa bado sijajipanga kabisa.
Baada ya kama wiki moja hivi akaniambia anataka atoe ule ujauzito mimi nilimkatalia na bahati nzuri certificate yake aliyokuwa anasomea alikuwa ametoka kufanya mtihani wa mwisho,ikabidi nimwambie aje kwangu. kipindi ninaye sasa akawa anatafutwa na baba yake ingawa mama yake alikuwa anajua na hii inatokana na kwamba baba mkwe na mama mkwe walishatengana kwa hiyo wako mikoa tofauti, na mimi nilikuwa nawasiliana na mama mkwe ila baba mkwe nilikuwa siwasilani naye kutokana na kuogopa, ila mama mkwe akawa ananisisitizia niende nikajitambulishe na nili mhakikishia mama mkwe kuwa nitaenda.
Baada ya miezi tisa mke wangu akajifungua mapacha na wakati huo baba mkwe alishajua mtoto wake yuko kwa mwanaume na akawa anawasiliana na mtoto wake huku akimwambia anipeleke nikajitambulishe.
Ikabidi tupange kuwa watoto wakikomaa inanilazimu niende kwa baba mkwe na hii ilikuwa tumepanga mwezi december 2013.Ghafla kwa bahati mbaya mama watoto akafiwa na baba mdogo wake kwa hiyo hapa sikuwa na jinsi ikabidi tuongozane wote kwenda msibani huku mawazo tele nikimwogopa baba mkwe.
Baada ya kufika msibani huku nikiwa nimeongozana na kaka yangu pamoja na watu wengine watatu tulipokelewa vizuri.Baada ya muda ukaanza utambulisho, watu wangu wakajitambulisha kuwa sisi ndo tumezaa na mwanao na ndo tunakaa naye, upande wao wakakubali na tukaweka bahasha yenye pesa ndani.
Sasa akili yao yote kutokana na kuwa nimekaa na mtoto wao kwa muda kama mwaka mmoja na nusu bila kujitambulisha basi wakajua nimekwenda kumaliza kila kitu yaani mahari wakati mimi haikuwa hivyo ila nilijua watanipimia kiasi cha mahari halafu ndo tujadiliane muda wa kutoa.
Baada ya muda wakaja na kiasi cha jumla ya shilingi milioni 4 .Tukawaambia hatujajiandaa kwa kutoa mahari, tuliwaambia hivi tukitaka kwanza watupe muda halafu baada ya hapo ndo tujitetee kiasi hicho kipungue,lakini wakaja juu huku wakisema tuna wadharau.Ikabidi tuwape akina shangazi mtu ambao ndo walikuwa wako juu kiasi cha sh. elfu 50 kama tu kupooza.
Baada ya hapo ikabidi watuambie mwakani(2014) mahari tunatakiwa kutoa, kutokana na hali ilivyokuwa pale ikabidi tukose hata kujitetea ikabidi tukubali tu. Baada ya kama siku mbili nikamfuata mke wangu na nikarudi naye sehemu ninayofanyia kazi huku baba mkwe akisisitiza mahari.
Sasa 2014 ndo imeingia na baba mkwe anataka mahari lakini kwa kiasi cha sh.milioni 4 ni nyingi sana na nimejaribu kumuuliza mke wangu kuwa labda aongee na akina shangazi lakini jibu alilo nipa mke wangu kwa kweli lilinihuzunisha.
Mke wangu ananiambia nitajuana na ukoo wangu hapa akimaanisha kuwa eti mahari labda nitalipiwa na mtu yeyote kwenye ukoo wangu,wakati siyo kweli ,mke wangu anajua hali halisi kuwa mahari itatokana na mshahara wangu kwa kuwa baba alishafariki.
Kwa hiyo wana MMU ninaomba ushauri nianzie wapi ili hicho kiasi kiweze kupungua angalau hata milion 2.