Nimeibiwa kwenye kituo cha kuuzia mafuta ya petrol Morogoro

Ntemi Kazwile

JF-Expert Member
May 14, 2010
2,182
307
Jana nilikuwa nasafiri kutokea Iringa nilikokuwa nimeenda kikazi, nilipofika Morogoro ikanibidi niingie sheli mojawapo hapo kujaza mawese (Sheli hii iko barabara ya Moro-Iringa kwenye junction na barabara ya Mazimbu).

Nikaomba nijaziwe full tank, kwa sababu najaza hapo mara kwa mara sikuwa na wasiwasi hadi nilipotupa jicho kwenye mita nikaona inaelekea lita 87 (huku gari bado inadai). Kiwango cha juu kabisa ambacho niliwahi kujaza kwenye gari langu ilikuwa ni lita 75 wakati taa ilikuwa imewaka na mshale kugota mwisho. Nilipata mshituko kwa sababu kwanza gari ilikuwa na mafuta yamepungua kidogo tu kwenye robo tank na halafu bado yalikuwa yanaendelea kutiririka (huenda hata 95 zingeingia).

Maswali yangu je kuna chombo chochote kinachowalinda walaji kuhakikisha kuwa hawaibiwa katika vipimo kama ambavyo mimi nimeibiwa jana??

Baada ya kuendelea kutuharibia magari yetu kwa chakachua sasa wanaelekeza nguvu kwenye mita sijui kama hii nchi itaendelea kwa ukesefu wa usimamizi wa sheria kama hivi.

Naomba wakazi wa Morogoro na wasafiri wengine wawe makini na sheli hii, ni hatari
 
Hii petrol station kuna wizi. Nami wiki mbili zilizopitanilifika kituoni hapo kujaza mafuta. Yule petrol attendant akataka kunizubaisha. Alipomaliza kujaza mafuta, akataka nilipe gharama ya mafuta iliyokuwa juu kwa kiasi cha Tsh 15000. Kwa kuwa nilikuwa makini kuangalia kiwango kilichowekwa, ilibidi kupishana na yule jamaa. Hatimaye nililipa kiwango sahihi.

Ni vyema tukawa waangalifu na kituo hiki.
 
Juzi niliwasikia Ewura wakiomba taarifa kama hizo so mkubwa nakuhauri uwatafute!
 
WanaJF nawashauri msijaze kwenye hiki kituo cha TIOT ni cha Barabuu aliyefulia kwa sasa, wale ni wezi na wachakachuaji wa wese wazuri, kajazeni pale Msamvu BP au ingieni ndani hadi hapa Agip opp. na hosp ya mkoa(Morogoro).

Hawa EWURA wameshakula hela hawana meno tena, Ni biashara Holela sio Huria, Bongo zaidi ya uijuavyo.

:dance:
 
Juzi niliwasikia Ewura wakiomba taarifa kama hizo so mkubwa nakuhauri uwatafute!

Contact zao ni zipi mkuu. Mimi ningependa kiripoti hii incidence angalau hata wasipofuatilia nimetimiza wajibu wangu. Iliniuma sana
 
Jana nilikuwa nasafiri kutokea Iringa nilikokuwa nimeenda kikazi, nilipofika Morogoro ikanibidi niingie sheli mojawapo hapo kujaza mawese (Sheli hii iko barabara ya Moro-Iringa kwenye junction na barabara ya Mazimbu).

Nikaomba nijaziwe full tank, kwa sababu najaza hapo mara kwa mara sikuwa na wasiwasi hadi nilipotupa jicho kwenye mita nikaona inaelekea lita 87 (huku gari bado inadai). Kiwango cha juu kabisa ambacho niliwahi kujaza kwenye gari langu ilikuwa ni lita 75 wakati taa ilikuwa imewaka na mshale kugota mwisho. Nilipata mshituko kwa sababu kwanza gari ilikuwa na mafuta yamepungua kidogo tu kwenye robo tank na halafu bado yalikuwa yanaendelea kutiririka (huenda hata 95 zingeingia).

Maswali yangu je kuna chombo chochote kinachowalinda walaji kuhakikisha kuwa hawaibiwa katika vipimo kama ambavyo mimi nimeibiwa jana??

Baada ya kuendelea kutuharibia magari yetu kwa chakachua sasa wanaelekeza nguvu kwenye mita sijui kama hii nchi itaendelea kwa ukesefu wa usimamizi wa sheria kama hivi.

Naomba wakazi wa Morogoro na wasafiri wengine wawe makini na sheli hii, ni hatari

Kwenye pump kuna mahali ukibonyeza inatoa hewa tu so mkuu ulikuwa ukijaziwa hewa.
 
Mi bado nadhani njia nzuri zaidi ni wana jamvi kuvianika vituo vyote ambavyo vina michezo michafu ya namna hii au kuchanganya mafuta. Itawasaidia wengi sana!

Mkuu pole sana, naisukuma hii kwena EWURA tuone kama watachukua hatua zozote
 
...hebu endelea na story!!! hukurusha ngumi??
Mi nisingelipa, na ningeondoka!!

jamani tuwe makini sana!! mi nilishawekewa mafuta ya 30,000/ Iringa oryx badala ya 50,000 niliyosema yawekwe.
Wana-time kama hutoki kwenye gari kuangalia pump, wanaset pump kutoa mafuta kidogo, then unatumia muda mwingi ukifikiri, 50,000 ndo imetumika kumbe 30,000.
 
Pole Mpwa! Naamini EWURA watasikia kilio chako na hatua zitachukuliwa. Mwaka wa uchaguzi huu bana ndio wakati wa wananchi kutatuliwa matatizo yao
 
Jana nilikuwa nasafiri kutokea Iringa nilikokuwa nimeenda kikazi, nilipofika Morogoro ikanibidi niingie sheli mojawapo hapo kujaza mawese (Sheli hii iko barabara ya Moro-Iringa kwenye junction na barabara ya Mazimbu).

Nikaomba nijaziwe full tank, kwa sababu najaza hapo mara kwa mara sikuwa na wasiwasi hadi nilipotupa jicho kwenye mita nikaona inaelekea lita 87 (huku gari bado inadai). Kiwango cha juu kabisa ambacho niliwahi kujaza kwenye gari langu ilikuwa ni lita 75 wakati taa ilikuwa imewaka na mshale kugota mwisho. Nilipata mshituko kwa sababu kwanza gari ilikuwa na mafuta yamepungua kidogo tu kwenye robo tank na halafu bado yalikuwa yanaendelea kutiririka (huenda hata 95 zingeingia).

Maswali yangu je kuna chombo chochote kinachowalinda walaji kuhakikisha kuwa hawaibiwa katika vipimo kama ambavyo mimi nimeibiwa jana??

Baada ya kuendelea kutuharibia magari yetu kwa chakachua sasa wanaelekeza nguvu kwenye mita sijui kama hii nchi itaendelea kwa ukesefu wa usimamizi wa sheria kama hivi.

Naomba wakazi wa Morogoro na wasafiri wengine wawe makini na sheli hii, ni hatari

1.inawezekana muuzaji wakati anakuwekea hakuset pump at 00.00 so alianzia wakati pump inasema 15litres[may be]
2.inategemea una gari gani,lingine linawaka taa[warning] lkn mafuta yanakuwa mengi so siku ulipoweka lita 75 level haikuwa chini kama hii siku ingine ''ulivyoibiwa''

WABONGO acheni umwinyi shikeni pump jazeni mafuta wenyewe msiwachie hao wezi wawaibie kirahisi.....huku kijijini unajaza mafuta mwenyewe then unaenda kulipa.
 
Hii sheli ni mpya inaitwa Petro. Nilikasilika na yule dada aliyekuwa ananijazia alijua kabisa kwamba ameniibia kwani nilipokuwa nalalamika alikuwa na guilty consious lakini kwa kuwa sikuwa na namna ya kuthibitisha kuwa nimeibiwa nililazika kulipa, kwa shingo upande! EWRA basi wasichuke fees bila kutoa huduma kwa sababu nasikia kwenye kila lita wana mkwanja wao.
 
Mi bado nadhani njia nzuri zaidi ni wana jamvi kuvianika vituo vyote ambavyo vina michezo michafu ya namna hii au kuchanganya mafuta. Itawasaidia wengi sana!

Mkuu pole sana, naisukuma hii kwena EWURA tuone kama watachukua hatua zozote

Invisible mi naanza,hapa moro viko kadhaa.Hicho cha TIOT iringa road karibu na njia ya kwenda Mazimbu, Kingine kipo mita chache toka keep left ya SUA kama unaenda SUA, Kingine ni TIOT iringa road njia panda ya kuingia mjini toka mzumbe, Hapa Oilcom karibu na mjimpya nao siku moja moja mafuta yao sio mazuri, pia na hiki kilichopo opp na CRDB mandela branch kinawalakini, Kwa moro sana sana ni hivyo, ila TIOT ni vituo namba moja vinavyochakachua wese na kwa bahati mbaya viko highway kama pale nane nane na kingulwira. EWURA mpoooooooooo? Chukueni hatua za kisheria sio kuchukua hela tu.
 
Mi bado nadhani njia nzuri zaidi ni wana jamvi kuvianika vituo vyote ambavyo vina michezo michafu ya namna hii au kuchanganya mafuta. Itawasaidia wengi sana!

Mkuu pole sana, naisukuma hii kwena EWURA tuone kama watachukua hatua zozote


hio ndio dawa yao mkuu.........kuvianika na kuwatangazia watu wawe makini wakienda kuweka mafuta huko.......
 
1.inawezekana muuzaji wakati anakuwekea hakuset pump at 00.00 so alianzia wakati pump inasema 15litres[may be]
2.inategemea una gari gani,lingine linawaka taa[warning] lkn mafuta yanakuwa mengi so siku ulipoweka lita 75 level haikuwa chini kama hii siku ingine ''ulivyoibiwa''

WABONGO acheni umwinyi shikeni pump jazeni mafuta wenyewe msiwachie hao wezi wawaibie kirahisi.....huku kijijini unajaza mafuta mwenyewe then unaenda kulipa.

Mkuu hata ukishika pampu mwenye haisaidii. Na kumbuka kuwa gari hili ninalo tangia 2006 na kuna nyakati si moja ambayo nimejaza wakati mafuta yakiwa yameisha kabisa na sijawahi hata siku moja kufikisha lita 80!!!!
 
Mimi nawashauri wanaJF pamoja kwamba tunaibiwa ukiwa unaweka mafuta sehemu yoyote shuka kwenye gari uangalie anavyoweka.

Usimuruhusu kubonyeza kwa nguvu mwembie aweke taratibu. Akiweka kwa speed badala ya kukuwekea 20,000 anakuwekea 10,000
 
1.inawezekana muuzaji wakati anakuwekea hakuset pump at 00.00 so alianzia wakati pump inasema 15litres[may be]
2.inategemea una gari gani,lingine linawaka taa[warning] lkn mafuta yanakuwa mengi so siku ulipoweka lita 75 level haikuwa chini kama hii siku ingine ''ulivyoibiwa''

WABONGO acheni umwinyi shikeni pump jazeni mafuta wenyewe msiwachie hao wezi wawaibie kirahisi.....huku kijijini unajaza mafuta mwenyewe then unaenda kulipa.

Underlined hapo umenena mkuu
 
WABONGO acheni umwinyi shikeni pump jazeni mafuta wenyewe msiwachie hao wezi wawaibie kirahisi.....huku kijijini unajaza mafuta mwenyewe then unaenda kulipa.

Ni petrol stesheni gani bongo hii watakupa pump ujaze mwenyewe? hapa dar sijaona hata moja.........! Ukichangia sometimes changia kibongo bongo kwa ku-reflect hali halisi mkuu
 
Mimi nawashauri wanaJF pamoja kwamba tunaibiwa ukiwa unaweka mafuta sehemu yoyote shuka kwenye gari uangalie anavyoweka.

Usimuruhusu kubonyeza kwa nguvu mwembie aweke taratibu. Akiweka kwa speed badala ya kukuwekea 20,000 anakuwekea 10,000
KoK,

Umenifanya nishtuke. Kama ni hivyo basi wengi wanalizwa bila kujua!
 
Tabia ya kutokulipa fweza kwa watumishi kihalali. Kama wafanyakazi wangelipwa kwa haki hao waweka mafuta wasingekuwepo, wapo kwa sababu serikali imeshindwa kuona haki inatendeka kuweka kiwango cha mshahara kinachoendana na maisha. Aibu kwa serikali ya JK na Chama Cha Majambazi.
 
Back
Top Bottom