Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Jana nilikuwa nasafiri kutokea Iringa nilikokuwa nimeenda kikazi, nilipofika Morogoro ikanibidi niingie sheli mojawapo hapo kujaza mawese (Sheli hii iko barabara ya Moro-Iringa kwenye junction na barabara ya Mazimbu).
Nikaomba nijaziwe full tank, kwa sababu najaza hapo mara kwa mara sikuwa na wasiwasi hadi nilipotupa jicho kwenye mita nikaona inaelekea lita 87 (huku gari bado inadai). Kiwango cha juu kabisa ambacho niliwahi kujaza kwenye gari langu ilikuwa ni lita 75 wakati taa ilikuwa imewaka na mshale kugota mwisho. Nilipata mshituko kwa sababu kwanza gari ilikuwa na mafuta yamepungua kidogo tu kwenye robo tank na halafu bado yalikuwa yanaendelea kutiririka (huenda hata 95 zingeingia).
Maswali yangu je kuna chombo chochote kinachowalinda walaji kuhakikisha kuwa hawaibiwa katika vipimo kama ambavyo mimi nimeibiwa jana??
Baada ya kuendelea kutuharibia magari yetu kwa chakachua sasa wanaelekeza nguvu kwenye mita sijui kama hii nchi itaendelea kwa ukesefu wa usimamizi wa sheria kama hivi.
Naomba wakazi wa Morogoro na wasafiri wengine wawe makini na sheli hii, ni hatari
Nikaomba nijaziwe full tank, kwa sababu najaza hapo mara kwa mara sikuwa na wasiwasi hadi nilipotupa jicho kwenye mita nikaona inaelekea lita 87 (huku gari bado inadai). Kiwango cha juu kabisa ambacho niliwahi kujaza kwenye gari langu ilikuwa ni lita 75 wakati taa ilikuwa imewaka na mshale kugota mwisho. Nilipata mshituko kwa sababu kwanza gari ilikuwa na mafuta yamepungua kidogo tu kwenye robo tank na halafu bado yalikuwa yanaendelea kutiririka (huenda hata 95 zingeingia).
Maswali yangu je kuna chombo chochote kinachowalinda walaji kuhakikisha kuwa hawaibiwa katika vipimo kama ambavyo mimi nimeibiwa jana??
Baada ya kuendelea kutuharibia magari yetu kwa chakachua sasa wanaelekeza nguvu kwenye mita sijui kama hii nchi itaendelea kwa ukesefu wa usimamizi wa sheria kama hivi.
Naomba wakazi wa Morogoro na wasafiri wengine wawe makini na sheli hii, ni hatari