Nimeichukia Taarabu ya kisasa

Nimeichukia Taarabu ya kisasa

Taarabu ulikuwa muziki wa mwambao wenye mahadhi tulivu na yenye kuburudisha mno ,hata mashairi yake yalibeba mafumbo ya kweli aingia mipasho matusi na kejeli za wazi.

Tangu hapo taarabu ikapoteza maana kabisa kuanzia mashairi mavazi mpaka uimbaji na uchezaji.

siku hizi maonyesho ya taarabu ni sehemu muhimu ya mashoga siku hizi Taarabu ni shortcut ya kuchambana uswahilini

Taarabu imepoteza maana imechuja imechakachuliwa vibaya mno
Shehe hiyo si taarabu ni MIPASHO kama CHAKACHA iliyopigwa uporo.
 
1459944216180.jpg
mkuu mshana jr ila taarabu kama hizo huzichukii maana kuna taarabu za aina nyingi
 
Itakuwa mleta mada mwenyewe Mshana Jr kafanya yake ili post iweze kuchangiwa.
[emoji85] [emoji134] [emoji85] [emoji134] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125]
 
Sivutiwi kabisa na modern taarab hata wimbo mmoja, taarab ilikuwa enzi za kina Ustadh mukrim,mohammed mrisho, Culture,egpytion musical club,Golden star hapo kwetu tanga,
 
Kabla hujatokewa na jamaa aliyekupa kazi mpya ya kupiga ramli? teh teh teh...sio mbali sana 2012
[emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Duu post ya zamani kweli hii
Ulianzisha mwenyewe khalafu unastuka?kiukweli siku hizi kuna kunukishana vikwapa tofauti na waqt ule neno limefichwa vyombo vimetulia siku hizi mziki mwepesi pana kibao cha njoo huwa naburdika sana japo si original version ila chanikumbusha mbali
Nimengi sana mpenzi yalo ni jaa moyoni
Sijifai sijiwezi hali yangu taabani
Njoo mpenzi wangu njoo
Rejesha yako imani
Wakokea moto ukisha kuwaka mzimaji nani
Siku hizi ukiniuliza hata moja sijui mahaba ya taarab ya sasa yameniisha.
 
Mkunwa na mkunaji ni yupi huona tamu...
Kuna jambo natarajii iii..kujua hilo hakika...×2
Zamani raha
 
Chonge mameee ooh Chonge tate nanee
Mpunga wasia ndege kaamie.....
 
Hahhahahaaaa hii fasihi kali sana hapa naona alimaanisha hanithi hadindishi hata anywe mchuzi wa pweza

Ndio hivo Mkuu! Ilikuwa ili uelewe lazima uwe na akili! Kuna moja inaitwa "Kinyozi" anaimba anapenda ustaarabu wa kinyozi akitaka kumshughulikia Mteja lazima asimame. Tafuta hiyo uisikilize
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom