Zero IQ
JF-Expert Member
- Dec 21, 2016
- 13,917
- 24,674
Ni siku mbili sasa toka Nivamiwe na wezi waliovunja Ofisi yangu iliyokuwa unaniweka mjini na kuiba kila kitu,
Hakika sikuamini ile siku Asubuhi nilipofika kufungua na kukuta OFisi nyeupe haina kitu ata kimoja ilinibidi nitazame mara mbili mbili bila kuamini kilichotokea,
Nilipatwa na mshituko ukizingatia ndio ilikuwa imepita wiki moja tu toka Nitumie kiasi changu cha pesa cha Akiba kuapdate mazingira ya ofisi, na kuongeza baadhi ya vitu ili ili pawe na muonekano mzuri wa kushawishi wateja,
Kiukweli baada ya Tukio nilitoa taarifa ofisi ya mtendaji, pia nikaenda kutoa taarifa polisi na kupewa RB,
Kinachonisikitisha ni kwamba muda wangu wote niliokuwa na ofisi ya kazi nilikuwa mtu wa kusaidia sana Washkaji, Ndugu jamaa na Marafiki panapokuwa na Shida kwa kipato changu tu hicho hicho ninachopata,
Lakini sasa baada ya kupata matatizo hakuna ambae amenishika mkono ata na kidogo,
Ndugu, rafiki na jamaa zangu wote niliwapa taarifa ya tatizo lilonikuta lakini niliishia kupewa Pole tu ya mdomo,
Hakuna ata mmoja aliyejaribu kuniuliza au kusema chukua hiki kitakusaidia wakati huu wa mpito Hakuna kabisa,
Sijui labda wanasubiri mpaka niwaombe lakini mimi Siwezi,
Katika maisha yangu neno Naomba nilishalipigaga marufuku haijarishi napitia hali gani ya kiuchumi,
Nilipambana kupata hivyo vitu kwa jasho, Naamini pia nitapata tena lakini kwa sasa Nimejifunza kitu kimoja tu kuwa na Roho Ngumu.
Hakika sikuamini ile siku Asubuhi nilipofika kufungua na kukuta OFisi nyeupe haina kitu ata kimoja ilinibidi nitazame mara mbili mbili bila kuamini kilichotokea,
Nilipatwa na mshituko ukizingatia ndio ilikuwa imepita wiki moja tu toka Nitumie kiasi changu cha pesa cha Akiba kuapdate mazingira ya ofisi, na kuongeza baadhi ya vitu ili ili pawe na muonekano mzuri wa kushawishi wateja,
Kiukweli baada ya Tukio nilitoa taarifa ofisi ya mtendaji, pia nikaenda kutoa taarifa polisi na kupewa RB,
Kinachonisikitisha ni kwamba muda wangu wote niliokuwa na ofisi ya kazi nilikuwa mtu wa kusaidia sana Washkaji, Ndugu jamaa na Marafiki panapokuwa na Shida kwa kipato changu tu hicho hicho ninachopata,
Lakini sasa baada ya kupata matatizo hakuna ambae amenishika mkono ata na kidogo,
Ndugu, rafiki na jamaa zangu wote niliwapa taarifa ya tatizo lilonikuta lakini niliishia kupewa Pole tu ya mdomo,
Hakuna ata mmoja aliyejaribu kuniuliza au kusema chukua hiki kitakusaidia wakati huu wa mpito Hakuna kabisa,
Sijui labda wanasubiri mpaka niwaombe lakini mimi Siwezi,
Katika maisha yangu neno Naomba nilishalipigaga marufuku haijarishi napitia hali gani ya kiuchumi,
Nilipambana kupata hivyo vitu kwa jasho, Naamini pia nitapata tena lakini kwa sasa Nimejifunza kitu kimoja tu kuwa na Roho Ngumu.