Nimeibiwa Xiaomi 12T Pro nikanunua Google Pixel 7A

Nimeibiwa Xiaomi 12T Pro nikanunua Google Pixel 7A

Traxtion

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2021
Posts
5,901
Reaction score
11,794
Nilikuwa natumia Xiaomi 12T Pro Kwa muda sasa ila majuzi usiku hapa Mbeya wahuni walinikaba na kunipora kila nilichonacho including my phone. Uzuri sikuwa na hela nyingi mfukoni kwa hiyo kitu cha maana walichooba kinachoniuma zaidi ni hiyo Xiaomi 12T Pro
Lakini nimeitumia for 3 years straight kwa hiyo sijahangaika kuitrack ikabidi ninunue simu ya kujishikiza chapchap lakini on limited budget.
Kuna rafiki yangu alinipa kasimu ka kujishikiza siku mbili tatu ila kalikuwa na uwezo mdogo
So nikafikiria ninunue Google Pixel 7A nitumie kwa muda kisha nitanunua simu nyingine huko mbeleni. Lakini baada ya kutumia hii simu kwa wiki moja na nusu hivi nimefuta mipango ya kununua simu nyingine hivi karibuni

Ile Xiaomi 12T Pro ilikuwa na better chipset, features nyingi kwenye software, slightly better display in my opinion na nilikuwa napenda, kwa matumizi yangu ilikuwa perfect
Lakini nilichogundua ni kwamba haina tofauti kubwa na Pixel 7A kimatumizi. Labda storage ile ilikuwa na 256GB hii ina 128GB.
Google Pixel 7A zilikuwa hazitunzi chaji sana ila baada ya ku update kwenda Android 16 inakaa na chaji kama tu ile Xiaomi yangu.
Nilipanga Pixel 7A iwe simu yangu ya muda mfupi ila kwa kuwa kwa upande wangu nimeona haina kasoro hata moja (kwa matumizi yangu) I think I'll keep using it for long time. It's just as perfect as Xiaomi 12T Pro

Hii nitakuwa makini nisiibiwe na nimekoma kuzurura usiku peke yangu 🙌

Also camera naona hapa kwenye Pixel 7A ni nzuri kidogo kuliko 12T Pro ila tofauti si kubwa sana
Sample photos hizi hapa chini. Hapa ni Mbeya actually
PXL_20260205_090630266.jpg
PXL_20260205_090649750.jpg
PXL_20260205_090853617.MP.jpg
PXL_20260205_090914512.jpg

PXL_20260206_060635674.jpg
PXL_20260206_112407574.jpg
PXL_20260206_140632171.MP.jpg

PXL_20260205_170621083.jpg
PXL_20260205_171343908.MP.jpg

.
.
Hii nimepiga jana saa 2 usiku with night sight off
PXL_20260207_170813539.MP.jpg

.
.
Na hii nimepiga baada ya kuweka Night Sight same location
PXL_20260207_170822779.NIGHT.jpg

.
Mwisho nawashauri msipende kuzurura sehemu ambayo haina watu peke yake usiku. Mimi huwa nazurura sana usiku na napenda maeneo ambayo hayana watu ila baada ya kupigwa tukio, sijajaribu tena kwenda maeneo yenye ukimya usiku
 
Nice Dude!
Sharing is caring..
Gharama za hizo simu zote mbili zipoje?
Ile Xiaomi 12T Pro nilinunua ikiwa mpya kwa 1.2 Million. Lakini sasahivi unapata used kwa 550K, sijajua mpya itakuwaje bei maana ni simu ya 2022 kama sikosei, miaka 4 imepita
Hii Google Pixel 7A nimenunua used kwa 430,000/=, lakini ni kama mpya tu
 
Dah dunia imeharibika sana, hadi akina mwakasege wameanza wizi 😂
Mbona wanaiba vizuri tu 😀
Mwaka jana kuna mshikaji wangu alikabwa akaibiwa simu, aliponisimulia nikawa namwambia ni mzembe, unawezaje kuibiwa Mbeya hii. Kumbe nilikuwa naongea vitu sivijui.
Sasa kama mimi wananitolea hadi bisibisi ili niwape vitu vyangu, nikaamua kutoresist so it only took a short time. Maisha yangu ni bora kuliko Xiaomi model yoyote ile
 
Mbona wanaiba vizuri tu 😀
Mwaka jana kuna mshikaji wangu alikabwa akaibiwa simu, aliponisimulia nikawa namwambia ni mzembe, unawezaje kuibiwa Mbeya hii. Kumbe nilikuwa naongea vitu sivijui.
Sasa kama mimi wananitolea hadi bisibisi ili niwape vitu vyangu, nikaamua kutoresist so it only took a short time. Maisha yangu ni bora kuliko Xiaomi model yoyote ile
Inabidi uanze kutembea na Biblia, wakiiona tuu wanakuacha na Bwana Yesu asifiwe juu 😂
 
Kwa hiyo hii Xiami 12T Pro ndiyo ilikuwa Flagshid ya Xiami kwa 2022 ?
Ilikuwa flagship killer kwa mwaka huo, yani ilikuwa katikati ya midrange na flagship
Flagship yao ya juu mwaka 2022 ilikuwa Xiaomi 13 Pro
 
Used zinakuwaga hazina matatizo madogo madogo?
Hii ya kwangu haina tatizo hata moja, ipo vizuri na wengi walidhani nimenunua simu mpya nilipowaonesha
Ila mind you, mara ya kwanza nilichukua simu used (Pixel 7a) kisha nikarudi home kutumia baada ya kukagua na kuangalia kioo kwa ukaribu nikaona OLED burn in (Yani Kuna maandishi yapo kwenye kioo kwa mbali na hayatoki, kwa haraka huyaoni ila ukitaka kuyaona weka wallpaper nyeupe ndio unayaona) nikarudisha simu dukani
Kisha wakazimwaga Pixel 7A mezani nikaanza kukagua vizuri kwa umakini sana ndio nikapata hii niliyokuwa nayo sasahivi ambayo ni nzima kwa asilimia 100. Hata ile ya mwanzo ilikuwa nzima ila kasoro yake ni hiyo "OLED burn in"

Ukinunua used kuwa makini na simu utakayochukua, hakikisha unaikagua kiundani
 
Kwa hizo picha; hiyo camera ya pixel 7A ni kali sana
Ina high definition kama Iphone 14
Kama vitu vingine vipo sawa basi ni simu nzuri
Of course mkuu, kiujumla ni simu nzuri sana
Nilifanya research kabla ya kununua nikaona reviews zake nyingi ni positive. Hii hata haina tofauti na ile Xiaomi 12T Pro niliyokuwa nayo. Ipo perfect, nimeipenda
 
Back
Top Bottom