The tolerance 1
JF-Expert Member
- Sep 10, 2022
- 404
- 512
Habari zenu wandugu.
Niende moja kwa moja kwenye mada, jamani jambo hili linaniumiza sana kila nikifikiria nashindwa kuamini. Mimi ni ke, nimeishi na mwanaume takribani miaka saba, tumeishi kama mke na mume na kila kitu kilikuwa kimeshafanyika kuanzia utambulisho wa pande zote na posa, ilibaki tu tarehe ya kufunga ndoa. Katika kipindi chote hicho tulifanikiwa kupata watoto wawili Mungu alitujalia.
Lakini pia tulifanikiwa kununua kiwanja na kuanza kujenga, na pia tulifanikiwa kununua kigari kidogo angalau cha kutembelea, japo hayo yote alikuwa akifanya mwenzangu halafu anakuja tu kunipa taarifa. Wakati tunaanza maisha hatukuwa na chochote, tulianza na kulala chini tena kwenye chumba cha giza takribani miezi mitatu ya mwanzoni, hata kula yenyewe ilikuwa ya tabu lakini tulivumiliana huku tukimuomba Mungu kuwa ipo siku atatjalia na sisi.
Nifupishe kidogo hadithi hii, kuna kipindi mwenzangu aliniambia anataka apange chumba kingine tofauti na nyumbani kwa kuwa alipokuwa anafanyia kazi ni mbali na nyumbani, hivyoo wakati mwingine anakosa wateja kwa kuchelewa. Tulikubaliana kuwa akapange tu kwasababu ni jambo la muda mfupi tu, hakuna shida.
Basi tulikubaliana akaenda kupanga lakini nikimuuliza mbona wakati wa kurudi haji na nguo nyumbani nifue, anasema anafua tu mwenyewe, wakati alikuwa anaimbia muda ni mchache na wateja ni wengi. Kwahiyo alisema anafua mwenyewe, alikuwa analala huko siku tatu au nne au week ndiyo anakuja nyumbani, anasalimia tu na kesho yake anaondoka tena, ila kwa kuwa nilimwamini sikuwa na tabu.
Basi ilipita takribani miezi sita fikiria sijui mume wangu analala wapi, kuna siku nakamwambia kwa upendo tu baba T naomba kwenda kupaona unapolala ili hata likitokea la kutokea nipate cha kusema kwa wazazi wako, maana wanajua nipo na wewe, na hawajui unalala sehemu nyingine tofauti na hapa nyumbani.
Heee,, ilikuwa ni ugomvi mkubwa! Yaani alikataa katukatu kunipeleka, nilikaa kimya kwa muda wa mwezi tena nikamuuliza, alikataa tena kunipeleka nikamwambia basi sitakuuliza tena. Siku ziliendelea kusogea nikawa sina amani na yeye tena. Ilifika wakati pia nikimkumbusha kuhusu kufunga ndoa anakuwa mkali sana, ndipo nikawa na wasiwasi kuna jambo linaendelea ambalo mimi silijui.
Nilikaa chini nikalia machozi nikamwambia Mungu kama kuna kitu kinaendelea aniambie. Baada kama ya wiki mbili hivi nilifanikiwa kuishika simu yake maana siku zote nilikuwa siishiki, ina 'password' na akimaliza kutumia anazima.
Aliniambia nimletee baada ya kusikia inaita, ikatokea bahati mbaya nikashika sehemu ya Whatsapp, lo! Ilikuwa ni huzuni, kumbe mwenzangu alikuwa ameshaoa mwanamke mwingine na wameshazaa mtoto mmoja tayari! Nilivyomuuliza aliniambia niamue kubaki tuwe wawili au niondoke, lakini yeye hawezi kumuacha yule mwanamke na kashamtambulisha kwao na mama yake pia anamjua.
Niliumia sana sana maana sikutegemea kwa miaka yote hiyo angenigeuka namna hiyo. Baada kama ya wiki mbili hivi aliondoka kabisa nyumbani na watoto na kwenda kuishi na yule mwanamke. Kilichonifanya nije huku ni kwamba ananiambia ameniacha kwa sababu nina mikosi, nimeishi naye lakini hakupata pesa.
Wakati tunaishu naye tulifanikiwa kununua kiwanja chenye thamani takribani 12m, duka na gari, na wakati tunakutana hatukua na chochote. Hizi pesa zote tulizipata tukiwa pamoja. Sasa napatwa na butwaa, hii inaweza kuwa kweli?
Wenzangu mliyopitia hali kama hii mlifanyaje? Ushauri wenu jamani katika hili, limeniumiza sana hili, lakini pia nimekuwa single mama bila kutarajia kwa mtu ambaye nilimuamini kupita kiasi na ndiyo mwanaume wa kwanza kwangu na sikuwahi hata mara moja kumsaliti, japo alikuwa ananiweka katika mazingira magumu sana.
Naombeni ushauri wenu maana naumizwa na mengi.
Asanteni.
Niende moja kwa moja kwenye mada, jamani jambo hili linaniumiza sana kila nikifikiria nashindwa kuamini. Mimi ni ke, nimeishi na mwanaume takribani miaka saba, tumeishi kama mke na mume na kila kitu kilikuwa kimeshafanyika kuanzia utambulisho wa pande zote na posa, ilibaki tu tarehe ya kufunga ndoa. Katika kipindi chote hicho tulifanikiwa kupata watoto wawili Mungu alitujalia.
Lakini pia tulifanikiwa kununua kiwanja na kuanza kujenga, na pia tulifanikiwa kununua kigari kidogo angalau cha kutembelea, japo hayo yote alikuwa akifanya mwenzangu halafu anakuja tu kunipa taarifa. Wakati tunaanza maisha hatukuwa na chochote, tulianza na kulala chini tena kwenye chumba cha giza takribani miezi mitatu ya mwanzoni, hata kula yenyewe ilikuwa ya tabu lakini tulivumiliana huku tukimuomba Mungu kuwa ipo siku atatjalia na sisi.
Nifupishe kidogo hadithi hii, kuna kipindi mwenzangu aliniambia anataka apange chumba kingine tofauti na nyumbani kwa kuwa alipokuwa anafanyia kazi ni mbali na nyumbani, hivyoo wakati mwingine anakosa wateja kwa kuchelewa. Tulikubaliana kuwa akapange tu kwasababu ni jambo la muda mfupi tu, hakuna shida.
Basi tulikubaliana akaenda kupanga lakini nikimuuliza mbona wakati wa kurudi haji na nguo nyumbani nifue, anasema anafua tu mwenyewe, wakati alikuwa anaimbia muda ni mchache na wateja ni wengi. Kwahiyo alisema anafua mwenyewe, alikuwa analala huko siku tatu au nne au week ndiyo anakuja nyumbani, anasalimia tu na kesho yake anaondoka tena, ila kwa kuwa nilimwamini sikuwa na tabu.
Basi ilipita takribani miezi sita fikiria sijui mume wangu analala wapi, kuna siku nakamwambia kwa upendo tu baba T naomba kwenda kupaona unapolala ili hata likitokea la kutokea nipate cha kusema kwa wazazi wako, maana wanajua nipo na wewe, na hawajui unalala sehemu nyingine tofauti na hapa nyumbani.
Heee,, ilikuwa ni ugomvi mkubwa! Yaani alikataa katukatu kunipeleka, nilikaa kimya kwa muda wa mwezi tena nikamuuliza, alikataa tena kunipeleka nikamwambia basi sitakuuliza tena. Siku ziliendelea kusogea nikawa sina amani na yeye tena. Ilifika wakati pia nikimkumbusha kuhusu kufunga ndoa anakuwa mkali sana, ndipo nikawa na wasiwasi kuna jambo linaendelea ambalo mimi silijui.
Nilikaa chini nikalia machozi nikamwambia Mungu kama kuna kitu kinaendelea aniambie. Baada kama ya wiki mbili hivi nilifanikiwa kuishika simu yake maana siku zote nilikuwa siishiki, ina 'password' na akimaliza kutumia anazima.
Aliniambia nimletee baada ya kusikia inaita, ikatokea bahati mbaya nikashika sehemu ya Whatsapp, lo! Ilikuwa ni huzuni, kumbe mwenzangu alikuwa ameshaoa mwanamke mwingine na wameshazaa mtoto mmoja tayari! Nilivyomuuliza aliniambia niamue kubaki tuwe wawili au niondoke, lakini yeye hawezi kumuacha yule mwanamke na kashamtambulisha kwao na mama yake pia anamjua.
Niliumia sana sana maana sikutegemea kwa miaka yote hiyo angenigeuka namna hiyo. Baada kama ya wiki mbili hivi aliondoka kabisa nyumbani na watoto na kwenda kuishi na yule mwanamke. Kilichonifanya nije huku ni kwamba ananiambia ameniacha kwa sababu nina mikosi, nimeishi naye lakini hakupata pesa.
Wakati tunaishu naye tulifanikiwa kununua kiwanja chenye thamani takribani 12m, duka na gari, na wakati tunakutana hatukua na chochote. Hizi pesa zote tulizipata tukiwa pamoja. Sasa napatwa na butwaa, hii inaweza kuwa kweli?
Wenzangu mliyopitia hali kama hii mlifanyaje? Ushauri wenu jamani katika hili, limeniumiza sana hili, lakini pia nimekuwa single mama bila kutarajia kwa mtu ambaye nilimuamini kupita kiasi na ndiyo mwanaume wa kwanza kwangu na sikuwahi hata mara moja kumsaliti, japo alikuwa ananiweka katika mazingira magumu sana.
Naombeni ushauri wenu maana naumizwa na mengi.
Asanteni.